Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Enzi hizo nafikiri 1984 Dr. Salim akiwa waziri mkuu alifanya ziara Lindi kama sijakosea na kukuta watu wakiwa wamevaa nguo chakavu ajabu ndio ikawa chanzo cha mitumba kuruhusiwa kuingia nchini.

Ulikuwa ukipatikana na Colgate, Imperial, Rexona au Lux Soaps au hata Lady gay Lotion toka Kenya ilikuwa kama umepatikana tu na meno ya tembo.

Hawa IMF/WB ukishakosana nao na kama hauna pengine pa kukopa ni lazima uwake tu, wanaobisha ni watoto wadogo wasiojua wapi tulikotoka, hawakupanga mawe mbele ya milango ya maduka ya RTC kushikia nafasi ya foleni ya kesho.
 
Kadangwa na kabudi eti ni mmbobezi wa sheria za kimataifa na kumfanya kuwa the chief negotiator. hahahhahahah una negotiate kwa kutumia sheria,

Akajifunze kwa President Trump & President xi, wote wameweka sheria pembeni.

Sasa sekta ya madini kaiua, uwekezajia sekta ya nishati (umeme kaua) anajifanya kujitutumia na kujenga bwawa mto rufiji eti kwa hela zake mwenyewe, mabwawa siku hizi wanajenga wachina nao kaisha watibua, Alianzia kwenye kilimo cha mbaazi akaharibu, akaenda kwenye korosho kaharibu, bila kujua yeye ndio tatizo fedha za kigeni haziingi nchini kaingilia mfumo wa biashara za fedha fedha, kote huko anadhurumu watu, sasa kaingilia sekta ya mawasiliano, akiivuruga na hii atajuta hamna rangi ataacha kuona
ugh!
 
Enzi hizo nafikiri 1984 Dr. Salim akiwa waziri mkuu alifanya ziara Lindi kama sijakosea na kukuta watu wakiwa wamevaa nguo chakavu ajabu ndio ikawa chanzo cha mitumba kuruhusiwa kuingia nchini.

Ulikuwa ukipatikana na Colgate, Imperial, Rexona au Lux Soaps au hata Lady gay Lotion toka Kenya ilikuwa kama umepatikana tu na meno ya tembo.

Hawa IMF/WB ukishakosana nao na kama hauna pengine pa kukopa ni lazima uwake tu, wanaobisha ni watoto wadogo wasiojua wapi tulikotoka, hawakupanga mawe mbele ya milango ya maduka ya RTC kushikia nafasi ya foleni ya kesho.
Mitumba ilianza kuingia Bongo kabla ya 1984; Kutokana na hali ilivyokuwa mbaya, White Fathers wa enzi zile walikuwa wakileta viroba vya nguzo za mitumba toka kwao Ulaya na kumwaga ktk Parish zao, at least bei ya mitumba hiyo ilikuwa tahafifu.
 
Mitumba ilianza kuingia Bongo kabla ya 1984; Kutokana na hali ilivyokuwa mbaya, White Fathers wa enzi zile walikuwa wakileta viroba vya nguzo za mitumba toka kwao Ulaya na kumwaga ktk Parish zao, at least bei ya mitumba hiyo ilikuwa tahafifu.
Kabla ya hapo ni mashirika ya kidini tu ndio walioruhusiwa kuingiza mitumba tena enzi hizo ikiitwa "Kafa Ulaya" na walikuwa wakigawa bure kwa waumini wao wenye uwezo mdogo kiuchumi.

Mitumba iliruhusiwa kuingizwa rasmi kibiashara 1984 baada ya Dr. Salim kumshauri Nyerere (Rip) ndio serikali ikaridhia kwani hali ilikuwa ni mbaya mno na viwanda vya nguo nchini viliishaanza kufa na hata kabla vilikuwa vikitengeneza nguo za kiwango cha chini mno mostly polyester.
 
Kabla ya hapo ni mashirika ya kidini tu ndio walioruhusiwa kuingiza mitumba tena enzi hizo ikiitwa "Kafa Ulaya" na walikuwa wakigawa bure kwa waumini wao wenye uwezo mdogo kiuchumi.

Mitumba iliruhusiwa kuingizwa rasmi kibiashara 1984 baada ya Dr. Salim kumshauri Nyerere (Rip) ndio serikali ikaridhia kwani hali ilikuwa ni mbaya mno na viwanda vya nguo nchini viliishaanza kufa na hata kabla vilikuwa vikitengeneza nguo za kiwango cha chini mno mostly polyester.
Asante mkuu Nyanjomigire!
 
Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.
Bahati nzuri hukusombwa kwenda Gezaulole enzi hizo, au sio?

Ni 'context' mkuu, ya wakati huo na wakati huu. Wakati huo palikuwepo na "Principle' iliyokuwa inasimamiwi na ilieleweka.

