Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

20,000*365 ni kama 7,300,000
 
Aim ilikua 1 kufikisha target,mimi ni mtu dhaifu sana wakuangalia hela tu ipo mbele yangu....

hivyo naibadilisha hela navitu vyenye thamani ya pesa yangu,nilianza kwa kununua pikipiki....

nainunua leo kesho natangaza naiuza kwa bei ya juu,nikiiuza nanunua kitu kingine,kesho kutwa....

natangaza nakiuza kwa bei ya juu,mwendo ni huo huo,na kodisha frem 300k namimi naikodsha kwa 400k...

maisha yalikua namna hiyo kimasihara kama asemavyo rikiboy ten Em hii hapa na zaidi,life goes on...
 
Vipi mali za wizi , hukukutana nazo? Manake vyombo vya moto navyo majanga
 
Ndiyo hivyo. Shida kubwa watu wengi wakienda shule kidogo anaona biashara za mtaani ni kama kushika uchafu. Kuna kijana mmoja mwalimu s/msingi wa kichaga alipanga chumba kwetu akaona fursa akafungua genge la mbogamboga hapo nje kalitengeneza kwa mabanzi tu ya kawaida. Saizi anauza laki 8 kwa siku. Tunataka kuanza kumtoza kodi lakini tunajishtukia kwa aibu, coz ni kasehemu ambacho wala hatukujua kuwa ni potential. Sasa mwambie graduate wa Mzumbe au Udsm afungue genge.
 
I like that!!
 
Needs vs wants. Ukifanya tathmini hio 3m au 4m uliyofikisha kutunza halafu ukatumia, utaona kwamba wala matumizi yake leo hii hayaonekani. Watu kinachowamaliza ni matumizi. Nilitoka Tz maskini hata buku ikawa inanipiga chenga, nikaenda USA nikaanza shika usd 5000 kwa mwezi... ambayo kwa exchange rate ya sasa hio ni zaidi ya tshs 10m. Nikawa nanunua suti za $1000 (Sean John), viatu ni jordans, nike, etc. Bling bling kibao. Magari nikawa nabadilisha kila mwaka (USA gari unalipia kwa mwezi kwa hio ni kama mkopo tu). Matanuzi kibao. USD5000 ikawa hata haitoshi kwa matumizi yangu kwa mwezi.
Kwa sasa nimemudu kuwa saver mzuri. Matumizi yasio na msingi sifanyi tena. Nguo sijanunua sijui miaka mingapi. Nanunua viatu tu mara moja moja. Nimeweza ku-save millions and millions and millions. Na nimejenga sana na nina rasilimamali kibao tena kwa hela binafsi na SIO YA MKOPO. PIA NDUGU SIKU HIZI NIMEWAFYEKELEA MBALI. Hakuna mnyonya damu mkubwa na mbaya kama ndugu ambaye hajapambana kama ww kimaisha ila anataka ale tu kwa mrija kupitia jasho lako.
 
hamna kitu unajua kuhusu vicoba it was better for you to stat low!
VICOBA = Village Commercial Bank...
Nakushauri bora pesa yako ukainvest sehemu au uingie partnership au ununulie ata shares kama una knowledge na hivyo vitu kuliko uko Kwenye VICOBA na masaccos,uko ujanja mwingi watu wanacheza na % tu..
 

Du hivi mnawezaje kusave hela mpaka ikafikia milioni 3 kwenye kibubu bila kuzila? Mtu anayesave hela basi najua hana cha kufanya!! Mie account yangu ina operate na elfu 2 au 3! Ikiingia hela ndani ya siku 3 ishakwisha yote hata mil 20 maana kuna kazi nyingi za matumizi ya hela...Hela wanaziweka watu ambao hawana majukumu hata kidogo yaani wale watu wanaotafuta fedha ya kunua sandozi ,kito,pafyumu,supra,mawani etc hao ndio wanaweza kusave fedha.
 
Vipi mali za wizi , hukukutana nazo? Manake vyombo vya moto navyo majanga
Nimewahi sana na nikihisi tu ni cha wizi huwa nina team yangu ya manunuzi (sinunui mimi)

nawatonya wanakuja,nawapa hela wananunua kisha wanasepa,muuzaji hatojua kama n mimi

nimenunua na team yangu ya manunuzi haikai mtaa niliopo hao wanakuja kwa case maalum tu
 
We hata huelewi kinachojadiliwa hapa. Hivi mashabiki wa Yanga akili zenu huwa mnaziacha kwenye maduka ya GSM?
 
Ukiona mtu anasave hadi inafika kiasi hicho bila kuzila ina maana anazo za kuzila hio ni ziada. Vile vile sio kwamba Hana cha kufanyia, za kufanyia shughuli nyingine zipo zinafanya vitu hizo zinazowekwa ni ziada.
Mwingine kwenye mapato yake ya biashara anatenga kiasi fulani cha kodi ya pango la hio biashara na gharama nyingine zitakazojitokeza.
Ila nimekuelewa wengine kila hela ikipatikana inapata matumizi/kazi.
 
We hata huelewi kinachojadiliwa hapa. Hivi mashabiki wa Yanga akili zenu huwa mnaziacha kwenye maduka ya GSM?

Hahahaaaaa yaani nyie maBUKU 7 FC ndio hamjielewi ,Mtoa mada kashawahi kusave hadi milioni 3 kwenye KIBUBU ndio swali langu likaja inawezekana vipi mtu uweze kusave hadi milioni 3 kwani hakuna kitu za kuzifanyia?
 
Duh mkuu kumbe ni mnunuaji mzoefu wa vitu vya wizi? Nilifikiri ungesema ukihisi au kujua ni cha wizi unaachana nacho!
 
Aisee genge kuuza 800,000/- per day si mchezo!
 
Hahahaaaaa yaani nyie maBUKU 7 FC ndio hamjielewi ,Mtoa mada kashawahi kusave hadi milioni 3 kwenye KIBUBU ndio swali langu likaja inawezekana vipi mtu uweze kusave hadi milioni 3 kwani hakuna kitu za kuzifanyia?
Kitu cha kuzifanyia ndiyo jambo linalokufanya usave. Nadhani umeshaelewa
 
Nina ki account cha $ kila mwezi naweka minimum $100. Ikifika mwisho wa mwaka nazitoa zote naamua tu vacation wapi. Sasa hapo wengine wakiona mwisho wa mwaka unasafiri huku na kule wanashangaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…