Kimasihara Mkambi ya Wasabatho na kuchezea Kichapo.
KIBWAGIZO
“…..Mtoto Sonia mimi, nimekuzimia. Katika kukupenda mimi nimeonesha nia. Njoo soniaaa, soniaaa, mi nakupendaaa, kupendaaaa, njoo soniaaaa,soniaaaa tupeane dendaaaa, tupeane dendaaa x2..”
UTANGULIZI
Ilikuwa ni siku Ijumaa (Sikukuu) nikiwa getho nikijiimbia mwenyewe wimbo huo , huku nikimsubiri kipenzi changu Nyanjiga, toto la kijita huko Majita. Huyu ni binti niliyekuwa nasoma nae kidato cha Tatu, yeye akiwa F3B, mimi nikiwa F3A katika shule ya Sekondari Nansimo (siyo jina halisi).
Huyu mpenzi wangu, tuliahidiana kukutana saa 5 asubuhi, kwenye makambi ya Wasababtho yaliyokuwa yanaendelea jirani na nilipokuwa nimepanga. Lakini hadi muda huo unafika alikuwa hajafika.
Nilianza kupata wasiwasi baada ya saa zima kupita bila kufika, lakini bado moyo ulinambia Nyanjiga hawezi kuniangusha. Na mara nyingi alivokuwa akipata dharura alikuwa akimpa kimemo rafiki yangu Kanywagale ambaye walikuwa wanaishi nae jirani. Ila safari hii, mambo yalikuwa tofauti. Saa 6:13 bila kumuona Nyanjiga wangu. Hatuna simu na siwezi kumpata kwa namna yoyote ile.
Nilihuzunika sana siku hiyo, lakn ghafla akili ikanambia nenda barabarani ukamsubirie huko, akitokea uje nae upate Kanchude. Ukweli nilienda barabarani, nikawa naangaza angaza ili nimuone Nyanjiga wangu, bahati mbaya sana hadi namaliza saa zima na madikika mengi, Nyanjiga hakuonekana.
Ilivyofika saa saa nane nikiwa nimekodolea upande anaotoka Nyanjiga niliona mdada mmoja kwa mbali, nuru ikaanza kuonekana usoni, tabasamu likarejea, lakn kadri yule binti alivyokuwa akisogea nilitambua kuwa si mwenyewe. Ni mwingine tu.
Njaa ilianza kuniuma, nikaamua nilirudi tu nyumbani, nipate labda chochote. Kama mjuavyo ndugu zangu cha tumboni ndo kinashikilia cha kichwani. Nikaamua kuondoka. Nilivofika kwenye maeneo ya makambi nikaamua kumtafuta Nyanjiga wangu! Zuungusha shingo, zungusha wapi? Zungusha shingo, zungusha wapi? Duu. Nikaamua kwenda tu Getho.
Nikiwa nakaribia getho, ghafla roho ikanambia emu rudi mara ya mwisho ukaangaze tena labda anaweza kuwa anakuja. Kweli nilirudi nikakaa barabarani nikiwa nakodoa sana, macho yameshauma, njaa inauma lakini Nyanjiga hakutokea. Zile hisia zote za usiku kwamba leo nitakuwa na Nyanjiga zimekwenda bila kujibiwa. Ule wimbo wa mtoto Sonia, leo nimeimba bure daah, kufanya usafi na kutandika kote kule? (Godoro naweka kwenye jamvi). Hadi saa 10 na madakika mengi nikaamua kuondoka tu nikiwa nimekata tamaa.
Nilifika nyumbani, nikawasha jiko la Mchina nikapika ugali, lakini kwa kweli ni kama hamu ya kula haikuwepo tena. Nyanjiga amenitawala, mara nimlaumu kwa kunidanganya, mara nimuone hana kosa. Mara nawaza tuachane, mara naona tuendelee tu. Nitamuacha kwa kosa gani, lakini kwa nini hakuja? Ahh, anyway nikakomba mboga, nikanawa na kutoa vyombo, hata bila kula vizuri. Baada ya hapo nikajilaza kwenye kigodoro changu japo nipumzike.
Nikiwa kwenye kigodoro hapo, hisia zilianza kunijia, mwili ukawa unahitaji Kanchude, ikafikia hatua naona kabisa nashindwa kuutawala uume wangu mwenyewe. Natamani Nyanjiga aje anioke lakini ndo hawezi kuja. Jamani kweli mapenzi na shule ni mlenda na chai.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Muhtasari wa Makambi ya Wasabatho.
Jirani na nilipokuwa nakaa, yalikuwa yanafanyika makambi ya Wasabatho ambayo yalikuwa yahitimishwe Jumamosi. Ili Jumapili kila mtu arudi alikotoka. Na Baadhi ya Wanamakambi walikuwa wamefikia pale nilipokuwa nimepanga. Walikuwa kama 11 Wamama 5, na wadada 6. Wanaume wao walikuwa wanalala kwenye ghala la pamba (Wao wanaita Stoo) na hapo stooni ndo makambi yalikuwa yanafanyika jirani na Kanisa la wasabatho la mahali hapo. Wenye ndugu walikuwa kwa ndugu zao. Nafikiri wasabatho wanaelewa. Ulikuwa Mkutano haswa.
