tinkanyarwele
JF-Expert Member
- Dec 30, 2016
- 2,016
- 1,946
Aaaah vijana wana mambo, hiv wote tukiamua tusijenge nyumba za kuishi itakuwaje? Usiogope kujenga!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mjengo Manga (Ghorofa)Milioni 280?
It's okay..thank you[emoji120]
Kulipa kodi kwa mtu ni kumtajirisha.
Unaweza waachia wanao biashara zilizosimama. Wakazidi kuingiza kipato.Hata hao wahindi kwao wana nyumba wamejenga. Huwezi kuwa unaishi say Afrika Kusini ukafikiria kujenga huko. Utapanga na kufanya biashara au shughuli yoyote halali. Hii dhana ndio ipo kwa wahindi, hapa wahindi sio kwao. Kwa baadhi wenye fedha nyingi sana uwa wanajenga maeneo kama masaki, upanga n.k na wengi uwa wananunua apartment.
Halafu kujenga sio umasikini, kumiliki nyumba ni jambo bora sana katika maisha maana nyumba ni kitu ambacho kinakupa mengi sana ikiwepo kukupunguzia gharama za kodi, kukuondolea stress za kutokuwa na kwako na pia hata ukipata tatizo la kiuchumi unakuwa na pa kuanzia.
Nyumba ni kitu ambacho hata ukiondoka duniani ghafla familia yako inakuwa na sehemu ya kuanzia kuliko ukiwa huna nyumba.
Nyumba ni muhimu katika ukuaji wa miji na Taifa kwa ujumla. Unavyoona nje yale majengo ni kwamba watu wamewekeza ndio maana kunapendeza. Na sisi tujenge majengo kukuza nchi yetu. Tuachane na wahindi wale hapa sio kwao ndio maana hawajengi. Tena si wahindi tu hata wazungu hawajengi hapa kwa kuwa si kwao hapa watachuma tu ila kujenga wataenda jenga kwao
Watu wa mbele wapo flexible and mobile.Hii ni tofauti sana mzee. National housing nyumba bei nafuu(bora kupanga kuliko kujenga) mfano nchi zilizoendelea hakuna viwanja vya bei powa.
Hata hivyo sheria za ujenzi ni kali kuliko za Tanzania, yani huwezi kujenga bila kibali,bila ramani, bila mpango yan ukipiga hesabu ya ujenzi unaona bora ukapange. Tanzania kujenga ni nafuu kuliko kupanga, kupanga kero nyingi kuliko kuishi kwako. Bora kujenga kuliko kukuza biashara sababu pesa inaweza kufia huko na pesa ya pango ukakosa vile vile.
Kama unajifahamu una biashara ambayo ukitoa 400K kwa mwezi kwa ajili ya kodi inayumba, katafute nyumba ya 150K.Kodi ya nyumba ni kati ya vitu vinavyotafuna mtaji wa biashara kuliko maelezo..umepanga nyumba ya wastani ya laki nne kila mwezi. Kutoa kiasi hiki kama kodi ya nyumba toka kwenye pato la biashara ni pesa nyingi sana. Usipokuwa makini unaweza ukayumba hata kibiashara. Kumbuka bado biashara ina gharama zake za uendeshaji ikiwemo kodi ya ofisi, mishahara, etc.
Usipo kuwa makini utajikuta milioni inachomoka kila mwezi kwaajili ya kodi pekee.....haina afya kibiashara.
Kingine ni swala la kukopesheka na taasisi za fedha. Biashara haiwezi kusimama bila mikopo, na hakuna mkopo bila dhamana. Siku hizi hawapokei tena eneo lisiloendelezwa kama dhamana ya mkopo. Wanahitaji nyumba. Huna nyumba utatumia muda mwingi sana kusimama kibiashara.
Vijana jengeni....nyumba ni asset.
Mkuu hizo wizara zimehamishiwa huko moja kwa moja na wao mikataba yao ni permanent and pensionable terms hivyo watafanya kazi huko mpaka kustafu kwao hapo kwanini wasijenge tena huko kama uwezo unaruhusu?Wale mawizara waliohamia Dodoma toka Dar wakajenge nyingine Dodoma?
