Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Asili inachukua mkondo wake.. Dini zilizotegemewa kama kimbilio la kumuokoa mwanadamu kiroho sasa zinashuhudia anguko kubwa kuliko wakati mwingine wowote ule
Kwasasa dini nazo ni mateka wa imani za siri za kidunia.. Na hapa namaanisha dini zote zinazomuabudu Mungu moja
Kwasasa dini zetu
. Ni dini za biashara.. Pesa zikiwa ndio kipaumbele kikubwa
. Ni dini za miujiza na mazingaombwe
. Ni dini za mipasho na ulaghai
. Ni dini zinazobeba majukumu ya waganga wa kienyeji walozi na wachawi
. Ni dini za kufanyiana fitina, majungu na kugombea vyeo na madaraka
. Ni dini kwa ajili ya wenye nacho hasa matajiri, wanasiasa, wasanii wakubwa, watu maarufu na hata wauaji wa kuogopeka
. Ni dini zenye kutanguliza maslahi binabsi ama maslahi ya watawala ama kundi fulani la watu
Tuna dini zisizofundisha uhalisia ama zisizojua kufundisha uhalisia ama kutafsiri maandiko na misahafu.. Tuna dini za kuhubiri vitu vya kufikirika zaidi na mifano mfu ya kufunga
Haya mambo yamesababisha ombwe kubwa kwa naamini na waumini wake huu ya uelewa, ufahamu na mikanganyiko mingi kunakopelekea anguko kubwa...!
Vyama vya siri vyenye kutoka mafundisho ya ufahamu na kujitambua, vyenye mikakati na maono ya mbali sasa ndio vimeziteka dini zoote na ndio vinaendesha dunia
Bila kuwa na uelewa binafsi
Bila kuwa na maarifa binafsi
Bila kuwa na imani thabiti na binafsi yako mwenyewe, juuu ya yale unayoamini na kwanini unayaamini.. Juu ya ithibati mbali mbali.. Umekwisha!
Asili inachukua mkondo wake.. Maana dini zimefeli..zimejaa mafundisho yanayohitaji ufafanuzi wa kina .. Lakini hao wafafanuzi sasa! Ni majanga..
Dini zetu zinatufundisha tusiue.. Lakini hatujafafanuliwa tusiue nini na kwa sababu gani.. Huu ni Mfano mmoja tu rahisi kabisa!
Dini zetu zinatuambia kuhusu nambari ya siri inayotawala na inavyotawala dunia lakini hakuna wafafanuzi wa haya maarifa.. Matokeo yake nambari hiyo imepenya mpaka kwenye dini zenyewe maana ndio mahitaji ya nyakati
Kuna wajenzi huru(Freemasons) wapembuzi yakinifu waliojawa maarifa, wanaoweza kujibu kila swali tata.. Wenye elimu pana na kubwa na maarifa kuhusu, dunia, ulimwengu na imani zake.. Hawa ni mabingwa wao mipangilio ya tarakimu.. Wanakuambia ulimwengu unaendeshwa na tarakimu (nambari za siri)
Kuna Satanism (imani za kishetani) zimepewa jina baya lakini zimejaa maarifa mengi na yenye nguvu sana .. Mengine yanatisha kwakuwa yana connection ya moja kwa moja na nguvu za asili.. Hawa ni wababe wao mambo ya kiroho
Paganism.. Wasiamini katika chochote bali imani hao😀.. Wenye kutafuta uwiano kati ya hao wengine Wote.. Wasiojua chochote kuhusu nambari za siri, wasuojua chochote kuhusu ulimwengu wa roho.. Wasiojua chochote kuhusu asili..
Waamini wa kwamba kila kitu kipo kwa sababu kipo(bila kufafanua sababu yenyewe) hakuna mwanzo na hakuna mwisho.. Hakuna Mungu, hakuna miungu wala hakuna roho! Wakizaliwa wanezaliwa na wakifa wamekufa!
Wakipata wamepata na wakikosa wamekosa! No more reasoning.. Hawa ni stress free species .. Hawajisumbui kwa lolote lile!
Hitimisho: colabo ya hawa watatu umezifanya dini zetu zote kuwa mateka wao na mafundisho yao kwa sehemu kubwa ndio yanatawala mahubiri ya kila siku kwenye nyumba za ibada zenye kumwamini Mungu mkuu..
