Nilikuwa barnaba Niko likizo baada ya kufunga shule, siku hiyo nimetoka zangu kucheza fainali ya kombe la kuku tumepigwa 6-1 na jamaa Fulani walikuwa wanajiita BLACK MAMBAZ wakachukua jogoo wao halafu wakatufurumusha na mawe maana yalikuwa ni madingi na ligi ilichezewa mtaani kwao.
Kwanza sikula kabisa usiku, ukichanganya maumivu ya kukosa kuku na ule mzuka wa kusubiria game hamu ya kula itoke wapi, akili yangu ilikuwa inawaza kumuona TH14 akitupia tu basi.
Siku hiyo Zidane alikuwa haoni pakupitisha mipira aliwekwa kwenye giza la catenacio kila akigeuka akiangalia mbele anamuona canavaro na nesta sio henry wala djokerf.
Mpaka dakika 91 baada ya mpira kuanza nawaona wataliano wakijiandaa kushangilia ubingwa wameshajifunga na bendera zao viunoni, nikajua tayari ngoma imelala na pia muda huo Italia alikuwa ametolewa na France world cup iliyopita kwenye robo fainali hivyo ilikuwa ni mechi ya kisasi.
Sekunde 28 za mwisho wataliano hawawezi kuzisahau kamwe katika maisha yao baada ya trezguet kuwavurugia sherehe, dakika tatu baada ya extra time wiltord ana wauwa wataliano kwa goli la dhahabu na mpira unaisha ufaransa anaweka record ya kuchukua euro na WC ndani ya miaka miwili.
Nikiwa kama shabiki mkubwa wa ufaransa naomba sana FIFA waturudishie tena goli la dhahabu, hili dunia iendelee kuona maajabu yalikuwa yanafanywa na ufaransa kipindi hicho