Cecil J
JF-Expert Member
- Oct 12, 2023
- 434
- 1,024
Kuna siku moja tukiwa tunarejea nyumbani baada ya masomo kipindi hicho nipo O-level, ulikuwa msimu wa mahindi bado mwezi kama mmoja kuanza kukomaa. Njia tuliyopita ilikuwaa na mashamba mengi ya mahindi, rafiki zangu watatu walisogelea shamba na kuvunja mihindi kwa ajili ya migagi (ina radha kama miwa kwa mbali), baada ya hapo mimi kama mla doria nikawa nawapa ishara, baada ya dakika kama mbili hivi walitoka jamaa wawili wanakimbia kutoka upande wa ndani wa shamba wanawafuata wadau waliokuwa wanavunja mahindi.
Ili kuepuka kesi mimi na jamaa mmoja ambaye alikuwa ameshika mabegi ya rafiki zetu waliozama ndani wala hatukukimbia tulikaa kimya tu. Jamaa wale wawili walikuwa wanachomoka kama mshale kuwasaka wale wash' kaji zetu.
Baada ya kukimbizana kwa muda mrefu walifanikiwa kuwakaribia na kuwakalili majina yao kwakuwa walikuwa wakikaa nao mtaa mmoja.
Fast forward Jumatatu imefika majira ya mapumziko iligongwa Kengele wote tukaitwa Assembly ground. Nilipoangalia mbele namuona mwalimu wa nidhamu, jamaa fulani mkaksi levo ya mwisho. Huyu alikuwa akifahamika kwa jina la Mboya, mtaalamu wa Geography.
Wale jamaa waliokaririwa majina yao waliitwa mbele, ghafla waliokuja kushtaki wakadai walikuwepo na watu wengine. Mwalimu akawaruhusu jamaa waje kufanya scanning mstari kwa mstari, hio ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuwa kama James Bond, alikuwa akienda mbele narudi nyuma akianza kuangalia nyuma naanza kufunga kamba za viatu 😂😂😂
Baada ya kutokuniona mimi na yule jamaa mbeba mabegi ambaye alikimbilia chooni mwamba alirejea mbele na kuanza kuangaza.
Jamaa zetu walibebeshwa mahindi yote ambayo yalikuwa ya.evunjwa kule shambani. Tulikuja kujua kwamba lile lilikuwa shamba la kanisa, na hao jamaa waliokuwa wakikimbiza rafiki zetu ndio waliokuwa walinzi wa shamba.
Ili kuepuka kesi mimi na jamaa mmoja ambaye alikuwa ameshika mabegi ya rafiki zetu waliozama ndani wala hatukukimbia tulikaa kimya tu. Jamaa wale wawili walikuwa wanachomoka kama mshale kuwasaka wale wash' kaji zetu.
Baada ya kukimbizana kwa muda mrefu walifanikiwa kuwakaribia na kuwakalili majina yao kwakuwa walikuwa wakikaa nao mtaa mmoja.
Fast forward Jumatatu imefika majira ya mapumziko iligongwa Kengele wote tukaitwa Assembly ground. Nilipoangalia mbele namuona mwalimu wa nidhamu, jamaa fulani mkaksi levo ya mwisho. Huyu alikuwa akifahamika kwa jina la Mboya, mtaalamu wa Geography.
Wale jamaa waliokaririwa majina yao waliitwa mbele, ghafla waliokuja kushtaki wakadai walikuwepo na watu wengine. Mwalimu akawaruhusu jamaa waje kufanya scanning mstari kwa mstari, hio ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuwa kama James Bond, alikuwa akienda mbele narudi nyuma akianza kuangalia nyuma naanza kufunga kamba za viatu 😂😂😂
Baada ya kutokuniona mimi na yule jamaa mbeba mabegi ambaye alikimbilia chooni mwamba alirejea mbele na kuanza kuangaza.
Jamaa zetu walibebeshwa mahindi yote ambayo yalikuwa ya.evunjwa kule shambani. Tulikuja kujua kwamba lile lilikuwa shamba la kanisa, na hao jamaa waliokuwa wakikimbiza rafiki zetu ndio waliokuwa walinzi wa shamba.