Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere aligoma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency ilikithiri kwenye mashirika na serikalini na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimika kuingia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
 
Mkuu usirahisishe kabisa,hii hali isikie kwa wenzio.Nina rafiki yangu yuko Nicarague,nao wanapitia hali kama hii,Ananiambia bank kwa siku hauruhusiwi kutoa zaidi ya dola 2 za kimarekani tena hapo ni counter kwa teller,Kwa ATM mashine haitoi zaidi ya dola 1 za kimarekani kwa siku.
1$= 2340.
 
Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere aligoma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency ilikithiri kwenye mashirika na serikalini na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimika kuingia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
Yaani mkuu story za humu, ndio maana wengine huwa hatuko serious nazo, tunajibu kwa mzaha tu.

Mtu unamuuliza kivipi ugomvi wa serikali na tasisi ya tathmini ya uchumi, ivuruge uchumi wa tz hana jibu!!!.

Report ya zitto imetoka, IMF wanaonyesha msimamo wao jinsi ulivyo hauna mchango wa moja kwa moja isipokuwa ni kama mshauri, watu tunaendelea kuhoji. Haya yote ni kwa maslahi ya taifa au maumivu ya mmoj mmoja!!!
 
Mtu unamuuliza kivipi ugomvi wa serikali na tasisi ya tathmini ya uchumi, ivuruge uchumi wa tz hana jibu!!!.
IMF ni taasisi ya kufanya tathimini ya Uchumi peke yake? Ndiyo maana swali lako halina majibu kwa maana halina msingi unaofanana na mada husika.
 
Kalamu1 umeandika vizuri sana kuhusu "Principle" na wengi wa kizazi hiki hawatakuelewa unamaanisha nini. Kuna wakati nawaza kama kwa jamii hii ya sasa ya watanzania kingetokea nini kama ile vita yetu na Uganda ingetokea zama hizi.

Kanuni maana yake ni lazima uwe na sababu za msingi za kukubali ama kukataa jambo. Kwa mfano Mwalimu alikuwa ni Mjamaa sasa baadhi ya masharti ya WB/IMF yalikuwa ni kinyume kabisa na falsafa yake ya Ujamaa. Leo tunagombana na IMF kwa kigezo gani cha kikanuni?

Lakini programu nyingi sana zilizoletwa na hao mabwana wakubwa zilikuwa haziendani na akili za sisi tulioletewa hizo programu ila zilikubaliwa ili mradi tu tukopeshwe ama tupewe misaada kwa miradi yetu wenyewe tuliyokuwa tunataka kuitekeleza.

Akiulizwa ni kwa nini anataka aliyekuwa Rais wa DRC wakati ule Laurent Kabila asilipe fedha zilizokopwa na Mobutu, lakini anaona sawa aliyekuwa Rais wakati hule Ally Hassani mwinyi alipe mikopo iliyokopwa na yeye, Mwalimu alijibu kwamba Mobutu alikopa kwa kuwatumia wakongo lakini fedha akatumia yeye binafsi wakati yeye Mwalimu alikopa kwa niaba ya watanzania na fedha akazitumia kwa watanzania. Hiyo ndiyo Kanuni.

Nisichoelewa ni kwa nini tunapanga kutekeleza miradi mikubwa sana kwa kutegemea fedha za mikopo na misaada toka kwa watu tunaowaona ni wanyonyaji wa uchumi wetu?
 
Hata Mugabe alikimbilia China yy ameishia wapi.
Kwa ujumla Zimbabwe nimekaa miaka 1995 ilikuwa ni Nchi ya mfano nenda leo nchi ambayo ilikuwa inatuletea misaada ya vyakula kama mahindi yaani kwa wale waliokula Ugali wa unga wa njano hili wanalijua Zimbabwa walianza kuleta misaada na kutusaidia mbegu za mahindi kutoka Zimbabwa.
Kwa hiyo china unayoisemea hakuna kitu zaidi kulimbikiza madeni zaidi
Ishu ambayo watu wengi wanashindwa kuelewa ni kuwa system nzima ya mfumo wa pesa hpa duniani inamilikiwa na wazungu kupitia world bank ndyo ukiwatibua tu! Wanakutoa kwenye system na hela yako inaporomoka thamani kwa kasi ya ajabu ndicho kilichowakuta zimbabwe na venezuela
 
Tatizo una changanya Mambo,
1.Nyakayi i.e. kipindi cha kutupa hela na kumiliki Mali e.g. TV