Wakati huu sijui tunachosimamia hasa, au wewe unakijua? Mimi sijaelezwa kinagaubaga nikaelewa, mbali ya kusikia tu kuwa kuna watu "wanyonge".

Ndio, mambo yalikuwa magumu kweli, na yakachagizwa na hao watendaji, hao akina mgambo na wao kuweka ya kwao kama ulivyoyaeleza. Hilo halikuwa lengo, na nashukuru kwamba hukuhusisha yaliyosimamiwa na hayo machafu yaliyojitokeza.

Sasa, siku baada ya siku tulitoka huko na hao jamaa IMF na WB wakaja na ya kwao aliyoyakataa Mwalimu kwa 'principle.'
Wakaleta "Structural Adjustment Programme", unaikumbuka?

Huenda siku moja utakuwa na mda wa kuielezea vizuri ili na wengine tujue ilikotupeleka.

Mambo mengi sana yalikuwa yanatokea wakati ule duniani kote, hata ndugu zetu waliokuwa na nafuu kidogo na wao
wanakumbuka hali hiyo ya mtikisiko. Kenya hadi leo wanamlaani Moi kuwalisha "Yanga" kama farasi! Ethiopia, miaka michache baadae wakaimbiwa "Do They Know It's Chistmas?"

Tushukuru mkuu, tulipita, hata kama ilikuwa ni kwa mbinde; lakini 'Principle' zetu zilibaki 'intact'. Sasa sijui kama katika hili tutakubaliana.

Kwa bahati nzuri, mada zako ni za kufikirisha sana bila la maudhi Allen Kilewella.
 
Acheni masihara tuombe tu Mungu tusiingie kwenye huu mtego maana uchumi utarudi nyuma kwa speed ya light,, na kuja kuwa stable itatuchukua mda sana.

Mungu atuepushe tu na huu mtego wa hawa mabeberu,,
Hakuna mtego wowote tunaowekewa sisi, bali mtego tunajiwekea wenyewe kwa sababu zisizoelezwa. Mbona juzi tu waliwekeana saini na WB kupewa zaidi ya dola bilioni (ndio, bilioni na sio milioni)?

Watu mnapenda sana kuchanganya mambo yenu kwa sababu zisizojulikana!
 
Ndiyo maana watoto wakiwa wanaropoka kwamba maisha enzi za mwalimu yalikuwa mazuri, huwa nawasikiliza tuu kisha nakaa kimya tuu.

Enzi za mwalimu nyerere, mtu akitoka Kinshasa au Bujumbura mnamuona kama ambavyo leo vijana mnavyomuona mtu aliyetoka New York. Mtaa mzima mnamzungumzia yeye.
 
Kwahiyo IMF na World Bank wakisema kitu inabidi tukubali na kufuata hata kama sio kweli au hatukubaliani nacho.
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
 
Bahati nzuri hukusombwa kwenda Gezaulole enzi hizo, au sio?

Ni 'context' mkuu, ya wakati huo na wakati huu. Wakati huo palikuwepo na "Principle' iliyokuwa inasimamiwi na ilieleweka.

Wakati huu sijui tunachosimamia hasa, au wewe unakijua? Mimi sijaelezwa kinagaubaga nikaelewa, mbali ya kusikia tu kuwa kuna watu "wanyonge".

Ndio, mambo yalikuwa magumu kweli, na yakachagizwa na hao watendaji, hao akina mgambo na wao kuweka ya kwao kama ulivyoyaeleza. Hilo halikuwa lengo, na nashukuru kwamba hukuhusisha yaliyosimamiwa na hayo machafu yaliyojitokeza.

Sasa, siku baada ya siku tulitoka huko na hao jamaa IMF na WB wakaja na ya kwao aliyoyakataa Mwalimu kwa 'principle.'
Wakaleta "Structural Adjustment Programme", unaikumbuka?

Huenda siku moja utakuwa na mda wa kuielezea vizuri ili na wengine tujue ilikotupeleka.

Mambo mengi sana yalikuwa yanatokea wakati ule duniani kote, hata ndugu zetu waliokuwa na nafuu kidogo na wao
wanakumbuka hali hiyo ya mtikisiko. Kenya hadi leo wanamlaani Moi kuwalisha "Yanga" kama farasi! Ethiopia, miaka michache baadae wakaimbiwa "Do They Know It's Chistmas?"

Tushukuru mkuu, tulipita, hata kama ilikuwa ni kwa mbinde; lakini 'Principle' zetu zilibaki 'intact'. Sasa sijui kama katika hili tutakubaliana.

Kwa bahati nzuri, mada zako ni za kufikirisha sana bila la maudhi Allen Kilewella.

Watu hawali principle mzee, watu wanahitaji mahitaji muhimu!
Hayo mambo ya Nyerere kujifanya mwanafalsafa, mwenye misimamo, eti isiyoyumba ilitusaidia nini sisi wakati wa njaa kali?
 
Back
Top Bottom