Kwasasa dini nazo ni mateka wa imani za siri za kidunia.. Na hapa namaanisha dini zote zinazomuabudu Mungu moja
Kwasasa dini zetu
. Ni dini za biashara.. Pesa zikiwa ndio kipaumbele kikubwa
. Ni dini za miujiza na mazingaombwe
. Ni dini za mipasho na ulaghai
. Ni dini zinazobeba majukumu ya waganga wa kienyeji walozi na wachawi
. Ni dini za kufanyiana fitina, majungu na kugombea vyeo na madaraka
. Ni dini kwa ajili ya wenye nacho hasa matajiri, wanasiasa, wasanii wakubwa, watu maarufu na hata wauaji wa kuogopeka
. Ni dini zenye kutanguliza maslahi binabsi ama maslahi ya watawala ama kundi fulani la watu
Tuna dini zisizofundisha uhalisia ama zisizojua kufundisha uhalisia ama kutafsiri maandiko na misahafu.. Tuna dini za kuhubiri vitu vya kufikirika zaidi na mifano mfu ya kufunga
Haya mambo yamesababisha ombwe kubwa kwa naamini na waumini wake huu ya uelewa, ufahamu na mikanganyiko mingi kunakopelekea anguko kubwa...!
Vyama vya siri vyenye kutoka mafundisho ya ufahamu na kujitambua, vyenye mikakati na maono ya mbali sasa ndio vimeziteka dini zoote na ndio vinaendesha dunia
Bila kuwa na uelewa binafsi
Bila kuwa na maarifa binafsi
Bila kuwa na imani thabiti na binafsi yako mwenyewe, juuu ya yale unayoamini na kwanini unayaamini.. Juu ya ithibati mbali mbali.. Umekwisha!
Asili inachukua mkondo wake.. Maana dini zimefeli..zimejaa mafundisho yanayohitaji ufafanuzi wa kina .. Lakini hao wafafanuzi sasa! Ni majanga..
Dini zetu zinatufundisha tusiue.. Lakini hatujafafanuliwa tusiue nini na kwa sababu gani.. Huu ni Mfano mmoja tu rahisi kabisa!
Dini zetu zinatuambia kuhusu nambari ya siri inayotawala na inavyotawala dunia lakini hakuna wafafanuzi wa haya maarifa.. Matokeo yake nambari hiyo imepenya mpaka kwenye dini zenyewe maana ndio mahitaji ya nyakati
Kuna wajenzi huru(Freemasons) wapembuzi yakinifu waliojawa maarifa, wanaoweza kujibu kila swali tata.. Wenye elimu pana na kubwa na maarifa kuhusu, dunia, ulimwengu na imani zake.. Hawa ni mabingwa wao mipangilio ya tarakimu.. Wanakuambia ulimwengu unaendeshwa na tarakimu (nambari za siri)
Kuna Satanism (imani za kishetani) zimepewa jina baya lakini zimejaa maarifa mengi na yenye nguvu sana .. Mengine yanatisha kwakuwa yana connection ya moja kwa moja na nguvu za asili.. Hawa ni wababe wao mambo ya kiroho
Paganism.. Wasiamini katika chochote bali imani hao😀.. Wenye kutafuta uwiano kati ya hao wengine Wote.. Wasiojua chochote kuhusu nambari za siri, wasuojua chochote kuhusu ulimwengu wa roho.. Wasiojua chochote kuhusu asili..
Waamini wa kwamba kila kitu kipo kwa sababu kipo(bila kufafanua sababu yenyewe) hakuna mwanzo na hakuna mwisho.. Hakuna Mungu, hakuna miungu wala hakuna roho! Wakizaliwa wanezaliwa na wakifa wamekufa!
Wakipata wamepata na wakikosa wamekosa! No more reasoning.. Hawa ni stress free species .. Hawajisumbui kwa lolote lile!
Hitimisho: colabo ya hawa watatu umezifanya dini zetu zote kuwa mateka wao na mafundisho yao kwa sehemu kubwa ndio yanatawala mahubiri ya kila siku kwenye nyumba za ibada zenye kumwamini Mungu mkuu..