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
NAMI NAENDA KUSHIRIKI MAKAMBI YA WASABATO
……..Nikiwa kwenye kigodoro changu hapo, hisia za kufanya mapenzi zilianza kunijia, mwili ukawa unahitaji Kanchude, ikafikia hatua naona kabisa nashindwa kuutawala uume wangu mwenyewe. Natamani Nyanjiga aje anioke lakini ndo hawezi kuja. Jamani kweli mapenzi na shule ni mlenda na chai……’ sasa endelea….
Ilikuwa ni Saa 12 Kasoro, niliingia eneo la makambi ili niende kuushitaki uume mbele ya mchungaji. Maana nilifika pale nikiwa nimeweka mikono mfukoni, na hata nilivyo kuwa natembea ndugu, wanaume wenzangu mtakuwa mnajua. Hivo sasa! Nilisimama kona moja hivi, ghafla wimbo fulani ukapigwa, naukumbuka kidogo;
‘’ Mimi hapa natamani kumuona Yesu, akija kwa fahari nao Malaika. Usitamani ya dunia, kwani hayo ni ya muda kitambo, uifikirie kesho, ili nawe uwe mshindi. Ewe mwenzangu kazana, ili uwe katika lile kundi, litakalo vikwa na Yesu taji la Johari” (Hapa naomba uingize sauti ya kisabatho wakiwa wanaimba)
Kipindi huo wimbo unaendelea ghafla aligeuka dada mmoja, tukagonganisha macho. Ni moja ya wale wadada 6, waliokuwa pale kwa mother house wangu. Haikuwa sura ngeni kwa sababu tulikuwa tunaonana, nikitoka shule. Basi tukatizamana kidogo, afu akatoa uso. Mi jicho langu likabaki kwake. Then, ikaja sijui ndo kufungua sabatho. Basi wakafungua, saa 12 hivi. Walipomaliza nyimbo zikaendelea.
Katika kufungua sababtho, Yule mchungaji kuna maneno aliyasema, ambayo sikuyapenda, kama alikuwa ananiambia mimi jambo fulani. Kichwani, nimeanza kupanga namna ya kumpata huyu mdada, lakini mchungaji anahimiza maadili na kuepuka zinaa na uzinzi kwenye makambi, daaaah.
Ukweli neno liliningia, ila sasa nitafanyaje? Roho i-radhi, lakini mwili ni dhaifu. I must try the best of my luck.
Tulitawanyika, wakaanza kuondoka mimi nikamfuata Yule dada, tukaanza kwenda nae nyumbani, tumekaribia kuingia ndani ya uzio (Uzio wa Matete), nikamwambia naitwa Lugumya, sijui unaitwa nani? Naitwa Nyamumwi! Okay sawa.
Nyamumwi mimi nakupenda bn, na ukweli katika makambi haya sijaona mwanamke anayevutia kama wewe. Ikiwezekana….. (akanikatisha… mama huyo anakuja). Akakimbia kuingia ndani, huku akinambia baadae kwa sauti ya chinichini.
BAADAE INAFIKA.
Ikiwa ni mida ya saa mbili usiku nikaamua kukaa sehemu ambayo wakitoka lazima niwaone. Kweli walitoka, wote 11 plus wa pale nyumbani. Wakaenda, mi nikiwa ninachora ramani walipoenda kukaa, nikavutavuta kidogo lakini moyo ukiwa unanimbia mbona mida ndo hii. Lakini namtoaj pale kwenye kundi la Wenzake.
Akili ikiwa inaendelea kuchakata namna ya kumpata na kuongea nae. Nikapata wazo, tumia binti wa mother house, nikamwita alikuwa kwenye makambi pia (Msichana wa Darasa la 7), nikamuuliza unamfahamu Nyamumwi, akanambia ndiyo. Naomba ukamwite basi, mwambie namuita. Akasema poa.
Kweli wajumbe, akanifanikishia, akaja, tukatafuta kagiza, kule kwenye kagiza nilijaribu kumgusa akakataa. Akanamabia tutakutwa, wewe tangulia nyumbani, nitasema nakuja kujisaidia afu nitakuja kukusikiliza. Sawa? Nikasema sawa! Akaondoka
Mi nae mdogo mdogo getho, mlango nikaacha wazi. Kila baada ya dakika 3 nilikuwa natoka kwenye kagodoro kwenda kuchungulia, hollaaa, dak 2 nachungulia hollaa, nikaanza kujisemea ya Nyanjiga yanajirudia. Wadau hapo, uume hautambui tena kama kuna mtu anaitwa Nyanjiga bali unamtambua Nyamumwi. Ukawa unasimama, naukunjia kwa nyuma, naubana na miguu (Wanaume hii mnaijua vizuri tu hahahaha). Nikaamua sasa nikasimame mlangoni kabisa.
