mackj
Member
- Jul 25, 2023
- 84
- 98
Kambi ya jeshi la polisi kikosi cha kutuliza ghasia FFU kilichoko mtaa wa uwanja wa ndege kata ya kamunyonge manispaa ya Musoma kinaendesha zoezi la ulipuaji mabomu na silaha za kivita ovyo bila utaratibu wakati wa mazoezi yao bila kutoa tahadhari kwa wananchi jambo ambalo limekuwa kero na kuzua taharuki kwa wananchi wa kata hiyo na kata jirani hasa kwakuzingatia kuwa kambi hiyo iko katikati ya makazi ya watu na pia imezungukwa na taasisi mbalimbali za kijamii kama vile mahospitali, shule, na nyumba za ibada
Kambi hiyo inapakana na shule ya msingi kamunyonge pamoja na shule ya awali ya kanisa la PAG na upande wa hospitali kambi hiyo iko jirani na zahanati ya kamunyonge, na hospitali ya OMEGA na hospitali ya AIC
Watoto ni waathirika wakubwa wa kadhia hii wanakuwa na hofu sana katika shule hizo ziko jirani na kambi hiyo kipindi wanapolipua mabomu na kufyatua risasi zao bila kutoa tahadhari kwa uma jambo ambalo ni kinyume na sheria ya mazingira sura ya 191 kifungu cha 106 (5na 6) na kanuni za udhibiti wa kelele za mwaka 2015
kundi lingine lililoko kwenye hatari kutokana kadhia hiyo ni wagonjwa mahospitalini ni hatari sana kwa afya zao hasa wale wenye shinikizo la damu na magonjwa mengine yanayohitaji utulivu
Kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira Sura ya 191, Kifungu cha 106 (5 na 6)
kinakataza kupiga kelele kuzidi viwango vilivyoruhusiwa na vilvile ni kosa
kupiga kelele kinyume na viwango vilivyoruhusiwa. Kanuni za udhibiti wa
kelele na mitetemo za mwaka 2015, zimeainisha viwango vya sauti
vinavyoruhusiwa kwenye maeneo ya makazi, biashara, viwanda na hospitali
ili kulinda afya ya jamii.
Viwango hivyo vinatofautiana kwa usiku na mchana (Mchana ni kuanzia saa
12 asubuhi mpaka saa nne usiku) na usiku ( saa nne usiku hadi saa kumi na
mbili asubuhi.
Usiku viwango viko chini zaidi kwa kuwa ni muda ambao jamii
inahitaji kupumzika.
Inasikitisha kuona vyombo vilivyokabidhiwa kusimamia sheria ndivyo vinavunja sheria bila haibu
Tunaomba mkuu wa mkoa Mara kwakuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kamati ya usalama ya mkoa aingilie kati jambo hili linalokiuka sheria ya mazingira
Imeandikwa na mimi makiwa jumanne kabasa
Kambi hiyo inapakana na shule ya msingi kamunyonge pamoja na shule ya awali ya kanisa la PAG na upande wa hospitali kambi hiyo iko jirani na zahanati ya kamunyonge, na hospitali ya OMEGA na hospitali ya AIC
Watoto ni waathirika wakubwa wa kadhia hii wanakuwa na hofu sana katika shule hizo ziko jirani na kambi hiyo kipindi wanapolipua mabomu na kufyatua risasi zao bila kutoa tahadhari kwa uma jambo ambalo ni kinyume na sheria ya mazingira sura ya 191 kifungu cha 106 (5na 6) na kanuni za udhibiti wa kelele za mwaka 2015
kundi lingine lililoko kwenye hatari kutokana kadhia hiyo ni wagonjwa mahospitalini ni hatari sana kwa afya zao hasa wale wenye shinikizo la damu na magonjwa mengine yanayohitaji utulivu
Kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira Sura ya 191, Kifungu cha 106 (5 na 6)
kinakataza kupiga kelele kuzidi viwango vilivyoruhusiwa na vilvile ni kosa
kupiga kelele kinyume na viwango vilivyoruhusiwa. Kanuni za udhibiti wa
kelele na mitetemo za mwaka 2015, zimeainisha viwango vya sauti
vinavyoruhusiwa kwenye maeneo ya makazi, biashara, viwanda na hospitali
ili kulinda afya ya jamii.
Viwango hivyo vinatofautiana kwa usiku na mchana (Mchana ni kuanzia saa
12 asubuhi mpaka saa nne usiku) na usiku ( saa nne usiku hadi saa kumi na
mbili asubuhi.
Usiku viwango viko chini zaidi kwa kuwa ni muda ambao jamii
inahitaji kupumzika.
Inasikitisha kuona vyombo vilivyokabidhiwa kusimamia sheria ndivyo vinavunja sheria bila haibu
Tunaomba mkuu wa mkoa Mara kwakuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kamati ya usalama ya mkoa aingilie kati jambo hili linalokiuka sheria ya mazingira
Imeandikwa na mimi makiwa jumanne kabasa