Umekula tunda gani leo?

Umekula tunda gani leo?

Mlo wangu wa kila siku jioni saa 2 ni matunda. Tikiti, parachichi, nanasi, maembe, papai. Nikila hii mchanganyiko huo situmbukizi kitu kingine mpaka kesho. Nakula sana mpaka kushiba
 
Pilipili nalo tunda!?
Kwa hakika kama kuna mtu kati yetu asubuhi ya leo kala tunda lolote lile basi ni wale waliolala zile hotel zenye bed n breakfast full course. Wengine wetu kwa uchache mno ni wale wafanya diet na kwa uchache zaidi wale wanaotambua umuhimu wa matunda mwilini kiafya. Wengi wetu humaliza mpaka wiki bila kula hata kipande kimoja cha tunda lolote.

Wengi huwa hawali matunda mpaka waandikiwe na daktari kama sehemu ya tiba. Kwao kula tunda ni sehemu ya anasa na kupoteza pesa..

Matunda yana faida kubwa mwilini kiafya kuliko hata nyama. Matunda ni sehemu muhimu ya tiba. Matunda yana uwezo wa kukujenga kiafya na kukukinga na maradhi mengi. Ni afadhali mara mia ukala matunda ya buku kuliko kula mchemsho wa buku 2, Matunda ni tiba ya magonjwa mbalimbali.

Matunda ni sehemu muhimu ya tiba mbadala na ujenzi wa mwili imara na wenye nguvu.
Baadhi yetu hupendelea shurubati zaidi kuliko matunda yenyewe. Ni sawa pia lakini shurubati isiyo halisi inakuwa imechanganywa na vionjo vingine hivyo kupunguza kwa kiasi fulani nguvu ya kutenda.

Huu ni ushauri wangu kwako pamoja na kunywa maji mengi na kupangilia milo yako lakini usisahau kitu hiki muhimu sana TUNDA. Jitahidi kupata kipande cha tunda kwenye kila mlo wako.. kuna siku utanikumbuka na kunishukuru kimoyomoyo
Je, umekula tunda gani leo?

 
Hapana pilipili sio tunda
Sehemu nyingine ni ngumu kupata matunda ya asili, inakuwa ngumu sana kula matunda lakini kwa wale wenzetu na mie tuliokulia maeneo kama Mbeya, Kilimanjaro, Kagera, Ruvuma, Arusha, nk matunda tunakula kama mgonjwa na daktari.
 
Kipindi cha nyuma nilikuwa naona wanaokula apple kama watu wanaopenda ufahari, kumbe apple linaondoa sumu kwenye ini, nilikuwa naangalia videos za faida za matunda YouTube nikajua apple lina faida kubwa sana.

Alafu kuna matunda yameadimika mf Stafeli, Mzaituni siyaoni, mimi nilipokulia yalikuwa kibao, watu wamejenga na miti yenyewe wakaikata.
 
Kipindi cha nyuma nilikuwa naona wanaokula apple kama watu wanaopenda ufahari,kumbe apple linaondoa sumu kwenye ini,nilikuwa na angalia videos za faida za matunda YouTube nikajua apple lina faida kubwa sana.

Alafu kuna matunda yame hadimika mf Stafeli,Mzaituni siyaoni,mimi nilipokulia yalikuwa kibao,watu wamejenga na miti yenyewe wakaikata.
Wengi hawajui umuhimu wa matunda mwilini kiafya matokeo yake ndio hayo
 
Kwa hakika kama kuna mtu kati yetu asubuhi ya leo kala tunda lolote lile basi ni wale waliolala zile hotel zenye bed n breakfast full course. Wengine wetu kwa uchache mno ni wale wafanya diet na kwa uchache zaidi wale wanaotambua umuhimu wa matunda mwilini kiafya. Wengi wetu humaliza mpaka wiki bila kula hata kipande kimoja cha tunda lolote.

Wengi huwa hawali matunda mpaka waandikiwe na daktari kama sehemu ya tiba. Kwao kula tunda ni sehemu ya anasa na kupoteza pesa..

Matunda yana faida kubwa mwilini kiafya kuliko hata nyama. Matunda ni sehemu muhimu ya tiba. Matunda yana uwezo wa kukujenga kiafya na kukukinga na maradhi mengi. Ni afadhali mara mia ukala matunda ya buku kuliko kula mchemsho wa buku 2, Matunda ni tiba ya magonjwa mbalimbali.

Matunda ni sehemu muhimu ya tiba mbadala na ujenzi wa mwili imara na wenye nguvu.
Baadhi yetu hupendelea shurubati zaidi kuliko matunda yenyewe. Ni sawa pia lakini shurubati isiyo halisi inakuwa imechanganywa na vionjo vingine hivyo kupunguza kwa kiasi fulani nguvu ya kutenda.

Huu ni ushauri wangu kwako pamoja na kunywa maji mengi na kupangilia milo yako lakini usisahau kitu hiki muhimu sana TUNDA. Jitahidi kupata kipande cha tunda kwenye kila mlo wako.. kuna siku utanikumbuka na kunishukuru kimoyomoyo
Je, umekula tunda gani leo?

Mi nimekuja tunda lile TUNDA LA KIMASIHARA.

#YNWA
 
Sijui ni mazoea au la ila ni mara chache sana kula chakula bila matunda hasa ndizi, na kingine napenda sana miwa na juisi yake sa sijui nayo ipo kwenye category ya matunda au la

Kingine pia nilianza kupenda matikiti ila baada ya kusikia hekaya za baadhi ya matikiti kama sio yote (huko mashambani) kudungwa sindano ili yasifanye nini sijui..., nikapoteza interest nayo kabisa.

Kilichobaki ni kuongeza idadi ya matunda ili kuondoa domination ya ndizi mbivu pekee, hivyo nina mpango wa kujikita zaidi kwenye machungwa, matango, parachichi, nanasi, papai na maembe.
 
Back
Top Bottom