Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Sidhani kama kuna tatizo linalohusiana na watokako. Tatizo mmoja anataka kumuiga mwingine. Kama alikosea na yeye pia atakosea.
Soma history ya mkoloni kwann jamii zingine aliona ni hasara kuzipa elimu,jamii inayoamini matumizi ya nguvu kuliko akili aliitumia kwenye Kazi za mashambani na ukuli bandarini sasa usipojua history ukachanganya vitu hivi ni lzm yaharibike mambo.We uoni hio jamii si wazuri kwenye reasoning Bali kwenye nguvu.Uongozi ni hekima na busara ukitumia mechanical ni lzm GARI litafail tu.
 
Kaka umenikumbusha mbali sana 1983, babubyangu alikuwa na uwezo vijijini, basinkukiwa na MTU Mwenye mgonjwa watu wanakuja home kukopa fedha, kuomba sukari kwa ajikivya uji wa mgonjwa HD nikaamini uji+sukari ni Dawa. Siku ya noeli Misa ya USIKU anakuja KATEKISTA kuazima taa ili ikamulike KANISANI.
Ilipofika chrimas, babu akienda Mjini Songea akaja na kaptura ya shule Rangi ya kaki, wengine wakiita stapoti. Basi nikitinga church nimekaa MBELE kabisa, nikawa natokatoka Mara kwa Mara ili niwakoge wenzangu, nikifunika sana. Baada ya Misa nikawa na senti sumni(50) Ikiwa na pichurevya Sungura nilinunua vitu balaa kuanzia mishkaki ya kitimoto, mangatundu, ubende, bangia na maandazi, ila Nilikuta mchoyo sana. Shida ikaja January 1984 naenda kuandikishwa shule mkono ulikuwa mfupi nikashindwa andikishwa kwa kuwa sikushika sikio. Basi sale Zangu nitaendelea kushine siku za jumapili tu.
Sikujua SHIDA zile zilitokana na nini. 1985 baba akajanichukua ni kaanza shule town.
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hhahaaaaaa, eti MTU anatumbuliwa watu wanashangilia, then anasamehewa wanashangilia!! Hivyo yaani hatueleweki ( mazamwamwa)
Nadhani siku ule moto wa kuzimu ukiwekwa makumbusho na tutakapoacha tumia alama ya twiga ( upole conspiracy) na kuacha kula ugali wa mahindi ( chakula cha ng'ombe) ndio tutakuwa na akili.Watu wamekufa akili thus ni mtaji kwa wachumia tumbo. MTU anatumbuliwa wakashangilia baada ya dakika moja anasamehewa wakashangilia tena,je utasema hawa watu wanakili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ikulu sio uwanja wa majaribio, awamu ya kwanza na ya tano zote ni awamu za mapinduzi, lazima kuwepo maumivu.
Mapinduzi gani export ya. Bidhaa imeshuka 50% direct foreign Investment down. By 60% biashara zinafungwa haya ndio mapinduzi kwa uelewa wako
 
Ikulu sio uwanja wa majaribio, awamu ya kwanza na ya tano zote ni awamu za mapinduzi, lazima kuwepo maumivu.
Mapinduzi gani export ya. Bidhaa imeshuka 50% direct foreign Investment down. By 60% biashara zinafungwa haya ndio mapinduzi kwa uelewa wako
 
Ndio maana nakuambia hakuna kisishowezekana mkuu.
Huyu mtu asipodhibitiwa atatufikisha huko.
Yani njia anayopita jiwe Zimbabwe ilipita humohumo naomba mungu mwisho wa Safari tusifike ilikofika Zimbabwe
 
Kaka umenikumbusha mbali sana 1983, babubyangu alikuwa na uwezo vijijini, basinkukiwa na MTU Mwenye mgonjwa watu wanakuja home kukopa fedha, kuomba sukari kwa ajikivya uji wa mgonjwa HD nikaamini uji+sukari ni Dawa. Siku ya noeli Misa ya USIKU anakuja KATEKISTA kuazima taa ili ikamulike KANISANI.
Ilipofika chrimas, babu akienda Mjini Songea akaja na kaptura ya shule Rangi ya kaki, wengine wakiita stapoti. Basi nikitinga church nimekaa MBELE kabisa, nikawa natokatoka Mara kwa Mara ili niwakoge wenzangu, nikifunika sana. Baada ya Misa nikawa na senti sumni(50) Ikiwa na pichurevya Sungura nilinunua vitu balaa kuanzia mishkaki ya kitimoto, mangatundu, ubende, bangia na maandazi, ila Nilikuta mchoyo sana. Shida ikaja January 1984 naenda kuandikishwa shule mkono ulikuwa mfupi nikashindwa andikishwa kwa kuwa sikushika sikio. Basi sale Zangu nitaendelea kushine siku za jumapili tu.
Sikujua SHIDA zile zilitokana na nini. 1985 baba akajanichukua ni kaanza shule town.

Sent using Jamii Forums mobile app

Siku zile mtu akitoka Burundi tuu, alikuwa anaonekana kama ametoka marekani kwa sasa. Zanzibar kulikuwa na maisha poa kabisa. Unguja ndiyo ilikuwa Dubai yetu.
 
Hao wenye uchumi mkubwa kwa sasa wanalia hali ngumu ya uchumi sembuse huku Africa.

US wanatarajia vifo laki mbili ndani ya mwezi mmoja ujao, ni shida za dunia nzima.

Biashara za kimataifa zimefungwa kila kona ya dunia.

Kama corona imekuja kiasili (nature) basi hatuna ujanja lakini kama imetengenezwa na watu fulani basi wakamatwe nawote wapigwe risasi.
 
Back
Top Bottom