Umaarufu wa 'Godzilla' baada ya Kifo!

Mkuu kuna mambo hubaki vile vile hata ufanye jitahada na juhudi zipi kuyabadilisha, mfano moja wapo ni hilo. ndio maana hakujawahi kuwepo Mtakatifu aliye hai. hapo ulipo hata ufanya jema na zuri lipi kuna watakao kupinga au kukukosoa. Cha msingi usisubiri shukrani au kusifiwa ukiwa hai. play your part and leave the word peaceful, thats all.
 
Haya malalamiko huwa yanashangaza mno.

Godzilla 'zizi' angekuwa wamemsahau asingekuwa anapewa hata interviews. Just week iliyopita alikuwa ametoa ngoma na ngoma haikuwa nzuri, ni kama ka-freestyle tu... Na freestyle haikuwa ile ya old zizi... Lakini pamoja na yote alipewa airtime ndefu na ya kutosha. Sio wiki hiyo tu, amekuwa akifanya interviews kibao , either studio au anafatwa. Coverage yake ilikuwa fresh tu, ukizingatia alikuwa hata hatoi ngoma kali tena. Nashindwa kuelewa huwa mnataka mtu a-support-iwe kwa namna gani.

Ukija kwa mashabiki, walikuwa wanamkumbuka ndo maana hata hapa JF kuna thread kibao za kujadili afya ya akili ya jamaa. Hiyo ni Love. Bila unafiki. Mnaolalamika ndo wanafki maana mlikuwa hamfuatilii wala kutilia maanani ishu zake ndo maana mnaona alikuwa ha-support-iwi.

Mi sidhani ni kirahisi kumuenzi kila mtu wakati akiwa hai. Huo muda watu hawawezi kuupata. Ndo maana support ya mara moja moja ni nzuri na imeuwa ikifanyika.

Kwa hiyo, kama alivyosema, Zellax!
 
Tatizo sio watu tatizo ni kifo chenyewe. Kifo kina tabia zake ambazo hazibadilishiki.
 
Mbona umesema maarufu kama ilikuwa hajulikani ? Fame without known can't be possible bro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…