Jobless_Billionaire
JF-Expert Member
- Aug 9, 2022
- 3,106
- 8,101
Habarini wakuu!
Hakika miaka inakwenda. Miaka ya nyuma, magazeti yalikuwa na mvuto sana kuanzia front pages hadi ndani. Yalikuwepo magazeti mengi sana ila Binafsi nilikuwa mpenzi wa magazeti ya Sani na Kiu.
Hao jamaa walikuwa wabunifu sana, kurasa za mbele zilipambwa kwa picha nzuri za mastaa na vichwa vya habari vyenye kuibua hisia sana. Picha za warembo wenye maumbile mazuri na muhtasari wa habari zilizomo ndani yake. Raha ya haya magazeti ilikuwa ni zaidi hata ya kumiliki smartphones siku hizi ambazo ni kama zinaleta depression tu kwa watu. Enzi hizo hakukuwa na mambo ya kuwaza sijui fulani hajaview status yangu, mbona hajanipost, sijui kaniblock na mambo kama hizo
Kulikuwa na simulizi zilizotungwa kwa imahiri, zinazokuachia kiu ya kutaka kufatilia toleo lijalo bila kukosa. Pia kulikuwa na katuni kama vile Lodilofa, Kipepe, Kifimbo Cheza, Madenge, Baba ubaya na nyingine nyingi. Hakika ilikuwa zaidi ya burudani.
Leo nimepita ukurasa fulani nikakutana na picha za katuni za enzi hizo nikapata kurejesha kumbukumbu nyuma sana jinsi burudani hizo zilivyoweza kukonga nyoyo zetu. Hiyo ni kwa ufupi tu.
Wewe unakumbuka nini kuhusu magazeti ya enzi hizo?
Hakika miaka inakwenda. Miaka ya nyuma, magazeti yalikuwa na mvuto sana kuanzia front pages hadi ndani. Yalikuwepo magazeti mengi sana ila Binafsi nilikuwa mpenzi wa magazeti ya Sani na Kiu.
Hao jamaa walikuwa wabunifu sana, kurasa za mbele zilipambwa kwa picha nzuri za mastaa na vichwa vya habari vyenye kuibua hisia sana. Picha za warembo wenye maumbile mazuri na muhtasari wa habari zilizomo ndani yake. Raha ya haya magazeti ilikuwa ni zaidi hata ya kumiliki smartphones siku hizi ambazo ni kama zinaleta depression tu kwa watu. Enzi hizo hakukuwa na mambo ya kuwaza sijui fulani hajaview status yangu, mbona hajanipost, sijui kaniblock na mambo kama hizo
Kulikuwa na simulizi zilizotungwa kwa imahiri, zinazokuachia kiu ya kutaka kufatilia toleo lijalo bila kukosa. Pia kulikuwa na katuni kama vile Lodilofa, Kipepe, Kifimbo Cheza, Madenge, Baba ubaya na nyingine nyingi. Hakika ilikuwa zaidi ya burudani.
Leo nimepita ukurasa fulani nikakutana na picha za katuni za enzi hizo nikapata kurejesha kumbukumbu nyuma sana jinsi burudani hizo zilivyoweza kukonga nyoyo zetu. Hiyo ni kwa ufupi tu.
Wewe unakumbuka nini kuhusu magazeti ya enzi hizo?