Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 12,675
- 25,924
actually, wenye macho ya kiroho, wanatakiwa kujua na kutangaza kwamba wakati dunia kufika mwisho umekaribia sana au soon utafika. mwenye sikio na asikie. kila kilichotabiriwa, tangu kuharibiwa hekalu la Yerusalem na warumi na Yerusalemu kutawaliwa na mataifa kwa muda, (na kweli ilitokea hivyo hadi 1948), kuchanua tena kwa mtini ambako kumetimia kwa kuzaliwa taifa la Israel 1948 miaka 400 taslimu tangu wasambaratishwe, miaka ile ile sawa na waliyokaa miseri (hiyo miaka didn't tally kwa bahati mbaya), vita vinavyotokea sasaivi, namna mataifa yanavyoichukia Israel na wayahudi, na mwisho, injili kuhubiriwa mataifa yote.Tumeonya Sana, tumehubiri Sana, tumeshuhudia sana kuhusu Vita zinazoendelea ya middle East.
Viongozi na watu mbalimbali wameonywa Sana kuhusu taifa LA Israel. Mpango wa Mungu kuhusu Israel lazima ukamilike.
Ahadi ya Mungu kuhusu Israel lazima ikamilike. Biblia imesema waziwazi kwamba wa Israel Wataokolewa na Yesu Mwenyewe hapo siku za usoni. (Warumi 11:26). Waisrael wote watamuamini Yesu kipindi cha utawala wa serikali moja ya dunia.
Kwa hiyo Ulinzi uliopo pale ni mkubwa mno, Mungu Mwenyewe anahusika na huu Ulinzi.
Vilevile Mungu hutumia wanadamu kulilinda hili taifa. Nchi za ulaya, USA nazo Zinatumika. Kanisa la Mungu duniani nalo hutumika kwa maombi ya Watakatifu. Kwa hiyo adui sio rahisi kupenya pale.
mtu ataniuliza, injili imehubiriwaje? sasaivi kwa njia ya internet (youtube, tiktok, instagram, x, n.k popote hata ukiwa china wanakozuia injili, kuna namna utapata kusikia kuhusu Yesu. labda iliyobaki, though sina uhakika ni Korea kaskazini ambayo nayo hata kama bado soon injili itafika. kwanza hata ile wanavyokamata watu wenye Biblia na kuwafunga korea kaskazini na kuwaonyesha raia wake wote wasiwe na Biblia ama la watafugwa, wanakuwa wameshawapelekea injili kwa namna moja. Yesu alisema sharti lazima injili ihubiriwe kila eneo, ndipo mwisho utakuja. ndio maana huwezi kuniuliza kwanini tangu zamani tunasikia dunia inaisha na haijaisha, shurti injili uhubiriwe, na kwa sasa ni eneo dogo sana la dunia injili haijafika.
maarifa kuongezeka, fikiria kuhusu AI, computer, hayo mavitu elon musk anarusha n.k., Yesu alitabiri tukiona dalili, tuchangamke, yupo malangoni.
wewe pia unayesoma hapa uwe wa dini yeyote ile, injili umeshaisikia. kwa nini Yesu alisema injili lazima isikike kila mahali? ili siku ya hukumu asiwepo atakayejitetea kwamba hakusikia injili. kuna hukumu ipo mbele yetu, kila mtu atavuna alichopanda, uamuzi ni wako sasa. vita vya Israel na yeyote visitutoe kwenye reli, tutazame kule mbele Yesu Kristo alipo, na shika sana ulicho nacho asije mwovu akaitwaa taji yako ya uzima.