LadyRed
JF-Expert Member
- Mar 19, 2016
- 9,636
- 11,483
Tanzania nzima hatuwezi kaa Kariakoo na Posta mkuuAngalia wahindi muhind anapanga nyumba kariakoo juu mfano analipa laki mbili kwa mwezi duka lake liko chini hapo hapo anapoishi hana gharama za usafiri wala chakula cha mchana mswahili hataki kulipa pango.laki mbili anaona bora akajenge nyumba yake kimara awe anakuja kwenye duka lake lililoko kariakoo la kuuza nguo gharama za kuweka mafuta kwenye gari yake kila siku ni elfu 20 kwa mwezi anatumia laki sita !! Kula yeye na mkewe chakula mchana wanatumia elfu kumi wote wawili kula hotelini kwa mwezi wanatumia laki tatu muhindi anakula kwake .Hapo nani mjinga Kati ya muhindi anayepanga na mswahili anayekaa kwake kwenye bungalow lake kimara? Piga hesabu kwa miaka 40 ,nani atakuwa lofa hapo Kati ya muhindi na mswahili