Ulikuwa mpenzi wa gazeti gani miaka ya nyuma?

Ulikuwa mpenzi wa gazeti gani miaka ya nyuma?

Habarini wakuu!

Hakika miaka inakwenda. Miaka ya nyuma, magazeti yalikuwa na mvuto sana kuanzia front pages hadi ndani. Yalikuwepo magazeti mengi sana ila Binafsi nilikuwa mpenzi wa magazeti ya Sani na Kiu.

Hao jamaa walikuwa wabunifu sana, kurasa za mbele zilipambwa kwa picha nzuri za mastaa na vichwa vya habari vyenye kuibua hisia sana. Picha za warembo wenye maumbile mazuri na muhtasari wa habari zilizomo ndani yake. Raha ya haya magazeti ilikuwa ni zaidi hata ya kumiliki smartphones siku hizi ambazo ni kama zinaleta depression tu kwa watu. Enzi hizo hakukuwa na mambo ya kuwaza sijui fulani hajaview status yangu, mbona hajanipost, sijui kaniblock na mambo kama hizo

Kulikuwa na simulizi zilizotungwa kwa imahiri, zinazokuachia kiu ya kutaka kufatilia toleo lijalo bila kukosa. Pia kulikuwa na katuni kama vile Lodilofa, Kipepe, Kifimbo Cheza, Madenge, Baba ubaya na nyingine nyingi. Hakika ilikuwa zaidi ya burudani.

Leo nimepita ukurasa fulani nikakutana na picha za katuni za enzi hizo nikapata kurejesha kumbukumbu nyuma sana jinsi burudani hizo zilivyoweza kukonga nyoyo zetu. Hiyo ni kwa ufupi tu.

Wewe unakumbuka nini kuhusu magazeti ya enzi hizo?

Alasiri na dar leo
 
Mzee mwenzangu kwangu Mimi Bongo,sani na Tabasamu ndio yalikua majarida yangu.Kwa kweli Ile mipicha ya totoz kwenye cover nimejichukulia sheria mkononi sana coz ndio ilikua balehe imepamba moto.
 
Siku ya Alhamisi ni RAI "nguvu ya hoja" chini ya mhariri John Bwire na Sanifu chini ya Munga Tehnani.
Gazeti la kila siku ni Majira.
Majarida ni SANI chini ya Said Bawji na mchoraji mwandamizi Philip Ndunguru na Tabasamu chini ya Masasi na mchoroji John Kaduma.
 
Habarini wakuu!

Hakika miaka inakwenda. Miaka ya nyuma, magazeti yalikuwa na mvuto sana kuanzia front pages hadi ndani. Yalikuwepo magazeti mengi sana ila Binafsi nilikuwa mpenzi wa magazeti ya Sani na Kiu.

Hao jamaa walikuwa wabunifu sana, kurasa za mbele zilipambwa kwa picha nzuri za mastaa na vichwa vya habari vyenye kuibua hisia sana. Picha za warembo wenye maumbile mazuri na muhtasari wa habari zilizomo ndani yake. Raha ya haya magazeti ilikuwa ni zaidi hata ya kumiliki smartphones siku hizi ambazo ni kama zinaleta depression tu kwa watu. Enzi hizo hakukuwa na mambo ya kuwaza sijui fulani hajaview status yangu, mbona hajanipost, sijui kaniblock na mambo kama hizo

Kulikuwa na simulizi zilizotungwa kwa imahiri, zinazokuachia kiu ya kutaka kufatilia toleo lijalo bila kukosa. Pia kulikuwa na katuni kama vile Lodilofa, Kipepe, Kifimbo Cheza, Madenge, Baba ubaya na nyingine nyingi. Hakika ilikuwa zaidi ya burudani.

Leo nimepita ukurasa fulani nikakutana na picha za katuni za enzi hizo nikapata kurejesha kumbukumbu nyuma sana jinsi burudani hizo zilivyoweza kukonga nyoyo zetu. Hiyo ni kwa ufupi tu.

Wewe unakumbuka nini kuhusu magazeti ya enzi hizo?

Wewe haujui magazeti jinsi yalivyo! Ni wazi haukuwa msomaji wa magazeti wala msikilizaji wa habari kwenye redio.
 
Sanifu lilikuwa bonge la gazeti. Ule ukurasa wenye Tolu wa Ajabu ulikuwa mtamu sana.
 
Back
Top Bottom