Ulishawahi kutengwa na rafiki yako wa karibu baada ya yeye kufanikiwa? Toa kisa chako ilikuwaje

Ulishawahi kutengwa na rafiki yako wa karibu baada ya yeye kufanikiwa? Toa kisa chako ilikuwaje

Mi nilimchukua mshkaj flan ambae tulimaliza wote shule,akaleta shida kwao wakamfukuza,akaja home nikaa nae sana kakaangu mkubwa akamtafutia kibarua,yaani kwa ufupi mwamba tulimgeuza kama ndugu kabisa,Mungu si Athumani katika mishe zake akatoka sijui alichofanya hadi akafanikiwa anajua yeye,kimya kimya akajenga mbezi hii ya kimara,mara kajenga chanika kimyakimya,ghafla akasema anaenda kumsalimia mamaake! Ndio kimoja hakurudi,hilo halikuwa tatizo ila shida ilikuwa moja tu alisepa na mke wa bro(aliemtafutia kibarua)
Hapo kakosea sana, tena sana.

Yaani hakuwaona wote hawa mpaka kwenda kuvunja ndoa ya aliyekufadhili.

Msaada wenu umewaponza.

Poleni sana WADAU
 
Haya maisha ya wanaofanikiwa kujitenga nami yamekuwa msisha yangu kila mara. Watu wa namna hii wana tabia zinazotofautiana. Kuna waliofanikiwa na kusahau kwamba tulitaabika wote. Hata nikijaribu kuwtafuta, wanajifanya kuwa na shughuli nyingi. Wengine wanakata kabisa mawasiliano, kiasi kwamba siwezi kuwafikia. Wengine wakishindwa kunikwepa, wanazusha zengwe la kunichafua. Wengine hata kujaribu kunifanyia kitu kibaya ili kuniondoa endapo kuna kitu wanaficha ambacho nakijua. Hayo yote ni maisha. Kikubwa ni kutengeneza mwelekeo wa maisha mwenyewe bila kuwategemea. Hii imesababisha kusonga mbele bila kutetereka na kuyaona ni ya kawaida.
 
Kinachosababisha urafiki uwepo kikibadilika au kufa na urafiki unabadilika au kufa. Usisahau hiyo pointi ukiwa kwenye urafiki na yeyote.

Mkiwa hamna kazi wote, mtakuwa marafiki kwa sababu mtafanana vitu vingi, ili urafiki uendelee ni labda mbaki hamna kazi au kila mtu apate kazi na zisiwe na tofauti kubwa. Mkiwa matajiri, mbaki matajiri, mmoja akifilisika, urafiki utaishia hapo. Mkiwa wanafunzi, uanafunzi usiishe, ukiisha na urafiki unaishia hapo, labda mpate kingine kitakacho sababisha urafiki uwepo.
 
Na hii ni kwa sababu kinachowaunganisha kikibadilika au kutokuwepo, mahitaji yenu ya kisaikolojia yanabadilika. Kuna mmoja atabaki toleo la zamani lenye mahitaji ya zamani, na mwengine amekuwa mpya hivyo ana mahitaji mapya. Na kila mmoja atamuona mwenzake kituko, japo aliyeachwa nyuma kimaendeleo atahisi anaonekana kituko zaidi.
 
Mi bado muangaikaji ambae siijui kesho yangu inakucha vipi ila naamini Mungu atanionyesha mlango pia. Tusiwapuuze watu tunaokuwa nao kwenye kipindi kigumu pindi tunapofunguliwa njia za mafanikio. Japo kuna ubize lakini si mbaya tukajuliana Hali tu..
Kweli kabisa
 
Kuna mwamba A level tulikia karibu mnoo na nimempa tag sana aisee bila kujisifia, sehem alipokua anakaa jiran kuna dogo anafanya kibarua cha usafi kwenye hizi ngo's wana deal na volunteers wa nje mambo ya kijamii...bas alikuja dem mzungu pale akatokea kumzoea yule dogo mfanya usafi akawa anamtembeza maeneo mbali mbali hadi kwao ndo kukutana na mwamba huyu niliesoma nae! picha linaanza jamaa english inampa tabu kuongea na kuandika dem alivorudi U.S nikawa namuandikia mimi barua kwa maneno yangu mwenyewe nachombeza kinoma had kuna muda dem alitaka waachane kisa distance aisee nilijifanya shakespear hatari 😁 niliandika batua za kum please sana yule bambadi... doooh jamaa kuja kupata invitation ya kwenda mbele picha linaanza wakaandaa sherehe kwako ya kumuaga! Mimi na dogo msafisha n.g.o wote hatujaalikwa yan nilifabya kupigiwa simu na mshkaj mwengne tena kuniuliza vp tunaenda sa ngap kwa flan kumuaga, hua najuta kwenda kwenye ile sherehe mpaka leo mana sikuitwa! anyway mpaka leo mwamba yuko USA zaid ya miaka 8, kuna kipindi nyuma alinichek alikuja dar kutembea ila hatukuonana m, daah tunamind kichizi me na dogo wa usafi aliesababisha mchongo. 🤣🤣 on a serious note, me nishampuuzia aisee
 
Mmenitonesha kidonda mwanangu Mirambo milioni 29 uliipeleka wapi? Leo upo kwangu unanipa IDEA za kipumbavu eti bro unajua hutu tubiashara twa kuuza mafuta ya vibaba na nyanya chungu tunalipa watu hawajui tu .Sijui ndio umedata mwanangu.Sema sio case utaishi mdogo wangu .Simu ni moja tu tukutane benki.
 
