Nakumbuka enzo hizo kuchat yahoo messanger. Kulikuwa kunw chatrooms za britney spears sijui madonna mimi nikawa nadhani nachat na britney.
Niaje niaje,
Wadau tukumbushane enzi hizo na matukio yetu ambayo ukiwaza saivi unajiona mshamba fulani hivi.
Nakumbuka nilitoa hela ndefu ili niungwe Facebook, nikiwaza nataman niende Internet Cafe nikamchape yule dada vibao.
Shati yangu ya shule bila kutia blue nilihisi sijatokelezea.
Zamani bwana memories zake zinafurahisha na kusikitisha.
Nilibugia kuberi nikadhani nikahisi chocolate, kichwa kiliuma sana.
Nishawahi lamba mafuta ya Kimbo nikidhani blue band
Wewe unakumbuka jambo gani?
Acha uwongo soda haijawahi badilika, formula ni ile ile hata kabla we hujazaliwa.Soda sh 50
Soda kweli sio hizi za sasa hivi
Iweke hapa hiyo formula ambayo haijawai badilika.a
Acha uwongo soda haijawahi badilika, formula ni ile ile hata kabla we hujazaliwa.
Matokeo yake? ๐kula ada za wazazi.. dah
acha tu mkuu ๐ ๐Matokeo yake? ๐
๐๐๐pole Sanaacha tu mkuu ๐ ๐
,kindungsye ukajiite godofuleiiiKukataa jina langu la jadi na kujiita jina la kizungu.
......na ungefanikisha kubadili jina hadi kwenye documents official, hii kumbukumbu ingekuumiza sana hadi leo.....Kukataa jina langu la jadi na kujiita jina la kizungu.
Kwa nini ulichelewa nawe? Tusimulie vizuri basiNiliambiwa nirudi home saa9 mwisho kulikuwa na mahafali shuleni kwetu mambo yakanoga nikarudi home saa 11 badala ya kuingia ndani nikajificha nyuma ya nyumba namsikia baba ananiulizia mara saa 12 akatoka kunitafuata shule mm nipo pale namuona akipita huku nazungukia upande mwingine akarudi namuona nimejificha tu baba alishindwa kula mama anamwabia kula huyu mshenzi akija ataona ๐๐๐nawasikia tu nipo dirishani had saa 3,saa 4
watu hawajalala wakaanza kunitafuta najificha mama akawaomba majirani mtaani kuwa hawanioni sijarudi majirani wakasema waliniona nyuma ya nyumba nilikimbia balaa wakaanza kunikimbiza kama mwiz๐๐๐
mtaa mzima wameungana nilishikwa nimebebwa juu juu nilichezea kipigo ๐๐๐
Utoto bhana๐๐
๐๐Kulikuwa na graduation wakachelewa kucheza kwaya mgeni rasm alichelewa kuja mie Tena nitaondaje katikat ya shughuli nikasubir had mambo yaelewek nikasahau home Sheria Kali๐๐๐Kwa nini ulichelewa nawe? Tusimulie vizuri basi
Napinga. Ladha ya Cocacola ya mwaka 2009 na ya 2023 sio sawa.a
Acha uwongo soda haijawahi badilika, formula ni ile ile hata kabla we hujazaliwa.
Zamani Coca-cola soda ilikuwa Ina GESI vibaya mno na sukari nyingi kinyama. Yaani enzi hizo ukifanya kosa Haina haja ya kupigwa, unanunuliwa coca tu. Maana walijua ukishamaliza kunywa wakati wa kubeua itakurarua vikali
Niaje niaje,
Wadau tukumbushane enzi hizo na matukio yetu ambayo ukiwaza sasa hivi unajiona mshamba fulani hivi.
~ Nakumbuka nilitoa hela ndefu ili niungwe Facebook, nikiwaza nataman niende Internet Cafe nikamchape yule dada vibao.
~ Shati yangu ya shule bila kutia blue nilihisi sijatokelezea. Zamani bwana memories zake zinafurahisha na kusikitisha.
~ Nilibugia kuberi nikadhani ni chocolate, kichwa kiliuma sana.
~ Nishawahi lamba mafuta ya Kimbo nikidhani blue band.
Wewe unakumbuka jambo gani?
Mm had Sasa siwez Yani lazima itanipalia๐Zamani Coca-cola soda ilikuwa Ina GESI vibaya mno na sukari nyingi kinyama. Yaani enzi hizo ukifanya kosa Haina haja ya kupigwa, unanunuliwa coca tu. Maana walijua ukishamaliza kunywa wakati wa kubeua itakurarua vikali