Hahahah wew jamaa banaBaada ya kufukuzwa kazini kutokana na mgomo tukalipwa million 8 na hela za nssf ikawa imefikia million 10 ila mpaka leo sijui nilizitumia vp zile hela.
Kila mtu amefikia hiyo 10m kwa namna yake.Habari jf
Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida ni changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.
Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!... Lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa siyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndio ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.
Najaribu kupambana nifike milioni 10 wapi!!
Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea
Nb: Hapa naongelea saving, hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine.
Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
we unazungumzia kuwa na App? Mi hata bila app nachukua kadi huyo kwenye bodabodaUsiwe na hio app kama unahitaji kuweka akiba/unaishi kwa bajeti
NdioWewe upo Dubai?
Haya pendekeza jina la ID nzuri uipendayo na uniambie nawezaje kuedit Id yangu ya zamani kuwa mpya.Badili id...siwezi kumwamini mtu anajiita mbu...wewe si mnyonyaji damu na mleta maradhi ya moyo tu?
Pendekeza jina na uingie hapa badili jina fasta;Haya pendekeza jina la ID nzuri uipendayo na uniambie nawezaje kuedit Id yangu ya zamani kuwa mpya.
Hongera sana,nauliza ulikuwa unatumia njia gan kuwafundishaNilianzisha biashara ya kufundisha watu jinsi ya kufaulu mitihani ya vyuo vya Marekani mwaka 2015. Miezi 3 baadae tulipata deal tukapata 16m na 4.5 m kati yake ilikuwa faida tukagawana na partner wangu so nikapata 2.25m.
Then Nikaanzisha biashara ya consultation kuhusu kumanage uzito mwaka 2016. Mpaka 2017 katikati nilikuwa na 10m saved tayari.
Una principle nzuri ,napenda kujua ukisema una nunua investment una maanisha nn..Binafsi saving kwangu haijawahi kuwa tatizo maana pia naogopa mikopo .
Nina salary ndogo tuu take home haizidi 600k but hapo nasevu half of it .
Sasa nikipata na viposho posho huwa sipingui 2.5-4 ndani ya miezi 6 na nikipata hiyo nanunua investment au nafanya mtaji somewhere.
Ndani ya mwaka naweza fikisha saving ya Kati ya 5ml hadi 6 kwa hiyo hizi naweka kweye assets mwisho wa siku nikijumlisha assets zangu zinavuka hiyo 10 mln.
Kitu cha kukwamisha ni labda nipate mgonjwa wa mda mrefu tofauti na hapo nafikisha,nimejenga kwa staili hii hii na kama nakopa ujue ni kwa friend na si vinginevyo.
Nakuunga mkono mkuu saccos zipo vizurKing ni hivi Sacco's zipo za maana hazina shida usisikilize maneno ya chadema mkuu
Ila kikoba kinasaidia mtu ambaye hawezi kutunza ela yake...maana hupati ela ya ziada na faida ni ndogo sana ukilinganishana riba kama ni lazima kukopa...Jiunge kikoba au Sacco's pia michezo ya Kila siku.
Nipo kwenye mchezo naweka 20,500 Kila siku sometimes nacheza majina hata 3.
Siku nikipokea hela napeleka kikoba.
Tumevunja juzi piga hesabu.
Mwaka huu mwendo ni ule ule namuomba Mungu sana ila najua inawezekana tu kwake in five years to come niwe na m 50 hivi
AminaEeeh Mungu nisaidie nishike hata milion 2 cash mkononi.
Duh aise...mimi nilipata hela za nssf mil 11 na kitu so nilichofanya sikutaka kukurupuka na biashara mpya nikachukua mil 5 nikaweka utt mfuko wa ukwasi..pesa mil 2 nikafanya mambo yangu na kumaliza deni la kiwanja then mil 4 zilizobaki ndo nazungusha kwenye biashara na faida naiona...pesa za haraka zinapotea kama upepo maaana unaona nying sema ukitulia zinakusaidia.Baada ya kufukuzwa kazini kutokana na mgomo tukalipwa million 8 na hela za nssf ikawa imefikia million 10 ila mpaka leo sijui nilizitumia vp zile hela.
Safi sana kiongozi kanyaga twende tumechelewa mnooMwaka Jana ndo nilishika kwa pamoja kwa mara ya kwanza ila mpaka time hii nimebaki na laki 9 pesa yote imeingia kwenye investment ya maana hope this year ndoto kutengeneza akiba ya 15M+ hapo baada ya matumizi yote.2025 ndo utakua mwaka wa kuvuna zaidi kwasababu biashara nilizowekeza zitarudisha majibu naamini.
Njia iliyotumika nilikua nahifadhi pesa zangu timiza ya Airtel money na nyingine niliweka kwenye kibubu na nyingine Nia sista wangu aliniingilia vikoba somewhere. Mwaka huu nimeingia mwenyewe kikoba.
Eeeh Mungu nisaidie nishike hata milion 2 cash mkononi.