Pole sana mkuu, kitu nilichojifunza kwenye haya nikujifunza kujipenda mwenyewe Kwanza. Iwe mke, mtoto, Ndugu, rafiki, mchumba wapende Ila jipende mwenyewe Kwanza . Hata ikitokea Hali kama hiyo hutaumia Kwa kiasi kikubwa Bali utachukulia ndio maisha Kwa sababu wewe binafsi ndio furaha yako ya Kwanza.


Usaliti upo na umetuzunguka katika Jamii hili lazima ulitambue

Huyo ni rafiki, kuna MTU kazaa mtoto kamlea, kamsomesha na Leo ni MTU mwenye maisha yake na Hana mpango na wazazi wake utaweza kuvaa viatu vya hao wazazi?

Kuwa na Tabia ya kupuuzia Mambo kama amekuona wewe wa nini na wewe muone WA kazi gani! Jeuri rafiki yake ni kiburi . Endelea na Mishe zako za kutafuta ridhki achana nae.

Usijipe umuhimu kwenye maisha ya watu, jipe umuhimu Kwanza wewe.
 
Mwanaume mwenzako anakutenga unalalamika, Vijana wa siku hizi sisi dah! sasa ukitengwa na Ukoo kama mimi?
Balaa, Kuna mzee mmoja alitengwa na ukoo, halafu katika huo mtaa wanaishi watu wa ukoo wake tuu karibu familia( 200) wote ni ukoo wake, mzee anafanya baishara zake hapo kwenye mtaa, sasa ukoo ulivyomtenga wakawaambia wanaukoo wote hakuna kununua kitu kwa mzee huyu kuanzia sasa, Yule mzee alifunga biashara maana hakuna mtu wa kununua bidhaa yake tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesema alikuwa na wapenz wawili wa kwanza siyo mwongeaji na wa pili muongeaji....kutokana na uongeaji na pesa pia wa pili akamzidi kete wa kwanza Ivo akafanikiwa kumtoa bikra Jay,siku ya siku ikafika wa kwanza kakaza anataka game akapewa na akakuta alichoambiwa anacho Jay hakipo tena....Ivo Mshikaji akakasirika ikawa kama amesusa Fulani....Jay hakupata pressure sana coz wa pili ndo anaemweka mjini.....mwisho wa siku akapata mimba akiwa mwaka wa 3....mimba akaniambia ni ya mpenz wa kwanza(asiye na Hela na siyo mwongeaji) na hata Ivo huyu mwenyehela alipoambiwa Nina mimba akakimbia(japo mimba ni kweli haikuwa yake maana yule aliyekuta bikra imetolewa mbali na kususa mzigo but Kuna time nyege zikimjaa alikuwa anakula mzigo kimtindo afu ndo tuhuma za ujauzito zikamwangukia)...
Mshikaji asiyenazo alikuwa Hana shida akakubali....ila changamoto ikawa namna ya kumtunza Binti na mimba yake(mwanzoni alikuwa hadaiwi matumizi kwa kuwa alikuwa haombwi,Jay si alikuwa anapewa na yule mwingine)....so majukumu yakamwelemea yule kaka,Ivo Jay Kwa kuwa alizoea kutunzwa vyema akatafuta mchepuko mwingine hapohapo chuo,huo mchepuko ukawa unahudumia ila ndo ukawa hautaki Jay awe na mpenz mwingine....
Sasa utamfukuzaje huyo uliyemkuta ...ndo jamaa akaamua kuitumia mbinu ambayo alimficha Jay....Kila wakikutana kusex,jamaa alikuwa anapenda wajirekodi na Jay pasipo kufikiri akawa anakubali....mwisho wa siku yule jamaa akamtumia pictures na video yule Shem(mwenye Ile mimba) .....Shem akamtumia watu wa Karibu na Jay Ili akimkataa Jay kuwe na uthibitisho.....Nadhan hicho ndicho kilichomkimbiza Jay maishani mwangu....Kwa Ile aibu hakutaka kuniona Tena.Japo nilisikia alidisco,akafanya Tena mitihani akafaulu na sasa ni mwalimu songea [emoji26][emoji120]

Mtafute mweleze hiyo ni kawaida.

Kwani si alikuwa anakuambia kuhusu wapenzi wake 2. Alikukimbia kwasababu gani sasa?
 
Wakuu habari za wakati huu! Nina Imani mu wazima wa afya na mnaendelea kupambana na maisha ya Kila siku. Mungu atusaidie sana.

Kama ambavyo title inajieleza, Mimi ni mtu ambae sina marafiki wengi, si kwakuwa ninajiskia sana, hapana ila ni aina ya watu ambao ninaweza kusema ni introvert. Nina marafiki wachache tu ambao nina amani sana kuwa nao.

