Ulianzaje kukaa gheto?

Ulianzaje kukaa gheto?

bora kupika, ila sio kuosha vyombo

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
Kuosha vyombo ni mtihani mkubwa kwetu sote[emoji2][emoji2]

Huwa naosha hadi nikipika tena[emoji2][emoji2][emoji1787][emoji1787] ila havipiti siku moja vikiwa vichafu

Au naweza viosha halafu vikakaa wiki nzima bila kutumika nagongea takeaways au mama nijazie sometimes.
 
Ukitaka usiwe mvivu wa kuosha vyombo baada ya kupika fanya hivi ÷

Kwanza; usiwe na vyombo vingi ghetto, uwe na vichache vya muhimu tu.

Pili; ukiwa unapika kila chombo ambacho hakina matumizi baada ya kumaliza kazi yake hakikisha unakiosha au unakisuuza na kuirudisha mahali pake.

Mpaka unamaliza kupika utajikuta huna chombo hata kimoja kichafu isipokuwa ulivyopikia na utakavyotumia wakati wa kula. Hivi haviwezi kukutia uvivu kuosha maana ni vichache.

Kwanini nasema uwe na vyombo vichache, kwanza siyo hulka mwanaume ghetto kwake kuwe na vyombo vingi vya kupikia hii ni kazi ya wanawake.

Ukiwa na vyombo vingi vitakufanya uwe unatumia tumia tu maana unavyo vingi na unaona uvivu wa kuosho vichafu.

Sasa hii itakukusanyia vyombo vingi vichafu na vitakutia uvivu wa kuosha na hutapika, bajeti yako utaivuruga kwenda kula nje wakati kila kitu unacho ndani.

Wengine husema kwa kuwa yupo dada wa jirani au mwenye nyumba nitamuita aje anioshee, kosa la kiufundi hapa unafanya. Utaoa/kuozeshwa kabla ya muda wako.

Kuoa/kuolewa huwa siyo umri bali ni utayari wa mtu kwamba anaingia kwenye majukumu haya. Usiige kila mtu ana akili zake jinsi ya kuishi kwenye ndoa.

Kuna vijana tulianza wote maisha wakawahi kuoa, mwaka juzi nakutana nao wanasema bora wasingeoa mapema wanasema angalau sasa hivi ndio wangeoa ili wawe wamejijenga zaidi kimaisha.

Wanaume wengi huamua kuoa mapema baada ya kuchoshwa na kuosha vyombo na kupika, Tumia hiyo njia kwanza,chakula cha kujipikia ni bora na ni afya zaidi kuliko cha nje.
Nakubali mkuu
 
So kupitia mimi hope mtajifunza vijana wenzangu kuwa endapo utalitumia vizuri basi hakika maisha yak yatabadilika.pia la mwisho ni kumtafuta mwenza mwenye maono ila uiangukia kwa kwa hawa makahaba wa mjini utaishia kuhangaika mwisho wa siku unarudi nyumbani ukiwa na miaka 40,bila kufanya lolote
Jerrybanks
Sikuwahi kutilia maanani sana huu uzi. Lakini kwa mara ya kwanza nimekutana na kitu. Link nilitumiwa na member wa jf mwaka juzi, lakini Leo baada ya kukosa cha kufanya nikaona niingie hapa. Mbarikiwe, naamini hadi kufika mwisho nitakuwa nimetoka na kitu.
 
Nipo mkoa mmoja wenye baridi nyanda za juu kusini, nipo geto hapa godoro tu nimeliweka chini pamoja na jiko la gesi la kupikia, maisha yanasonga mdogomdogo.
Komaa utatoboa. Ila chini ya godoro hakikisha unaweka mkeka chini ili lisije likapitisha unyevu ukakuathiri kiafya siyo mzuri. Mambo yakikaa sawa nunua kitanda kabisa usilale chini muda mrefu.
 
Sikuwahi kutilia maanani sana huu uzi. Lakini kwa mara ya kwanza nimekutana na kitu. Link nilitumiwa na member wa jf mwaka juzi, lakini Leo baada ya kukosa cha kufanya nikaona niingie hapa. Mbarikiwe, naamini hadi kufika mwisho nitakuwa nimetoka na kitu.
Hapa ni kisima cha maarifa mkuu. Ukisoma comments zote kuanzia juu unajikuta umeshapata ujasiri wa kupambana bila kukata tamaa. Karibu sana.
 
Kipoozo cha stress...

Kesho navuta showcase kaliii + 32' flat screen.

Getto
IMG_20220526_142606.jpg
 
Natoroka kulipa bili nakimbilia kwa mshkaji wangu nakutana na mshkaji wangu naye anatoroka kulipa bili anakuja kwangu.

Tukaenda zetu kukaa baharini kuanzia asubuhi mpaka saa nne usiku tukaenda kulala kwa mshkaji wetu mwingine na ndiyo tumeamka hapa.
 
Natoroka kulipa bili nakimbilia kwa mshkaji wangu nakutana na mshkaji wangu naye anatoroka kulipa bili anakuja kwangu.

Tukaenda zetu kukaa baharini kuanzia asubuhi mpaka saa nne usiku tukaenda kulala kwa mshkaji wetu mwingine na ndiyo tumeamka hapa.

[emoji23][emoji23]afu si ulisema una watoto 3 hukai nao ?
 
Back
Top Bottom