ULINGANISHO WA UBORA: Tanki la Maji la Plastiki vs, Tanki la bati au chuma. Lipi imara?

ULINGANISHO WA UBORA: Tanki la Maji la Plastiki vs, Tanki la bati au chuma. Lipi imara?

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Tanki la kuhifadhia Maji la Plastiki dhidi ya tanki la chuma

Unapotafuta tanki la kuhifadhia maji ya mvua au hata ya bomba kwa ajili ya matumizi ya baadae huko sokoni utapata matanki ya kila sampuli ambayo yametengenezwa kutokana na malighafi tofauti. Sasa kwa leo tuangalie haya mawili.

Kama umekuwa ukifanyia utafiti matanki ya chuma cha pua basi utakuwa umeshayaona yale ya kuunganisha kwa boriti ambayo hayashiki kutu (stainless) na haya ya plastiki (poly tanks) ambayo ni mengi utakuwa umeyaona kila sampuli hapa Tanzania yapo kila kona.

Binafsi kwenye ka compaund kangu natamani niweke haya ya chuma...sasa nikasema wacha nilete hii analysis niliyoinasa huko kwa wenzetu.

TUANGALIE SIFA LINGANIFU ZA MATANKI HAYA

Yale ya chuma: Sifa zake

  • Matanki ya chuma cha pua yana maisha marefu ya kutoa huduma ya kuhifadhi maji (ingawa yana gharama kubwa unapoyanunua ikilinganishwa na tanki la plastiki ambalo bei yake ni chee).
  • Matanki ya maji ya chuma hayawezi kushika moto - labda hii inaweza kuwa faida kwa maeneo ambayo yana moto wa msituni hasa wale ndugu zangu mnaoweka matanki haya kwenye bustani huko maporini kv kwenye bustani za vitunguu nk.
  • Kwa kuzingatia kwamba matanki ya chuma ni mazito...ni vigumu kwa wezi kuiba kirahisi ukilinganisha na yale ya plastiki ambayo huibwa mara kwa mara.
  • Matanki ya chuma ni vigumu kutoboka kwa muda mfupi na hayaathiriwi pakubwa na joto...tofauti ya yale ya plastiki ambayo hukauka hasa kwenye maeneo ya kitropiki kama Dar es salaam ambako jua huwaka sana.
  • Matanki ya Chuma ni rahisi kuyatengeneza yanapopata hitilafu. Ni suala la kumuita mtu wa fabrications au nut and bolt guy anakuja anafix tu mara moja. Unlike tanki la Plastiki likitoboka inabidi uachane nalo...kwa sababu hata likiungwa kwa moto ubora wake hupotea.
  • Matanki ya chuma hupunguza uwezekano wa maji kuwa contaminated au kuchafuliwa na fangasi na algae ambao wana athari kwa mtumiaji wa maji
  • HIVYO BASI kwa mtazamo wangu nadhani kama una uwezo ni vema kutumia tanki la chuma...japo kwa hapa kwetu Tanzania hayapatikani kiurahisi.
  • images.jpg
    plastic vs stainless steel.jpg
 
Hasara zake?
  • Matanki ya chuma gharama zake ni kubwa (initial costs) ukifananisha na matanki ya plastic. Ingawa kwa long term inaweza kua cost ndogo. Mfano ndani ya miaka 10 ulienunua tank la chuma utaendelea kupeta mimi wa tank la plastic naweza badirisha ata mara mbili.
  • Kama maji yana madini yanaweza sababisha kutu. Chuma nyingi wanazifanyia galvanized ili kuzuia kutu (oxidation reduction topic form 3), sasa ikikutana na maji yenye madini mengi mfano ya chuma, inasababisha reaction kutokea tena, mfano Maji ya kule Morogoro wilaya za Ifakara unakuta yana madini ya Ulanga, ulanga ina chuma sana. (Ila hii point wataalam mnaweza ni pinga).
  • Matank ya Chuma unavonunua nunua kubwa kabisa. Maana unaweza nunua dogo kwa bei kubwa, baada ya muda unaongeza matumizi, gharama ya kununua jingine inakua hasara mara mbili.
  • Matank ya Chuma mazito balaa. Kuliamisha lazima ukodi watu au gari spesho (winchi).
Ila point zako zina uzito zaidi. Ata mimi ningechagua matank ya chuma over ya plastic kama bajeti sio tatizo.
 
Marehemu mshua angu alinunua simtank mwaka 1994,hadi leo lipo fiti na linapiga kazi fresh tu,linamsaidia sana bi mkubwa,kitu kilichobadilishwa ni kifuniko cha juu tu,kilirushwa na upepo kufika chini kikapasuka,siwaelewi kabisa mnaosema eti yale ya plastik hayadumu,lina miaka 27 sasa na halina hata dalili ya ubovu.
 
tank za chuma zinapatikana wapi hapa mjini DSM, ARUSHA NA DODOMA? KWA Anayejua tafadhali.
 
Back
Top Bottom