Sasa kuna mmoja ambae ndio mtu wa karibu zaidi, jambo lake ni langu na langu ni lake, tumesaidizana kwenye nyakati ngumu na hatukuwahi kutengana kote tulikopita kama marafiki. Hatuna maisha mazuri kwakuwa bado ni vijana na tunapambana kutafuta angalau siku moja tuwe kwenye nafasi nzuri pia kimaisha.

Sasa changamoto imekuja kuonekana baada ya huyu mwenzangu kuwa amebahatika kupata chaka sehemu, yaani imekuwa si yeye ninaemfahamu tena. Kwa ukaribu wangu na yeye sidhani hata kama ni kubanana inaweza kuwa kwa mwenendo huu anaouonyesha.

Imekuwa ni mara chache sana siku hizi kuonana tena involuntarily ingawa najua yupo, na baadhi ya watu anakutana nao anapokuwa nje ya majukumu yake ila si mimi tena. Unaweza kumtumia ujumbe usijibiwe kabisa na tangu aanze kazi nakumbuka alinitumia ujumbe siku mbili tu za kwanza tangu alipoanza kazi.

Kiufupi sijapendezwa na mwenendo huo, muda mwingine asiponijibu ujumbe au simu yangu najisikia unyonge sana. Najiona kama nimepoteza nafasi kama rafiki kwake kutokana na aidha anahisi ntamlilia shida au sina msaada tena kwake. Silaumu yeye kupata kazi sababu mwisho wa siku haya ni maisha, tunatakiwa kukua kuelekea hatua nyingine. Mwenzangu katangulia ilhali wakati wangu wa milango kufunguka Bado..

It pains, kwa nyakati tulizifanikiwa kukutana tangu apate kazi anaonyesha kabisa he doesn't care about me and not interested with me anymore,, even jokes we used to make Hana response nazo kabisa. Mnaweza kuwa kwenye maongezi ghafla tu utaiskia anasema nataka niende kwa akina flani, like he's escaping me. Nimeamua kuacha kumtafuta pia sababu nishakuwa inferior kwa jinsi asivyojali tena kuhusu Mimi.

Ndipo nimepata kujifunza kuwa vitu vidogo sana huua urafiki.Si kwamba nahitaji pesa Toka kwake, it's all about value of friendship (THAMANI YA URAFIKI), Sawa naweza kukwama nikahitaji msaada kwake kama kawaida lakini si kudepend moja kwa moja kwenye kile alichonacho. Mara nyingi tu nimemshika mkono kipindi mambo yangu yanakwenda sawa, nimenusuru mahusiano yake zaidi ya mara moja, nimemvusha kifedha kipindi Mwanamke wake kalazimisha kuja ilhali hakuwa na pesa, nilimkabidhi sehemu ninayokaa Ili aenjoy na Mwanamke wake as a best friend of me. Treatment nayoipata sasa ndio inayoninyima furaha, sitegemei kama atajali tena lolote kati yangu naye. Nadhani kakutana na watu wapya, wa category yake ndio maana imekuwa hivi.

Anyway, Mi bado muangaikaji ambae siijui kesho yangu inakucha vipi ila naamini Mungu atanionyesha mlango pia. Tusiwapuuze watu tunaokuwa nao kwenye kipindi kigumu pindi tunapofunguliwa njia za mafanikio. Japo kuna ubize lakini si mbaya tukajuliana Hali tu..

Asanteni wakuu🙏, dondosha pia kisa chako
Nilishawahi kukimbiwa na rafiki* niliomchukulia kama mdogo wangu) nilikuwa nimeachana na mme, sina income, sina savings, nimehamia sehemu mpya. Nilikuwa sijui mwisho wa mwezi bills nazilipaje.
 
Mmenitonesha kidonda mwanangu Mirambo milioni 29 uliipeleka wapi? Leo upo kwangu unanipa IDEA za kipumbavu eti bro unajua hutu tubiashara twa kuuza mafuta ya vibaba na nyanya chungu tunalipa watu hawajui tu .Sijui ndio umedata mwanangu.Sema sio case utaishi mdogo wangu .Simu ni moja tu tukutane benki.
Ya kweli hii?
 
Mtafute mweleze hiyo ni kawaida.

Kwani si alikuwa anakuambia kuhusu wapenzi wake 2. Alikukimbia kwasababu gani sasa?
Eti Kwa sababu nilitumiwa nione video za uchi anavyosex na mchepuko mwingine....Ivo wote tulioona tukio hatutaki maishani mwake
 
kuna Rafiki angu alikuwa anafanya kazi kampun moja ya vipodozi yeye kama maneger wa.ile kampuni kwa hiyo magari yao yalikuw yanaenda mikoani yeye alikuwq anawapa mizgo na hesabu zote anafunga yeye. dahha Jamaa alianza kubadilika.ukimtumia sms hakujibu na anajibu baada ya week moja mbeleee ,alikuwa anajua unataka msaada wake hadi nikaacha sikumtafutaga tena hadi leo....
 
Back
Top Bottom