Umati wa usaili UDOM: Tunahitaji mjadala wa Kitaifa kuhusu tatizo la ajira nchini

Umati wa usaili UDOM: Tunahitaji mjadala wa Kitaifa kuhusu tatizo la ajira nchini

Kilemakyaaro

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2016
Posts
5,051
Reaction score
5,104
Leo asubuhi nimemleta mtu hapa UDOM kuhudhuria Usaili wa kazi za Utumishi, hakika watu ni wengi. Binafsi nliyemleta ameitwa kwenye Usaili wa nafasi za National Audit, only 10 kama sio 20 nafasi lkn wameitwa watu sio chini ya 3400, yaani watu hao ndio wapatikane only 20 people. Kibaya zaidi wameitwa watu waliosoma Business Administration lkn wamefika wakaaambiwa hawana sifa.

Sasa unajiuliza kama hawakua na sifa waliwaita vipi? Hizo garama alizotumia kuja hapa Dodoma atalipwa na nani? Kuna dada kwa Mfano katokea Ifakara, anasema kaja kwa malori na kaingia Dodoma saa 8 za usiku then amekataliwa kufanya usaili eti kasoma Business Administration, kwakweli Inauma na inakera mnoo.

Kingine nnaomba kufaham ikiwa watu wa Utumishi wananufaika vip na hizi Interview maana haiingii akilini wanaohitajika kua 10 au 20 unaita watu 3600 kwenye usaili. Yaan hawana njia ya kuwachuja japo basi waitwe 100 ama 200 badala ya kuwapotezea muda hawa vijana tena ambao wengine nauli wamekopa?

Hili swala ni nyeti sana kwa mustakabali wa Taifa, hawa watu waiichoka nchi haiwez kua salama maana ukiangalia idadi ya wanaosaka ajira na nafasi zilizopo kuna shida mahala.

Mwisho niwaombee wanaosumbuka na hizi Interview Mungu Awape Subra
 
Website ya Ajira ni tatizo sana kwenye suala la kuajiri watu.

Kama taarifa inasema mtu awe amesomea Bachelor of Account wewe ukiwa na B.com yako au B.A yako hawakuchukui hats kama kwenye bachelor yako ulistick na Account.
 
Tupo hapa ukumbi wa Jakaya Kikwete Conference Centre

Tunajadili mabadiliko ya mtaala unaoweza kuandaa wahitimu kujiajili, kuajiliwa katika kukuza uchumi wa kati

Karibu tujadili

Let's be A Job creator rather than being the Job seeker
 
Unajua issue ni kwamba tume ya ajira wanakwepa lawama kwa hiyo inabidj wamuite kila ambae ame qualify minimum requirements za nafasi husika ambayo imetangazwa. Si unakumbuka zile enzi ambapo malalamiko yalikua makubwa sana kuwa taasisi na mashirika ya umma yanaajiri kwa kujuana na vimemo?

Hilo ndo likazaa tume ya ajira ambayo sasa ndo inaratibu michakato ya ajira kwa taasisi za uma kwa asilimia kubwa, sasa ili kuondoa au kupunguza hayo malalamiko, inabidi waite tu wote waliokidhi vigezo hata kama wako 10,000 na nafasi ziko 2 tu.

Maana fikiria, kama wametangaza nafasi halafu walio meet vigezo vilivyowekwa wako 2000, mnapunguzaje kupata 20 tu ambao ndo mtawaita interview wagombanie hizo nafasi 5 bila hao wengine 1980 ambao na wao wana minimum requirements zote zilizowekwa kulalamika kuwa ajira ni za kujuana?

Ndio maana wanaamua wawaite wote tuu hata kama wako 10,000 kila mmoja apambanie hizo nafasi 10 zilizopo.
 
Tupo hapa ukumbi wa Jakaya Kikwete Conference Centre

Tunajadili mabadiliko ya mtaala unaoweza kuandaa wahitimu kujiajili, kuajiliwa katika kukuza uchumi wa kati

Karibu tujadili

Let's be A Job creator rather than being the Job seeker

Cha kushangaza unaweza kukuta wote mliopo kwenye huo mjadala mmeajiriwa, na hakuna anayethubutu kwenda kujiajiri! Nchi hii kwa vituko ni hatari.
 
Hivi haiwezekani kudai fidia mahakamani maana kama hukuwa na sifa kwanini walikuita kwenye interview?nadhani aende mahakamani kudai fidia ili iwe fundisho
 
Ndio maana nilimuelewa vizuri SANA huyu jamaa

 
Hivi haiwezekani kudai fidia mahakamani maana kama hukuwa na sifa kwanini walikuita kwenye interview?nadhani aende mahakamani kudai fidia ili iwe fundisho

Gharama za kudai hiyo fidia zitazidi unachodai. Hii ndio Tanzania bana.
 
Vimemo havitaisha hata siku moja, nina rafiki yangu alipata mtu wa kumuungaisha tanroad mwaka jana huku wengine tukikimbizana kufanya app kabla ya deadline jamaa yeye ameshapigiwa simu anataka kufanya wilaya gani ktk nafasi hizo. Kwa hyo wakati mwngine hizo nafasi ni kuchosha watu na kuwapa gharama zisizo za lazima ikiwa tayarii wao wana watu wao.

Mimi nikiona kazi ya serikali inahitaji mtu mmoja wawili wala sijichoshi kuiomba.

Kuna tangazo lingin waliwahi kutoa sijui nafasi za nini beforw deadline watu washaitwa wakafanye interview wewe huku unakimbizana na gharama za posta na printing kumbe tayar wenzio washakaa kwenye interview tena one week before deadline
 
Tupo hapa ukumbi wa Jakaya Kikwete Conference Centre

Tunajadili mabadiliko ya mtaala unaoweza kuandaa wahitimu kujiajili, kuajiliwa katika kukuza uchumi wa kati

Karibu tujadili

Let's be A Job creator rather than being the Job seeker
Izo conference ndio janga lingine mnawapotezea mda zaidi vijana mkisubiri posho baada ya vikao vyenu yani hii nchi watu wabinafsi sana.
 
Back
Top Bottom