Ambokile Amanzi
JF-Expert Member
- Dec 12, 2018
- 965
- 1,333
- Thread starter
-
- #21
Unaandika mambo meeeeengii... ujinga mtupu! — Kuandika kwenyewe hujui.Dunia ya sa hv kingereza ni lazima ukijue tena vizur ..tusijidanganye kabisa ..... Kwa Kenya haina shida wale ni waswahili Tu fresh , lakn zaidi ya yote kingereza ni lazima ukijue ili utoboe ....hyo ni international language..acheni ujinga wa jiwe wa kujifungia ndani na kuwakomoa wananchi wake na mikodi ya ajabu ajabu alaf hela zianenda kwenye midege huko mnabaki mnashindia majani ya michicha na ugali
Unateseka sana mkulungwa, pole lakini. Kuna matumaini madogo sana kwa watu wa aina yako. Punguza chuki binafsi na kulia lia kisa humuelewi mazza.Wewe nina uhakika hata Kizungu kikizungumzwa huna uwezo wa kukielewa.
Unabaki na zile you know zea zea.. ofkozii.
Jikite na Kiswahili bwana mdogo. Usijitutumue.
Mwisho ya wapi?
Yamefanyaje?Maswala vs Masuala….
Nina uhakika kuwa umahiri wangu wa kuzungumza Kiingereza ni mara mia mbili zaidi yako.Kwanza, English haikwepeki dunia hii, jifunze tu kama huwezi utaishi sana kwa stress.
Pili, Rais Samia hajasema atahutumia Kiingereza au Kiswahili tayari wewe umemhukumu na kuja na upumbavu wako.
Kama hujui, Kikwete amewahi kuhutubia bunge la Kenya na alitumia Kiswahili.
TakatakaNina uhakika kuwa umahiri wangu wa kuzungumza Kiingereza ni mara mia mbia zaidi yako.
Sibabaiki kwa sababu ninakijua vilivyo.
Kwahiyo usinitishe tishe hapa bwana mdogo.
Haswaaaaa!ningependa Bi Mkubwa atumie Kiswahili!
hua nafurahi sana nikiona viongozi mbali mbali wa asia hasa wa Kichina wakitumia lugha yao.
Lugha yenyewe watz wengi siku hizi ni shida, hata afadhali kule Mombasa Kenya wanatushinda,,tumebaki na kiswahili cha mitaani kisicho rasmi...Mama wewe soma hotuba ya kiingereza tu ujiondokee...Hii lugha ya kiswahili haina soko. Kwasabb ilipaswa kubeba teknolojia/maarifa ambayo ndiyo yangevutia watu kujifunza kiswahili
Lazima lugha inayotumiwa iakisi "hadhira pana" inayolengwa.Uganda siku ile, pamoja na waganda kukijua kiswahili lakini hadhira ile ilihusisha pia na wawekezaji wa bomba la mafuta ambao hawajui kiswahili bali kiingereza, kuna sababu gani kulazimisha kiswahili kama Magufuli aliyekuwa hajui hiyo lugha nyingine?
Weye ni msukuma AmbokileHaswaaaaa!
Flexible ndio nini?huyu yupo flexible,jiwe hakujua kingereza
Kweli wewe ni Bunsen Burner.Mama wewe soma hotuba ya kiingereza tu ujiondokee...
Ujue pia akiwa pale Nairobi bungeni atakua haongei na wakenya pekee, balianaongea na jumuiya ya kimataifa kupitia bunge la Kenya. Peleka watoto shule waweze kupambana duniani mkuu.Uganda akiongea Kiingereza, sawa tu manake wale jamaa wana bifu na Kiswahili!!
Kenya, kwa kuwakomoa tu, anapaswa atumie Kiswahili manake Kiswahili wanakijua vizuri lakini kutokana na ulimbukeni wao wa kumsujudia Mzungu, wanajifanya hawakijui!!
Kwa Uganda pale unadhani kuna mtu hakumuelewa? Pengine angeongea kiswahili ndio wengine wasinge muelewaLazima lugha inayotumiwa iakisi "hadhira pana" inayolengwa.
Hao unaowaita wawekezaji walikuwa hawazidi hata kumi.
Lakini kulikuwa na maelfu ya wananchi ambao walihitaji kusikia mambo yakizungumzwa kwa Kiswahili.
"Muktadha". Zingatia sana.
Ukitaka kuendelea kuonekana kituko kwenye nchi za Commonwealth endelea kuongea Kiswahili.Tumesikia Bi. Samia anaenda Kenya kwa ziara ya kikazi mnamo hapo kesho.
Ni matumaini yangu na fahari yangu kwamba atatumia Kiswahili katika shughuli zote atakazoalikwa kuzifanya.
Hivi majuzi tu alipoenda Uganda, tuliona anatumia kizungu kuhutubia.
Wengi wa wananchi wetu nina uhakika hawakuelewa hata anachozungumza.
Ifahamike kwamba, Kiswahili si lugha ngeni Afrika Mashariki. Tuachane na Viingereza pasipo na ulazima.
Sijui ni nani aliyewalaghai kwamba kuongea kizungu ni ufahari na usomi?
Hata katika mazingira yasiyohitaji kizungu, bado watu watajing'ang'aniza kuongea kizungu hata kama hawakiwezi na tunajua kwa hakika kwamba hawakiwezi.
Hebu tuachane na hizi "You Know You know ofcozi zea zea" mingi mingi. Tunajiaibisha na kujidunisha.
Tunayo lugha adhimu ya Kiswahili. Tuitumie hiyo.
Nasubiri kuona hiyo Kesho vile Bibi SASHA atakavyojitutumua na viingereza vyake uchwara.
Ashauriwe vyema. Maana shughuli za aina ile sio mahali pa kuonesha mbwembwe za kuzungumza kwa lafudhi bandia za kimalkia.
Tunahitaji kusikia "maswala" yakijadiliwa na kuzungumzwa. Hatuhitaji mikogo ya lafudhi bandia za Kizungu.
Walakini uko wapi hapo?
Hebu nioneshe.
Ujue pia akiwa pale Nairobi bungeni atakua haongei na wakenya pekee, balianaongea na jumuiya ya kimataifa ..