Sasa nikawa natoka mlangoni naenda nje kumchungulia kama anakuja, huku nikitembea uume umebanwa kwa nyuma. Chungulio la kwanza likuwa kapa, la pili kapa, ila la tatu, ukweli nilmuona anakuja. Kiroho cha hofu kikanipata, nikakimbia fasta kurudi kusimama kwenye mlango wa getho.
NYAMUMWI ANAINGIA GETHO NA KULIWA KIRIBOY, LUGUMYA APATA KICHAPO.
Alivofika, nikamshika mkono nikamkaribsha ndani, nikarudishia mlango ila sikuufunga. Tukakaa kwenye kigodoro changu, mimi nilichofanya ni kumlaza tu kwenye hicho kigodoro, tukalana mate, nikapenyeza vidole kwenye Underskirt kuitafuta chupi, kweli nikapata chupi nikaingiza kidole nikachezea chezea.
Kidogo tu akanambia ngoja nivue, akavua chupi tu, nyingine akazisogeza kwa juu, lakini maziwa nilikuwa nayashikia kwenye nguo humo humo. Mi nilivua, nikabaki na pensi, goma lilivoanza nikaivua kabisa hiyo pensi. Kipindi hicho hatukuwa tunavaa chupi. Nikaingia nikaanza kuchakata, yaani wajita wanakatika wewe asikwambie mtu. Waliowahi kuwala ni mashahidi.
Tukiwa tunakulana kumbe dirisha moja nilikuwa sijafunga top, zimebaki zile nyavu za kuzuia mbu, dirisha lenyewe lilikuwa dogo na chumbani kulikuwa giza na kimwanga hicho kidogo cha dirisha.
Ambacho hatukujua kipindi anakuja kuliwa, kumbe mtoto wa kiume (form 1) wa yule mother house alimuona. Kwa hiyo akamfuatilia na kubaini kuwa yuko room kwangu. Akaenda kumtonya mama yake. Sisi hatuelewi tunaendelea tu na mambo yetu. Maana nilipiga cha kwanza, nikaunga kutafuta cha pili.
Sasa utamu ukiwa umekolea, mtoto akawa anagugumia, kwa kilugha inulileeee, inulileeeee, inulile Lugumyaaa!, lugumya nanaaa, nana lugumyaaaa, lugumya aoooo, aoooo weee, aooooo weee, nkola lugumya, nkolaa enikwendaa, unana kisi wee, ahahhahahaah, Nyamumwi awe, basila wee! Ulyaki sinu go! Hahahahah! Mi nikawa napump tu. Yeye anaendelea kuongea kilugha chao, wajita nafikri wataelewa.
NACHEZEA KICHAPO.
Nikiwa naendelea kuyumba kwa mtani wangu wa majita Nyamumwi, nimejisahau kabisa kama tumejiiba tu, kumbe mother house alikuja na fimbo akasukuma mlango taratibu akaingia. Nilivyorudisha makalio juu ili nipush kuingia ndani nikakutana na kiboko huko juu na kushuka nacho.
Nikapiga kelele, mamaweeee, mamaweeee, nikajitoa nikachezea kichwani, nikapitia surauali kwenye kamba, kumbe nimechukua koti. Nikawa nakimbia navaa naona mguu haungii. Nikaingia kwenye chumba cha mpangaji mwenzangu ambaye alikuwa ni wanafunzi pia. Mguu huko kwenye mkono wa koti sehemu nyingine nimefichia makalio. Hakika niliumbuka. Jamaa akiniona, anacheka afu mm natetemeka, kukamatwa na mother house. Nitasomea wapi? wazazi wangu wakijua? Shuleni wakijua? Daaah!
Nikafungiwa kwenye hicho chumba, mother akaamru kifunguliwe hatukufungua. Akaongea sana hapo. Akanambia, kesho nihame hapo kwake. Asubuhi kulivokucha nikaingia room yangu, nikachukua suruali nikavaa, nikaenda kwa binamu yangu alikuwa anakaa kwenye hicho kijiji. Jumapili, wale wakaondoka. Mi nilirudi jioni. Nikawa namkwepa. Akaniona akaniita, nikaenda. Nilivofika, nilianza kulia, akanionea huruma. Nikabaki pale hadi nikamaliza Shule yangu.
Nyamumwi sijawahi kuonana nae tena. Yule jamaa niliyeingia chumbani kwake na koti badala ya surauali, akawasimulia wadau. Wakawa wananitania kwa jina la Bwn Kakoti. Nyanjiga yeye, kumbe aliugua maralia, ndo maana hakuja.
Naomba kuwasilisha
Lugumya.