Umeme unakatwa saa sita usiku, hadi saa 12 jioni

Siasa za bongo ngumu.

Kipindi Dr Kalemani anatumbuliwa JF tulishangilia na kupongeza uteuzi wa January, Sukuma gang tukasinyaa kusubiri weledi wa waziri aliyeshangiliwa na wengi.

Muda si muda akaanza reshuffling, watu wakaula wa chuya, bodi ikajazwa wabobezi wa nishati. Tukapongeza humu.

Baada ya siku tukaambiwa sukuma gang waliharibu nchi, kwa miaka mitano mitambo ya umeme haikuwahi kufanyiwa marekebisho , watu wakashangilia humu. Sukuma gang tukaendelea kusinyaaa.

Kali ya waziri akasema Bwawa la umeme halitakamilika Kama ilivyopangwa awali, kwani tunahitaji Cranes kutoka mamtoni sijajua ilifikia wapi lakini sisi sukuma gang tukaendelea kusinyaa.

Tukaenda mikanganyiko ikawa mingi, huku wanasema mgao wa umeme huyu anasema hatutalala gizani huyu naye anakana hadi sasa nachokumbuka ni kwamba Rais ametoa agizo mgao wa umeme usiwe kama ilivyopangwa mjengoni yakasikika makofi lakini uhalisia

Hakuna umeme mtaani, wenye biashara zinazohitaji umeme wanajua, tumehamia kununua tochi hapa nina betri 10 reserved kwa ajili ya tamko la tanesco.

Sisi sukuma gang tunaendelea kunyamaza..Watu wale kulingana na urefu wa kamba zao wavimbiwe vya kutosha.

Hallelujah!!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Swala la umeme limekuwa changamoto kubwa sana mimi najiuliza maswali mengi sana huu usiku wanafanya matengenezo gani?
Na kwa nini wasingefanya matengenezo kipindi kile maji hakuna?

Yaani kwenye mgao wa upungufu wa maji hawakuona opportunity ya matengenezo.
 

Umeme haujawahi katika napokaa Kwa zaidi ya dakika 5 for years!
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja

SIMU : 0748550000
 
Naona zoezi lao la kutoa nguzo za miti na kuweka nguzo za zege linaendelea

Ova
 
Bujibuji Simba Nyanaume

Haya sasa toa ushirikiano utatuliwe tatizo lako

Ova
 
Huku kwetu sijaona mgao, umeme upo vile vile labda ukatike na kurudi baada ya dakika 10-20! Ni uswazi tu
 
Makontena ya jenereta ndo yanaingia nchin umeme ukiwepo nan atanunua jenereta
 
January ni "Overrated" leader,uwezo ambao jamii inaamini/imeaminishwa anao,in reality HANA
Jamii inayoamini January ni kiongoz mzuri ni Tanzatwitter na JF tu.
 
Wawajibike, hawana uwezo wa kuwa wizarani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…