Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Binafsi sijawah fikisha 10 mill ,ila kama umefanikiwa kufikisha 3 au 4 mil ,sio mbaya kwa maaana umepiga hatua kutoka katika namba moja 1 kwenda namba nyingine 2, utafika 3 ,4 nakuendelea .
waweza fanya yafwatalo
1.nunua kiwanja mahali ambapo mji unatanuka kisha kiache kwa muda kidogo.

2.wekeza katika hisa kama una uelewa na hizi mamboo

3.wekeza kwenye matunda ya msimu au wanyama mfano kuku au ngoimbe kwa maana wanatumika kila siku.

4.fungua restaurant au kibanda cha chips mahala penye msongamano wa watu.nafikiri mchanganu ya biashara ya chips ipo humu kibao na pia imejadilikwa kwa kina na jinsi ya kuzuia na kupmbn na changamoto


ni hayoo tuuu
 
Pindi Npo chuo bodi waliniingizia 1.2 M Kwenye accnt yngu. Daah nilijiona bonge la tajir, aisee ile pesa haikudumu ata mwezi.

Apo ndo nkajua million ni pesa ya mboga tu. Sa hv nina ndoto za kushika billion na kuendelea.
Hapo kwenye bilion umeongea vemaa
 
Habari jf

Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida ni changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.

Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!... Lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa siyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndio ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.

Najaribu kupambana nifike milioni 10 wapi!!

Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea

Nb: Hapa naongelea saving, hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine.

Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
Kila mwaka huwa nacheza vikoba na huwa natoa laki moja kila mwezi ukiongeza na kiingilio huwa tukivunja nakuwa na 1mil na laki 4 nimefanya hivo kwa muda wa miaka mitatu na mwaka jana tulipovunja mwezi wa 12 ikabidi nikae na kutafakari kwa hiyo ntafanya mzecho huu wa kichaa hadi lini?
Kila mwezi ofisini kwetu watu huwa wananifata kuomba niwape mkopo na mara nyingi huwa nafanya fair mtu anaomba nimpe laki moja hadi laki tano
Ila mwishoni naambulia za uso mtu analudisha laki moja siku nyingine elfu50 hadi deni linaisha
Mwisho nikatafakari nikasema ebu nifanye hii kama fursa mtu akitaka pesa nampa kwa mkopo na liba nikaweka 20% .
Kabla nikakutana na watu wanishauri ila kila niliyemuuliza alinambia usisubutu utatapeliwa
Moyoni nikasema najitosa na hii 1mil na laki4 mwezi wa pili mwaka huu nikaanza rasmi biashara mpaka sasa malengo yangu hadi mwezi wa 12 nifunge nikiwa na mil10 mpaka sasa nimefikisha mill6 na nusu
NOTE: hii pesa huwa siigusi kwa chochote kile
 
Kama unapata salary au return ya 3M kwa mwezi, fungua fixed account ya miaka miwili NMB weka 1M kila mwezi bila kupepesa jicho, 2M weka katika Matumizi ya chakula na ada za watoto kama unao, hakikisha unapunguza Matumizi yasiyo ya ulazima kama partying daily Ili kufikia malengo fulani inahutaji sacrifice kubwa.
 
Habari jf

Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida ni changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.

Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!... Lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa siyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndio ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.

Najaribu kupambana nifike milioni 10 wapi!!

Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea

Nb: Hapa naongelea saving, hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine.

Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
Mkuu Kwa serving ya kupitia mshahara ni ngumu, unless Uwe unapata net pay ya kuanzia 5M kuendelea.
Nakushauri badala ya kuweka Benki ili zijae tafuta namna ya kuzizungusha. Ongeza muda wako WA kufanya kazi toka masaa nane au kumi na mbili upate walau masaa 48 ndani siku ya moja yenye masaa 24, inaweza kuonekana kichekesho fulani lakini ukweli ndo huo.
Namna ya kuongeza masaa ya kufanyakazi ni kuwa na kazi nyingine ndogo ndogo ambazo zitafanywa na watu wengine ambao watakusaidia kuingiza kipato na faida kidogo. Wataalam wa mambo ya fedha Kwa lugha ya Malikia wanaita Levarege,
Chukulia mfano METL kila sekunde moja kuna product yake inanuliwa ambayo pengine inampatia shilingi moja Tu ya faida fanya hesabu upate Kwa Siku anaingiza faida ya shilingi ngapi.
Jambo lingine Acha kuomba muda wa kazi za ziada kazini kwako, badala yake huo muda utumie kufanya shughuli zako. Punguza muda wa kukaa na marafiki baa, punguza magroup ya kuchangiana nk.
NJIA RAHISI NA NYEPESI
Hii njia niliwahi kuitumia wakati nahitaji kukusanya hela Kwa ajili ya kwenda chuo:-
Jiunge na Saccos ambayo inaaminika na ambayo siku ukiamua kujitoa unachukuwa share zako zote. Utafanyaje? Ukishajiunga endelea kuweka share zako jaribu kuweka kile kiwango unachohitaji kufanya serving kila mwezi, hii itakuwezesha usitoe na kitumia hiyo hela hata kama utakuwa na Shida ya kufa, make sheria hazitokuruhusu. Lakini utakuwa na wigo wa kupata mkopo na kutatua matatizo madogo madogo huku akiba yako ikiendelea kusimama. Epuka mkopo mkubwa ambao utavuruga utaratibu wako wa serving ya kila mwezi hasa kipindi utakapokuwa unarejesha deni.
La mwisho na gumu ni kuwa na roho ngumu, Acha kufanya hela yako iwe ya ukoo, hela yako ibaki kuwa ya kwako. Tenga makundi ya lazima ya kuisaidia kama wazazi Kwa pande zote mbili endapo umeoa na uwe na kiwango maalumu.
Mwisho Mimi milioni kumi yangu ya Kwanza nilipata Kwa kulipwa mafao yangu ya PPF baada ya kufanya kazi miaka 7.
Bahati nzuri ni kwamba mwajiri aliuza kazi zilizokuwa chini ya Idara niliyokuwa nafanyia kazi, na zikawa zimechukuliwa na outsourced company. Hivo nilikomba mpunga wangu PPF na nikaendelea na kazi ya mkataba under outsourced company. Nadhani Sisi ndo tumechukuwa hela mwisho kabla ya hizi sheria kandamizi za kuzuia FAO la kujitoa.
 
Yah, savings ni matokeo ya kuwa na excessive earnings. Huezi kuwa unapata elfu 5 ambayo haitoshi hata milo kwa siku kisha uniambie utasave...Unasave nini hapo?

Tofauti na mtu ambaye anapata maybe 15K per day. Atakula 7K kisha 7K ingine anai save. Inawezekana kabisa. Kitu kimenishinda ni kujitesa na njaa ati kisa na save. Mi huwa nakubaliana na hali halisi tu sina kipato cha ku save natulia na kubuni mbinu tu nitapataje zaidi.

Raha ya ku save uwe na excess cash.
Umeongea point kinomaa
 
Back
Top Bottom