Umeshawahi kuachana na mpenzi wako kwa sababu umeona mahusiano yenu "hayatofika mbali" (hamjagombana kabisa)

Wakati nikiwa kijana kama nyie niliwahi kupendana na binti mrembo. Yule binti alikuwa freak katika mambo ya usafi. Tuliwahi kukaa pamoja wakati tuko chuoni nje ya nchi. Basi ilikuwa taabu ile kupenda kwake usafi kupita kiasi. Akimaliza kutumia sink anafuta kwa kitambaa ili kusibaki tone la maji. Nikikata ndevu zangu akakuta kaudevu kamoja kamebaki kwenye sink ama tone la maji limerukia kwenye sakafu ilikuwa ni ugomvi mkubwa sana. Nikikaa kwenye kitanda nikitoka, ilibidi nipige pasi ile sehemu niliyokuwa nimekaa inyooke! Nikaona hapa nitakufa kabla ya siku zangu. Baada ya chuo, nilikata mawasiliano kimya kimya... Ni mrembo lakini mpaka leo hajaolewa - miaka yake 40 na kitu.
 
Ila mkuu nawe ungeoa yeye, ungeeeka ndani kabisa
 
Hahahahaaaaaaaa pole mkuu hiyo ilikua adhabu aisee
 
Kuna boya nilimuacha jamaa alikuwa ananipangia mavazi ila kutoa pesa kununua hataki anataka nivae nguo za ajabu zenye kuonesha mwili wangu nilisepa haraka.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Mtu anakupangia mavazi halafu hataki kukununulia,,akome[emoji1787].
Mimi mwanaume wa kuja kunibadilishia mavazi ajiandae tu pesa ya kutosha Maana sina mavazi mchanganyiko[emoji23][emoji23].
Nimejaza mavitenge yangu tu
 
Aisee
 
Watu Mungu mnampenda kumbe ila kwa nini amri zake hamfuati? Back to topic, unaweza kumwacha mtu kwa kuwa eti hamtofika mbali kumbe yeye hana mpango wa kwenda huko mbali kwa hiyo ni vema ukaendelea kujiburudisha tu
[emoji41][emoji41]
 
Umeona eeh shoga[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Natamani nione siku moja[emoji23]
Hahahaaaaa ila mmh kudundwa jamani uuwiiii... Yani mi nikigundua hapa nshaharibu uuwiiii na magoti juu kuomba msamaha yani mtu atafoka wee mi kimya neno langu moja tu nimekosa naomba unisamehe sitarudia tena...... Nawashangaaga watu wadada wanaovimba hahahaa unakuta mtu anaendeleza ligi hata haogopi jamani... Hahahaa tuwe wapole hivi hivi shoga angu tusije pasuka siku
 
Ukikosa kweli unaomba msamaha.
Hata Mimi nikikosa Cha kwanza ni kuomba msamaha.
Lakini kuna situation yaani unaona kabisa hujakosa mf hujapokea simu kwa wakati,jitu linatengeneza kesi na huku anajua nyumbani kazi zote zangu.
Huyo kuomba msamaha siwezi,atausikia tu
 
Hahahaaa kweli kuna situation my dear
 
Upo kama mimi mama mchungaji hahahaaaa...
Nguo ambazo sio za vitenge nahisi hata 10 hazifiki[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Nina vitenge,, yaani ndo mitoko hiyo hiyo,za kanisani hizohizo.. nyumbani Ni hizohizo na huwa hazipauki Maana ninazo nyingi[emoji23][emoji23]
 
Alikuwa hataki mavazi ya kiostadhi na mimi toka mdogo nimelelewa kwenye aina hiyo ya mavazi ndefu kichwa nifunike tofauti na hiyo siwezi kutoka home kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…