Uliza swali lolote linalohusu taaluma au nafasi za taaluma (academic positions)

Uliza swali lolote linalohusu taaluma au nafasi za taaluma (academic positions)

Kwanza Binti anataka kusoma kitu gani? Au anatamani kufanya nini baadae?

Lakini, kama akitaka kusoma field ya science au engineering, basi inabidi aanzie Certificate maana naona Maths ana F, sijajua kama utaratibu umebadilika.

kwa sasa, ni vizuri kumuuliza anachotaka kusoma ili iwe rahisi kujua hatua zinazofuata, maana kuna fields za kusoma zaidi ya 100 na zinatofautiana vigezo.

Mwambie asijisikie vibaya kwakuwa amepata Four ya 28, kuna njia nyingi sana kupitia NACTE ili kufikia malengo aliyojiwekea, kuna watu wengi makazini walipiga Four za mwisho, ila kupitia certificate na diploma sasa wapo kwenye nafasi za juu serikalini na sehemu binafsi.
Oops! Hajasoma kemia wala fizikia huyo ni arts pure, halafu hivyo nilivyoandika ni meseji niliyopokea kutoka kwake na nilipo muuliza vizuri ndipo akaniambia kwamba ameambiwa aingie humo (DIT, NIT na NACTE) ili kuangalia kozi zinazoendana na ufaulu wake na masomo yake
 
Eti kozi ya famasi Kwa shahada ipoje kuhusu soko lake.
 
Eti kozi ya famasi Kwa shahada ipoje kuhusu soko lake.

Moja ya Course yenye kuhitajika sana Tanzania ni Pharmacy, unaingia kwenye kila aina ya hospital kama pharmacist hapa Tanzania, TMDA kama mkaguzi wa madawa, na maduka mengi makubwa ya dawa kwa mujibu wa sheria inawataka kuajili pharmacist ikiwa mwenye duka hana taaluma hyo etc.

Ni moja ya course ambayo inahitajika sana, demand ya pharmacists ni kubwa Tanzania [emoji1241]. Kama una uwezo husijifikirie mara mbili nenda kasome.
 
Oops! Hajasoma kemia wala fizikia huyo ni arts pure, halafu hivyo nilivyoandika ni meseji niliyopokea kutoka kwake na nilipo muuliza vizuri ndipo akaniambia kwamba ameambiwa aingie humo (DIT, NIT na NACTE) ili kuangalia kozi zinazoendana na ufaulu wake na masomo yake

Ooh!, kwa ushauri wangu, kama amesoma pure arts, basi aende kusoma Diploma ya sheria (diploma in Law), at least hii anaweza kujiendeleza hadi school of Law na akapa muhuri wake na nakupiga pesa bila kujali changamoto za ajira, kwa course nyingine za arts atateseka sana baadae maana soko lake la ajira lipo tight mno, akisoma Law basi firms ni nying za kupractice.

Uzuri ordinary diploma in Law kwa ufauru wake anapata vizuri maana wanataka at least four (4) passes including English language. Moja ya vyuo vinavyotoa hyo hapa Dar, ni Tumaini University Dar es salaam college na etc….

I stand to be corrected.
 
Back
Top Bottom