Ulitumia kiasi gani cha fedha ama umepanga kutumia kiasi gani cha fedha kugharamia harusi yako?

Hyo siku ya ndoa nikitoka kanisani(siku hyo hyo ya ibada) namchukua mtoto wa mtu namuweka ndani jioni tunapika ugali na mchemsho wa kuku wa kienyeji na wine 12k
Namuungia bundle la mwezi la 15k ili apost picha ambazo tumepiga kanisani...
nguo atavaa gauni lake analopenda mimi ntavaa kaunda yangu safi...
Gharama ntakua nimemaliza hapo.
 
Pete nilinunua zenye ppt ya dhahabu, kuogopa zisije kupauka.
Nakumbuka brother aliambiwa arudishe alipoulizwa umenunua Pete aina gani akasema Dhahabu bi mkubwa akaja juu akamwambia rudisha kachukue silver akarudi kuchukua silver ila hadi leo sijui kwanini alirudishwa
 
Huyo Mkeo/Bibi harusi mtarajiwa atakubali kuolewa bila sherehe?

Maana hapo ndipo Mtihani ulipo
 
Nakumbuka brother aliambiwa arudishe alipoulizwa umenunua Pete aina gani akasema Dhahabu bi mkubwa akaja juu akamwambia rudisha kachukue silver akarudi kuchukua silver ila hadi leo sijui kwanini alirudishwa
Huenda ilifanyika hivyo ili kupunguza gharama.

Lakini Pete ya dhahabu ina Faida zake ukiwa nayo, hata Siku ikitokea umekwama kabisa kiuchumi unaweza kuipeleka Kwa sonara ukapigwa zako hela kurudisha nusu hasara kama alivyoimba Stamina 😅
 
Harusi au sherehe yoyote ile ni PESAAAA kama huna pesa kaa kule kona ,tulia kama moja na kama huna pesa nenda Serikalini na mashahidi wako wa 3 funga ndoa na mchezo kwishaaa.
 
Harusi au sherehe yoyote ile ni PESAAAA kama huna pesa kaa kule kona ,tulia kama moja na kama huna pesa nenda Serikalini na mashahidi wako wa 3 funga ndoa na mchezo kwishaaa.
Umesema sahihi, ukiona huwezi kumudu gharama za harusi mnaweza Kufunga Ndoa yenu kimya kimya na mkamaliza mchezo.

Jambo la muhimu ni Ndoa tu, maana hayo mambo ya harusi ni ziada tu
 
Miezi 6 ya kuwakomalia ndugu na jamaa wakuchangie harusi, wakati huo huo unataka harusi ya shilingi milioni 20 halafu muhusika ana shilingi milioni 1 kama kianzio

Milioni 19 zote zinategemea wadau [emoji119]
Huo usumbufu ndio siupendi hata kama ni jambo la kijamii
 
Hizo gharama za kuwapeleka maharusi na waalikwa ShishiFood nani atagharamia?
Baba, mama, dada, kaka wa both sides, imeisha.....mashangazi sijui ndugu matembele waende wanakwenda. Hii budget mtu hawezi kukosa, la sivyo asioe..!!!
 
Baba, mama, dada, kaka wa both sides, imeisha.....mashangazi sijui ndugu matembele waende wanakwenda. Hii budget mtu hawezi kukosa, la sivyo asioe..!!!
Upo vizuri kwenye Bajeti

Vipi una Upare ndani yako ama ulienda short course Uingereza 😜

Kwa maana hiyo race wako vizuri sana kwenye kupanga bajeti 🙌
 
Huo usumbufu ndio siupendi hata kama ni jambo la kijamii
Mimi pia sipendi aisee huo usumbufu, ni vile tunaishi kwenye jamii ya watu wengi ambao wanadhani michango ya harusi ni haki yako kuchangia ukishapewa Kadi zao za michango ya harusi 🙌

Vinginevyo utanuniwa balaa
 
Upo vizuri kwenye Bajeti

Vipi una Upare ndani yako ama ulienda short course Uingereza 😜

Kwa maana hiyo race wako vizuri sana kwenye kupanga bajeti 🙌
Umejuaje babu, hapa ni kutonga na bajeti du, ombehiyoko
 
Idea nzuri...na maisha yanaendelea
 
Umejuaje babu, hapa ni kutonga na bajeti du, ombehiyoko
Kwahiyo umeamua kusisitiza ulichoongea Kwa Kipare?

Ngoja nimwite Mjukuu wangu Atoto aje anisaidie kutafsiri hicho Kipare

By the way, Bajeti ni muhimu. Vinginevyo baada ya harusi Mume anaweza kuanza kutembea huku akiongea pekeyake kutokana na stress za madeni
 
Mi nilishasema nataka ndoa ya watu nane tu,ndugu wanne upande wangu na wanne upande wa mume
Hiyo imekaa vizuri, changamoto utanuniwa na ndugu ambao hautakuwa umewaalika kushiriki hiyo harusi yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…