Ulisifika Kwa Lipi Shuleni....

Daah... arra yule jamaa aseeh alipotea mapema.

Hiyo ishu ilikuwa noma
Yeah....

Kuna kipindi walinunua mfuko wa kg 50 za sukari na mkopo Nido .

Member wa chai wote tulihamia kwao.... Tatizo daby ulikuwa Mzee wa misuli saana hizo mambo zilikupita
 
Sipatii picha hizo bakora [emoji3][emoji3]
 
Bado unatabia ya kuiba?
 
Bado unatabia ya kuiba?
Hapana, wizi wangu ulikua ni madaftari tu maana nilikua mvivu wa kuandika notes na mtu ukimuomba daftari ukasome anauliza kwa nini hukuandika notes, sasa kuepuka usumbufu wa kuulizana nilikua naiba daftari.

Baada ya kumaliza shule na hayo yakaishia hapo hapo. Huo wizi ulikua shule ya msingi na sekondari ya kawaida, nilipoenda kidato cha tano hakukua na haja ya kuiba madaftari maana hakukua na haja ya kuandika sana zaidi ya kusoma vitabu na vijitabu vya waalimu wa tuition.
 
Hujawahi kustukiwa?
 
Nidhamu ya uoga iliyo tukuka. form 1 mpka 4 bila kuchapwa bakora hata moja na shule ya bweni ya serikali enzi hizo 90's
 
πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
 
Mtu mwenye surname/jina la ukoo linalo chekesha kuliko wote, wakati wa kuitwa majina darasani ikifika zamu yangu lazima watu wacheke

Ila nilikuwa nawakomesha kila mwisho wa term wananipigia mokofi kwa kuwaburuza

Listi ya watu wenye Fujo nipo, team ya mpira wa miguu nipo, team ya basketball nipo, kwenye riadha nipo halafu mwisho wa term ni wa kwanza au wapili.
 

Ufupi aloo.

Nilikuwa mfupi mpaka wakawa wananiita Mrefu. Chaaa!
 
Walikua wananiita opong weah maana nilikua naingia nazo nyavuni zile K za kijijin kama sina akili ..jioni kwenye bondo natoa maziwa niliopewa na wameru daah aisee
 
ujanja ujanja tokea primary mpaka chuo kikuu,hii ni kutokana na muonekano wa sura yangu,ongeaji na ujuaji mwingi.
nilipokuwa chuo kikuu niliwahi kuingia chumba cha ma waalimu wakiwa zaidi ya 6,mwl moja akaniambie ujeu ww umekaa kiujanja janja sana hata mtu kuamini kitu filani juu yako si rahisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…