Uliwezaje kutongoza kwa mara ya kwanza?

Uliwezaje kutongoza kwa mara ya kwanza?

Nilijing'atang'ata vibaya sana nna uhakika kabisa yule binti hakuelewa nilichokua naongea japo alikua ameshakula sana mandazi yangu. Mbaya zaidi kesho yake nikakutana nae yuko na li broo limoja huni kweli nahisi tu lilikua linaenda kummega nili mind balaa nikampiga chini kabla hata hajanikubalia.
 
Usiku unapanga mashairi ya kuimbisha demu, pakikucha ukimuona mlengwa yote uliyopanga yanayeyuka unaongea mengine yasiyohusiana kabisa na mtongozo[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nlitumia njia ya barua lakn bado kweny kumpa ikawa kasheshe. Kila nkimuona nahisi kuna neno litamkera naamua kuirarua naenda hom kupanga mashambulizi upya

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Habari za wakati huu

Nimeona nilete mada muhimu kama hii mezani kwani kutongoza ni point muhimu sana iwe kwa mwanaume na hata kwa mwanamke japo ni nadra kusikia mwanamke katongoza na wanaume wengi tunawachukulia wanawake wanaotutongoza kama ni wameshindikana ila ukweli hauko hivo kwani mapenzi hayana mwenywe kila mtu anaweza kamatika.
kwahiyo hebu jarib kushea na wana jukwaa siku ya kwanza unatongoza ilikuwaje.
je uliona aibu au ulikuwa jasiri?
karibuni kwa mawazo.
Da aisee unanikumbusha mbali sana miaka ya 95 hivi nilianza tabia mbaya ya kutongoza kwa kuandika barua za mapenzi kwa mwanafunzi mwenzangu, mwingine nilimtumia dada fulani jirani na home kwetu akaenda kunitongozoea na nikapewa majibu murua mie nikamalizia tu na kupewa gemu
 
Aiseee sisi madomo zege tunazungukaga saaana.....
Unamuonesha msichana kuwa unampenda yeye ndo aaamue....

Siku moja ingawa haikuwa ya kwanza kwa kweli hii miguu siyo ya kuiamini saaana...inaweza kukuumbua hahaaaaa...ilikuwa inagongana hatari
[emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Nilijing'atang'ata vibaya sana nna uhakika kabisa yule binti hakuelewa nilichokua naongea japo alikua ameshakula sana mandazi yangu. Mbaya zaidi kesho yake nikakutana nae yuko na li broo limoja huni kweli nahisi tu lilikua linaenda kummega nili mind balaa nikampiga chini kabla hata hajanikubalia.
[emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji117][emoji117]
 
Nakumbuka kuna demu alikuja gheto,
Nikaishia kuweka nyimbo za video za Tabu Ley ,na Mbili Abel.

Sikuambulia kitu.[emoji3][emoji3],
Domo zege Ulimi kilo 2.
 
Nilichambwa mbele ya rafiki zangu niliabika mimi,niliaibika sana!.
Sikia tu mtoto wakike amesimama mbele yako,mguu mmoja mbele, kiunoni kajivika kanga kana kwamba anataka kukata mauno! Halafu ananesanesa halooo!! Lile neno la "UNIKOME" nilikuwa nalisikia kuanzia kiambishi awali cha Kati na kiambishi tamati!,mzizi wa neno,na ndipo nilijua hilo neno ni sentensi ya kujitegemea na iliyijitosheleza!.
Nilikuwa mnyonge kama nimemwagiwa maji!.. kitoto cha watu kimefura,ule mtaa niliacha kwenda kwa wiki kadhaa.😂
Ulizingua man" ile UNIKOME"wenyeji huwa tunastukiza Kofi la USO"
 
Back
Top Bottom