2.UJAMAA na MASHARTI YA MABEBERU, hata sasa wanataka USE SHOGA, je utakubali??? wana gawa kondomu, ili hali, nyenzo za umiliki Mali wana zishikiria, UNAPEWA ELIMU YA MATUMIZI na sio MATENGENEZO, e.g. simu, laptop n.k

n.b. JAMBO USILO LIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA, usimlaumu mwl, sema tu ALI SAILTIWA.....
Hujawahi kumuona shoga mtaani? Mpaka wabunge wapo. . Acheni propaganda.. Pogba afukuzwe magogoni.. Wengi wenu kizazi cha instagram hamjui shida
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Unfortunately, ndiko tunakoelekea. Ila sio IMF tu watakaosababisha hali hiyo. Chanzo kikubwa ni utawala mbovu uliopo unaoamini kuwa serikali inaweza kufanya biashara na ikapata faida.
 
Unfortunately, ndiko tunakoelekea. Ila sio IMF tu watakaosababisha hali hiyo. Chanzo kikubwa ni utawala mbovu uliopo unaoamini kuwa serikali inaweza kufanya biashara na ikapata faida.
IMF watolewe kabisa kwenye hili, maana hata uchumi ukikua huwa hawahusiki.
 
Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.
Umenikumbusha mbali sana. Tumevaa sana hizo nguo shuleni. Kitambaa kilikuwa kikiitwa malekani. Na kwa sababu ya ukosefu wa vitenge na kanga, kina mama nao walivaa hizohizo malekani lakini zilizowekwa rangi za kienyeji nadhani, na wao wakaziita kamanyora. Ilikuwa patashika. Ila vijana wa dotcom hawajui haya.
 
Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
Kilichotokea africa ndicho kilichotokea amerika ya kusini tht why today Tanzania tunamiliki only 4% ya madini asilimia zilizobaki wanamiliki mabeberu
 
Hawa wazungu vitafunwa kweli yani ugombane na mtu mmoja utese mamilioni ya watu?
Ila msimu huu tuna chakujitetea kuwa kwa bahati mbaya tunae kichaa na tulichaguliwa hatukumchagua wenyewe.
 
Ishu ambayo watu wengi wanashindwa kuelewa ni kuwa system nzima ya mfumo wa pesa hpa duniani inamilikiwa na wazungu kupitia world bank ndyo ukiwatibua tu! Wanakutoa kwenye system na hela yako inaporomoka thamani kwa kasi ya ajabu ndicho kilichowakuta zimbabwe na venezuela
Hii ya kweli kabisa kwani hawa Watu sio wa kubeza kumbuka kila kitu wao wanapanga bei ss tukilima huku wao wanatupangia bei.
Sasa watu kama hawa huwezi kubishana nao kwani wao wanaamuzi yote hata ya kiutawala wakiamua kumweka Mtu wao wanamweka
 
Kweli njaa kipimo cha akili
Miaka hiyo ya 83-84 kule vijijini hali ilikuwa mbaya mno bora ya DAR kidogo nakumbuka mwaka 88 sukari ilikuwa hadimu kwelikweli ambapo wazazi wetu walikuwa wananunua zile pipi za rangi zinasagwa na zinatumiwa kama sukari kwenye chai....
 
Sidhani kuwa yote hayo yalitokana na ugomvi wa mwalimu na IMF, siyo kweli...Hayo yote yalitokana vita kati ya Tanzania na Uganda...kumbuka kabla ya vita maisha yalikuwa mazuri kabisa...Dola moja ya marekani ilkuwa kati ya sh. 5 hadi sh. 7 kama sijakosea...lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya vita...uchumi ukawa mbaya ...ikabidi tujitumbukize baadaye kusaini mkataba na IMF wakati wa Mwinyi..Nyerere alioma kusaini mkataba huo...Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency na kadhalika na kadhalika....Nchi karibu zote za Afrika zikalazimikakuinia mkataba na IMF...lakini mikataba hiyo na IMF ilileta balaa...huko Nigeria watu karibu 200 walikufa katika maandamano kupinga mabadiliko ya kiuchumi kutokana na masharti ya IMF..Zambia pia kulikuwa na maandamano pia Uganda, Algeria na kadhalika...
Nadhani umejichanganya kidogo.Badaa ya Mwinyi kukubali masharti ya IMF ndipo tulipoanza kupata unafuu kama taifa. Bidhaa zilianza kufurika madukani, nguo aina ya malekani na kamanyora zikaanza kutoweka (baada ya kuingiza nguo kutoka China, Japani, India na mitumba kutoka Ulaya). Nakumbuka akina mama walianza kuvaa kanga za China, Japani na India. Kiujumla hali ilibadilika kuwa nafuu kuanzia kipindi hicho.
 
Back
Top Bottom