Mambo ya kuanza maisha.
Baada ya kumaliza chuo nilirudi zangu zoo kupumzika, baada kama ya mwaka hivi nikatimba mjini.nikafikia kwa mshkaji tuliyekuwa nao chuo, tayari ana ajira, anaa chumba kimoja,sinza.
Demu wa jamaa akawa anakuja jamaa anapiga mashine, na mimi nipo gheto, mateso makubwa nilikuwa nipata. yule binti mwanafunzi wa IFM, kila weekend lazima amletee jamaa anapiga mashine na mimi nimo bila huruma. Kuna siku washenzi wale walianza kupigana mashine mchana na mimi nipo, nikasepa zangu, yaani tulikuwa tunakula story fresh tu mara ghafla mizuka ikawapanda, nashangaa, yule demu tayari kakalia mashine, nikatoka nje machozi yananilenga lenga.
Sasa jamaa akaja pata demu mwingine kazini kwake huko,akaanza kumkwepa mkwepa yule denti, mpaka ikafikia point yule denti akagundua jamaa anademu mwingine na ndio maana jamaa anamkwepa. siku ya siku demu kaja kabana mitaa ya jirani, tunachat ananiambia yuko kwao, tegeta huko, ananiuliza kama jamaa kaisharudi,jamaa naye tunachat ananiuliza kama yule denti kaja, mi nawajibu wote ukweli, ila sikuwaambia kama kila mmoja ananiuliza.MISTAKE.
Baada ya muda, jamaa kaja, kumbe kaja na yule demu wake mpya, huyu hakuwahi kumlia mle ndani walikuwa wanaenda lodge ya jirani, ile namtumia meseji denti kwamba jamaa kafika, yaani ile naisend tu, demu mpya na yeye anaingia.MISTAKE NO.2
Hazikupita dak kumi, yule denti akatimba gheto, ukatokea ugomvi wa kuuwa mtu, jamaa na demu wake mpya wakakimbia baada ya kuwa nimemdhibiti huyu denti sababu alikuwa kama kichaa sasa. saa mbili usiku.
Namtafuta jamaa kwa simu kazima, hapatikani, Ijumaa hiyo, tukaa na shemeji mle ndani, nikamuambia twende tukale nimsindike, akasema ye haondoki hadi jamaa arudi anataka aelewe msimamo wa mahusiano yao.nikaenda zangu kupiga msosi, nikiwa huko akanitumia sms nimpelekee kitimoto na ndizi na bia mbili, nikambebea.
Kwa kifupi usiku huo nikala mzigo, asubuhi jamaa ananipia simu nikamuambia huyu yupo kalala hapa anamsubiri, akasema yeye harudi hadi jtatu jioni, nikamuambia amuambie ili aelewe, jamaa hataki hata kumtext demu wake, nikala tena mzigo siku nzima. jumapili nikamsindikiza mpaka kwao, nikala mzigo hapo hapo kwao, akachukua nguo tukarudi gheto, nikala mzigo, mpaka nilikonda.