Lakini umesoma alichoandika mtoa mada soma tena umekurupuka vibaya.[emoji16][emoji16][emoji16]acha kupotosha watu sisi dar tuna nyumba zaidi ya 4 lakin upiga kwa mwaka hela tunayo chukua si chini ya milion 16 na nikufumbue katika biashara ambayo haina hasara ni nyumba ni bonge la biashara watu kila siku wanakuwa wanahitaji kuishi maisha yao hapo kwenye nyumba bado ujaja kwenye hustle zetu wenywe huku tumetulia tunajua nyumba zipo miezi ikifika hela zinaingia ila upate mpangaji mzuri anae lipa kodi kwa wakati siyo kichefu chefu wa kupiga calenda
According tu Kiyosaki sio? hiyo inabaki kuwa ni falsafa yake na wafuasi wake akiwemo mm ila kamwe haiwezi kuwa maana halisi ya asset au liabilityAssets: kitu kinachoingiza pesa mfukoni mwako mfano ardhi, shamba
liability:kitu kinachutoa pesa mfukoni kwako mfano nyumba ya kuishi gari la kutembelea ni liability
source: financial IQ kutoka kwa robert kiyosaki
Wachache sana wana elim hio, angalia wanavyobisha kwenye huu uzi,Babu zetu walijenga nyumba za kulala, baba zetu wamejenga nyumba za kulala na sisi tunaendelea kurithi akili ile ile, japo pamoja na kuona hali ngumu ya hao wazazi waliokuwa wanamiliki hizo nyumba bado tunakosa ubunifu. Huwezi sikia mtu anawaza kuanzisha kampuni au investment endelevu.
Yaani mtanzania akiugua mwaka Kwisha habari yake kwa sababu anategemea active income badala ya passive income. Ukiugua au ukafukuzwa kazi nyumba ya kulala itakulisha? Au utakuwa ombaomba.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Masikini ni watu pia, tuheshimiane tafadhali!
Kujenga pia ni kutajirisha mafundi na watu wa hardware... Jenga ila kama tayari umeridhishwa na kipato chako na tayari umri umeenda kidogo. Ninavyoona kama una chini ya miaka 35 hamna haja ya kutumia rasilimali kujenga na badala yake lenga kuwa na kipato kikubwa zaidiJe, ukilipa kodi ya nyumba inazalisha? Kama unapanga na inakugharimu ni bora kujenga na kuwa na nyumba na kutolipa kodi. Kulipa kodi kwa mtu ni kumtajirisha. inabidi kila mja awe na kwake yawe makazi bora au ya wastani kwako ni kwako.
Umejenga kwa kutumia milioni 30 hiyo ni milioni 30 imetoka kwenye mtaji wa biashara. Na huo mstari wa nyumba unayoishi ni asset umeoitwa na wakati. Tujifunze kuwa asset ni kitu kinachokuongezea thamani kila mwezi. Hiyo ndio maana halisi. Kama umejenga kwa pesa yako cash, bado nyumba unayoishi ina gharama za umeme, maji na maintainance. Ni liability na sio asset. Wale wenye mikopo ndio zaidi wana marejesho. Angalau aliejenga kwa ajili ya kupanfisha anaweza kusema nyumba yake ni assetKodi ya nyumba ni kati ya vitu vinavyotafuna mtaji wa biashara kuliko maelezo..umepanga nyumba ya wastani ya laki nne kila mwezi. Kutoa kiasi hiki kama kodi ya nyumba toka kwenye pato la biashara ni pesa nyingi sana. Usipokuwa makini unaweza ukayumba hata kibiashara. Kumbuka bado biashara ina gharama zake za uendeshaji ikiwemo kodi ya ofisi, mishahara, etc.
Usipo kuwa makini utajikuta milioni inachomoka kila mwezi kwaajili ya kodi pekee.....haina afya kibiashara.
Kingine ni swala la kukopesheka na taasisi za fedha. Biashara haiwezi kusimama bila mikopo, na hakuna mkopo bila dhamana. Siku hizi hawapokei tena eneo lisiloendelezwa kama dhamana ya mkopo. Wanahitaji nyumba. Huna nyumba utatumia muda mwingi sana kusimama kibiashara.
Vijana jengeni....nyumba ni asset.
Kizuri kichukue kibaya achana nacho. Wahindi ni katika watu wenye mafanikio makubwa katika kurithisha watoto wao mali zao tena na tena. Ni kwa sababu wanajua jinsi ya kuitumia pesa kuongeza ziwe zaidi bila anasa. Somo hilo litakufaa wewe na hata wanaokuja baada yakoKwahiyo wewe mbuzi, sisi tuache kuishi maisha yetu kama watu weusi "tuanze kukopi kila kitu, kila lifestyle ya Mhindi???