Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,112
Wakuu,kwanza nikiri wazi kwamba JF siyo tu mtandao wa kupashana habari na kuongeza uwezo wa kujenga hoja kinzani lakini pia,ni moja kati ya sehemu inayonipa raha hata ninapokuwa na stress kutokana na shughuli za kila siku. Leo napenda tuchangie mada hii iliyonifanya nicheke baada ya kutathmini baadhi ya majina ambayo watu wanayatumia hapa JF mfano Mbogo,Popobawa,Gandagumu,Mtimkavu,Mcameroon,kitimoto n.k Binafsi nilipojibatiza jina la Gandagumu ilikuwa ni kuendeleza kumbukumbu ya itikadi ya U-hardcore niliyokuwa nayo sekondari miaka mingi iliyopita.Niliamini katika kujikaza na kupambana kuyafanya yale ambayo wengi wanashindwa kuanzia lifestyles,mtazamo,maamuzi,mahusiano na weledi...! |Je,wewe ulifikiria nini ulipojibatiza jina unalolitumia hapa JF?