Miaka kadhaa nyuma nikiwa ndio kwanza nimepata kazi katika mkoa mmoja hapa Tanganyika.
Nikapata habari ya msiba wa ndugu wa dada ambaye nilisoma naye katika mkoa huo.
Huyu dada alikuwa haishi mkoani hapo hivyo alisafiri kuja kuhudhuria msiba. Kwa kuwa nilikuwa mkoani hapo nami nikapanga kuhudhuria pia na nikaulizia namna ninavyoweza kufika maana ilikuwa ni safari ndefu japo ni ndani ya mkoa.
Hatimaye nilianza safari siku moja kabla ya mazishi ili kumpa kampani classmate. Nilifika msibani majira ya saa kumi jioni na kupokewa na classmate ambaye wakati huo alikuwa ni mke wa mtu tayari.
Kutokana na pilika pilika za msibani na ukizingatia kuwa ni mke wa mtu basi akanikabidhi kwa mmoja wa rafiki zake ambaye alikuwa akifanya kazi mkoani lakini alikuwa anatokea eneo hilo hilo msibani, huyu alimsindikiza classmate kwenye msiba. Hivyo huyu dada ndio akawa amekaa na Mimi maana msibani hapo watu walikuwa wamekaa makundi makundi wakiongea kilugha.
Binti mweupe, mwenye mwili wa wastani, mcheshi na mwenye haiba ya kike ndio akawa ananipa kampani pale msibani.
Majira ya saa moja binti akaniomba akaniwekee begi nyumbani kwao lakini pia aliniomba nikaoge huko kwao. Tulifika nyumbani kwa yule dada mwendo wa Kama dakika tano hivi, ndipo nikagundua kuwa wazazi wake walikuwa safari ila kulikuwa na kijana mmoja pale ambaye alikuwa akilinda mji.
Kwa hali ya hewa ya kule, ilibidi dada achemshe maji na kunionyesha chumba kwa ajili ya kubadili nguo. Nilioga na kumaliza Kisha tukarudi msibani ambapo tulikula na kuzungumza na classmate mpaka saa tano usiku. Kadiri muda ulivyokwenda ndivyo mazoea yakaongezeka. Sasa tuliweza kucheka na hata kutaniana.
Dada aliniambia inabidi nikale kule kwao, hivyo safari ilianza.
Tukiwa njiani kuelekea kwao na huyu dada, ndipo mazoea yalipovuka mipaka, maana tulitembea tukiwa karibu sana, huku tumeshikana mikono.
Tulipofika kwao, nikaingia chumbani na binti pia akaingia chumbani kwake.
Majira ya saa sita na nusu binti akaja kunigongea na kuniuliza kama nahitaji blanket maana kitandani kulikuwa na shuka tu. Nikamjibu, blanket la aina gani? Binti alicheka kisha akajibu blanket la kujifunika. Nikamjibu hapa nahitaji kukumbatia sio kujifunika. Binti aliinama Kisha akaniambia, ungetaka kukumbatiwa si ungekuja na mwenzako. Aligeuka na kuondoka.
Nami nikajilaza. Dakika kama kumi baadaye alirudi akiwa na blanket aligonga mlango na kupitiliza kitandani, huku akiniaambia, sogea tulale. Ni aina ya wale wanawake wenye vilio na kurusharusha miguu.
Sikuwa na kipingamizi zaidi ya kusogea na hatimaye nikala tunda usiku.
Siku ya pili msibani, nikiwa na classmate nikamuuliza kama rafiki yake ameolewa akanijibu kuwa ameolewa kwa ndoa kabisa.
Nilikula mzigo tena usiku ule, alfajiri nikadandia basi kurudi mkoani.
Sikutaka hata mawasiliano na mke wa mtu.
Sent using
Jamii Forums mobile app