SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kumekuwepo na madai kuwa ulaji wa ugali hudumaza akili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?

02692B18-05FE-4851-857F-7A5DA6E174CD.jpeg
 
Tunachokijua
Ugali ni chakula kinachotumika sana Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kwa mujibu wa utafiti wa Onu Okpa et al (2019), “Sub-Saharan African Maize-Based Foods - Processing Practices, Challenges and Opportunities” mahindi huchangia 30% ya nishati za vyakula wanavyotumia watu wa ukanda huu kila siku.

Kwa mujibu wa utafiti huu, kila mtu anayepatikana Kusini mwa Jangwa la Sahara hutumia wastani wa kati ya gramu 52-450 za mahindi kwa siku. Ni chanzo kikuu cha ugali unaotumika kila siku kwenye nchi hizi. Kwa Tanzania, 64% ya wananchi wake hula chakula hiki walau mara 5-7 kwa wiki.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa ugali ni chakula kinachotumika sana, pengine kuliko aina nyingine za vyakula. Baadhi ya watu huutengeneza kwa kutumia unga wa mhogo, mtama, ulezi pamoja na aina zingine za nafaka.

Bila kujali tofauti ndogo za mgawanyiko wa virutubisho, nafaka zote husifika kwa kuwa na kiasi kikubwa cha nishati na wanga, pia kiasi kidogo cha madini na vitamini muhimu kwa afya.

Kuhusishwa na udumavu wa akili
Kitaalamu, udumavu wa akili husababishwa mambo mengi ikiwemo baadhi ya changamoto za kijenetiki mfano Down’s syndrome, kukosa hewa ya kutosha wakati wa kuzaliwa, maambukizi makali ya homa ya uti wa mgongo, utapiamlo, matumizi ya baadhi ya madawa na pombe wakati wa ujauzito pamoja na sababu zingine siziso wazi sana.

Kwa kurejea mgawanyiko wa virutubusho vinavyopatikana kwenye nafaka zinazotumika kutengenezea ugali, hakuna uhusiano wa moja kwa moja unaoweza kutajwa, au pia kuhusishwa na kusababisha udumavu wa akili kwa watu. Virutubisho na madini yake havina athari hasi kwenye afya ya ubongo.

Pia, JamiiForums imezungumza na wataalamu wa lishe ambao wamethibitisha kuwa chakula hiki ni salama, hakiwezi kusababisha madhara tajwa.

Hivyo, JamiiForums imebaini kuwa madai haya hayana ukweli uliojengwa kwa hoja za kisayansi. Ni uzushi usio na uthibitisho wa tafiti au takwimu.
Katika hoja hii ukweli upo kwa asilimia furani, kwamba ugali unachangia ufahamu kuwa finyu. Siyo ugali tu hata mikate hii mweupe, na hata chai ya rangi pia.
Ugali wa mahindi hasa hizi sembe, mikate mweupe, yaani ngano iliyo kobolewa, majani ya chai, maharage, vyote hivi vina asili furani ya ulevi. Kama unabisha kula ugali wa sembe na maharage, lazima ndani ya dakika furani kunauchovu unaupa.

Kunywa chai ya rangi na mkate, nakuhakikisha kuna uchovu lazima utaupa. Kwa kifupi huo uchovu ndiyo unadumaza ufinyu wa kufikili.

Ndiyo maana tunashauliwa tule matunda na mboga mboga za majani kila wakati, angalau kuupa ufahamu nguvu.

Tuelewe kitu chochote kinacho leta ulevi/uchovu huwa ni adui wa ufahamu. Ndiyo maana tukifanya kazi tukachoka inabidi tupumzike kwa muda furani ili kuupa ufahamu nguvu tena.

Baadhi ya nchi zilizo endelea hazili kabisa ugali na vyakula ambavyo hupelekea kulegeza ufahamu.
Mfano kwa Africa ni Nigeria & Ghana, hizi nchi ni nadra kukuta mtu anakula Ugali wa mahindi, na kama ukiukuta ugali wao lazima kuna vitu wamevichanganya ili kufanya ugali huo kutokufanya ufahamu uchoke.
Ndiyo maana Nigeria inaogopeka sana duniani kote, maana watu wao wanaakili nyingi mno.

Kwa Africa bado tunahitaji elimu ya chakula ili tuweze kujenga afya za fahamu na miili yetu.
Mtu mwenye afya njema si yule aliye nenepa bali mwenye ufahamu wa kufikili haraka.
 
Katika hoja hii ukweli upo kwa asilimia furani, kwamba ugali unachangia ufahamu kuwa finyu. Siyo ugali tu hata mikate hii mweupe, na hata chai ya rangi pia.
Ugali wa mahindi hasa hizi sembe, mikate mweupe, yaani ngano iliyo kobolewa, majani ya chai, maharage, vyote hivi vina asili furani ya ulevi. Kama unabisha kula ugali wa sembe na maharage, lazima ndani ya dakika furani kunauchovu unaupa.

Kunywa chai ya rangi na mkate, nakuhakikisha kuna uchovu lazima utaupa. Kwa kifupi huo uchovu ndiyo unadumaza ufinyu wa kufikili.

Ndiyo maana tunashauliwa tule matunda na mboga mboga za majani kila wakati, angalau kuupa ufahamu nguvu.

Tuelewe kitu chochote kinacho leta ulevi/uchovu huwa ni adui wa ufahamu. Ndiyo maana tukifanya kazi tukachoka inabidi tupumzike kwa muda furani ili kuupa ufahamu nguvu tena.

