Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Habari jf

Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida ni changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.

Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!... Lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa siyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndio ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.

Najaribu kupambana nifike milioni 10 wapi!!

Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea

Nb: Hapa naongelea saving, hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine.

Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
Kila mtu amefikia hiyo 10m kwa namna yake.
Ukisema ufanye saving usipokuwa na mikakati madhubuti utazeeka bila kuifikia.

Mimi kazi yangu ya pili yaani cotract nilipaisha hadi 20m kwa wakati mmoja hiyo ni baada ya kutoa kila kitu katika matumizi ya muhimu na ya kawida.

1. Nature ya kazi yako inaweza kukufikisha pale au

2. Kwa kuweka kwenye fixed account na ukawa mwaminifu katika saving.
 
Inahitaji upambane sana, kujinyima vingi
 
Badili id...siwezi kumwamini mtu anajiita mbu...wewe si mnyonyaji damu na mleta maradhi ya moyo tu?
Haya pendekeza jina la ID nzuri uipendayo na uniambie nawezaje kuedit Id yangu ya zamani kuwa mpya.
 
Nilifungua account ya saving nmb na ndio natumia kusevu hadi sasa ,hio haina makato na hauwezi kutoa hela atm wala sim banking unaruhusiwa kuchukua fedha mda wowote ila itakubidi uingie ndani bank physically,ukifungua hio account unakua na atm card kwa ajili ya kuangalia salio tu,nidhamu kali ya matumizi ya fedha inahitajika.
 
Nilianzisha biashara ya kufundisha watu jinsi ya kufaulu mitihani ya vyuo vya Marekani mwaka 2015. Miezi 3 baadae tulipata deal tukapata 16m na 4.5 m kati yake ilikuwa faida tukagawana na partner wangu so nikapata 2.25m.

Then Nikaanzisha biashara ya consultation kuhusu kumanage uzito mwaka 2016. Mpaka 2017 katikati nilikuwa na 10m saved tayari.
Hongera sana,nauliza ulikuwa unatumia njia gan kuwafundisha
 
Binafsi saving kwangu haijawahi kuwa tatizo maana pia naogopa mikopo .

Nina salary ndogo tuu take home haizidi 600k but hapo nasevu half of it .

Sasa nikipata na viposho posho huwa sipingui 2.5-4 ndani ya miezi 6 na nikipata hiyo nanunua investment au nafanya mtaji somewhere.

Ndani ya mwaka naweza fikisha saving ya Kati ya 5ml hadi 6 kwa hiyo hizi naweka kweye assets mwisho wa siku nikijumlisha assets zangu zinavuka hiyo 10 mln.

Kitu cha kukwamisha ni labda nipate mgonjwa wa mda mrefu tofauti na hapo nafikisha,nimejenga kwa staili hii hii na kama nakopa ujue ni kwa friend na si vinginevyo.
Una principle nzuri ,napenda kujua ukisema una nunua investment una maanisha nn..
 
Jiunge kikoba au Sacco's pia michezo ya Kila siku.

Nipo kwenye mchezo naweka 20,500 Kila siku sometimes nacheza majina hata 3.

Siku nikipokea hela napeleka kikoba.

Tumevunja juzi piga hesabu.

Mwaka huu mwendo ni ule ule namuomba Mungu sana ila najua inawezekana tu kwake in five years to come niwe na m 50 hivi
Ila kikoba kinasaidia mtu ambaye hawezi kutunza ela yake...maana hupati ela ya ziada na faida ni ndogo sana ukilinganishana riba kama ni lazima kukopa...
 
Mwaka Jana ndo nilishika kwa pamoja kwa mara ya kwanza ila mpaka time hii nimebaki na laki 9 pesa yote imeingia kwenye investment ya maana hope this year ndoto kutengeneza akiba ya 15M+ hapo baada ya matumizi yote.2025 ndo utakua mwaka wa kuvuna zaidi kwasababu biashara nilizowekeza zitarudisha majibu naamini.

Njia iliyotumika nilikua nahifadhi pesa zangu timiza ya Airtel money na nyingine niliweka kwenye kibubu na nyingine Nia sista wangu aliniingilia vikoba somewhere. Mwaka huu nimeingia mwenyewe kikoba.
 
Baada ya kufukuzwa kazini kutokana na mgomo tukalipwa million 8 na hela za nssf ikawa imefikia million 10 ila mpaka leo sijui nilizitumia vp zile hela.
Duh aise...mimi nilipata hela za nssf mil 11 na kitu so nilichofanya sikutaka kukurupuka na biashara mpya nikachukua mil 5 nikaweka utt mfuko wa ukwasi..pesa mil 2 nikafanya mambo yangu na kumaliza deni la kiwanja then mil 4 zilizobaki ndo nazungusha kwenye biashara na faida naiona...pesa za haraka zinapotea kama upepo maaana unaona nying sema ukitulia zinakusaidia.

Faida ya hizo pesa zinazotokana na business nacheza hii michezo ya kina mama kwa mwezi lak 2 ili pesa iwe kwa mzunguko isitumike sehem sio sahihi...
 
Mwaka Jana ndo nilishika kwa pamoja kwa mara ya kwanza ila mpaka time hii nimebaki na laki 9 pesa yote imeingia kwenye investment ya maana hope this year ndoto kutengeneza akiba ya 15M+ hapo baada ya matumizi yote.2025 ndo utakua mwaka wa kuvuna zaidi kwasababu biashara nilizowekeza zitarudisha majibu naamini.

Njia iliyotumika nilikua nahifadhi pesa zangu timiza ya Airtel money na nyingine niliweka kwenye kibubu na nyingine Nia sista wangu aliniingilia vikoba somewhere. Mwaka huu nimeingia mwenyewe kikoba.
Safi sana kiongozi kanyaga twende tumechelewa mnoo
 
Back
Top Bottom