Baadhi ya nchi zilizo endelea hazili kabisa ugali na vyakula ambavyo hupelekea kulegeza ufahamu.
Mfano kwa Africa ni Nigeria & Ghana, hizi nchi ni nadra kukuta mtu anakula Ugali wa mahindi, na kama ukiukuta ugali wao lazima kuna vitu wamevichanganya ili kufanya ugali huo kutokufanya ufahamu uchoke.
Ndiyo maana Nigeria inaogopeka sana duniani kote, maana watu wao wanaakili nyingi mno.

Kwa Africa bado tunahitaji elimu ya chakula ili tuweze kujenga afya za fahamu na miili yetu.
Mtu mwenye afya njema si yule aliye nenepa bali mwenye ufahamu wa kufikili haraka.

Ati Afrika tunahitaji elimu ya Chakula.
Una matatizo sehemu. Kwasababu....unataka kulazimisha madai ambayo tayari yalishwa tolewa ufafanuzi; Ulaji Ugali haudumazi akili.
Sijui ulikula nini kuja kuyasema hayo uliyoyasema. Baga?
 
Mimi hula ugali sana na sidhani kama kweli akili yangu imedumaa. Aaliyeleta madai hayo tuje tupimwe IQ zetu kama yeye atakuwa na IQ kubwa kuliko mimi. Mimi ni shabiki wa jamaa huyu

View attachment 2638430
Muinjilisti na mhubiri Lemma wa CHADEMA ndiye aliyenukuliwa. Hatahivyo, kuna genge lililo shikilia bango suala hili kwa lengo la kufedhehesha tu. Shaming. Ni lugha ya wakimbari. Racist and Bigoted.
Watashindwa na walegeee!
 
kitu cha TMK hakijawahi kuwaacha watu salama yaani watu ugali unaleta udumavu ooooohhhh NOOOOOO uongo kabisaaa
 
Watu wengi wanaamini ugali ndio chakula pekee cha kuupa mwili nguvu na afya njema lakini si kweli

Ugali ni mlo hatari ni kama sumu ndio maana hata wanyama wachoyo kama mbwa, nguruwe, paka, nk. Hawana akili lakini katu huwakuti wakila ugali maana ni chakula kisicho na nutrients zozote mwilini.

Hapa Tanzania jamii na makabila makabila makubwa hatupendelei ugali mfano sisi watu wa mkoa wa Kagera, Moshi(wachaga) na Mbeya hawali ugali lakini Tanzama mikoa duni kama Dodoma, Singida, Lindi, na watu wa Pwani wala ugali

Wenzetu wamataifa mengine wana afya afya na wala hawajui ugali ni nini Tazama wenzetu kutoka west Africa hawali maugali kama Watanganyika wana body zimejengeka.

Waganda, Wakenya, Wanyarwandwa hawali ugali. Mtu ukila ugali kwanza unalewa kama umepiga jibapa la Konyagi masaa mawili, ukila ugali wa Mara digestion ni ngumu mwilini chakula hakushuki hupati choo siku mbili, sasa hicho chakula au uchafu tu.

Wazungu na warabu wako vizuri kiafya wala hawayajui maugali ni nini wao wanajilia ngano, wali, nyama na maziwa, sisi Watanganyika kutwa usiku tunakula maugali na milenda kama tumerogwa

Madhara ya ugali kwa watu wetu, tumekosa washiriki wazuri kwenye michezo yani leo umpeleke Kibwana amkabe Sadio Mane AFCON haiwezekani.

Watoto hawana akili mashuleni wapo tu wamechoka yaani wamelewa chakali shuleni hawaewi kisa kula maugali.

Miili kama midogo kama digidigi unakuta mwanaume Dar anavamiwa na panya road anajificha kisa kula maugali

Sipendi ugali nakushauri usije ukala haya sumu ya akili na mwili ugali ni sumu kali

Nikiwa Rais nitapiga marufuku ugali

#kataa ugali Mtanganyika
 
Na ukisoma historia zinadia kuwa kabla ya wakoloni kuja Afrika, Afrika haikuwa na utamaduni wa kula ugali.

Kwa hiyo ujio wa wakaloni ndio mwanzo wa ugali.

Kabla ya wakoloni Afrika ilikuwa na wazee timamu sana kwenye kichwa ila hayo yote yalikuja ku change ghafla baada ya ugali kuwasili.

Ukifanya tafakuri ya kina utaona wakoloni walitumia ugali kama bio weapon ya kuwadhoofisha wazee wetu kiakili.

Na sehemu wakoloni waliyokuja kumaliza mchezo kwa kuwavuruga akili mazima wazee wetu ni pale walipoingia porini kutafuta majani yanayoteleza na kuyapa jina la mlenda na kufanya hiyo ndio combinations bora ya mlo wa ugali.

Baada ya hapo ndio tumefikia hapa tulipo kila mtu amepoteana, tumekata ringi hatuna dira.

And sometimes if we're being honest, we gotta admit to speak the truth, that the world is better off without us.
 
Sina uhakika kuhusu faida za ugali mwilini, ila umedanganya kuhusu mataifa mengine kula ugali. Africa nzima chakula kikuu ni ugali kama unasema Nigeria, Ghana, Cameroon na west kwa ujumla hawali ugali basi inaonekana hujasafiri kwenda popote. Halafu hujui hata Corn flakes, pop corn 🌽 wanazobugia wazungu ni mahindi hayohayo tofauti ni mbeguna mapishi tu?.. kama ugali ungekuwa na shida yoyote basi hata shuleni na vyuoni kusingekuwa na wakufunzi, maana wote wamelelewa na ugali na maharage. Sema nini, unaonekana una ulimbukeni fulani hivi..
 
Back
Top Bottom