Umeshawahi kuachana na mpenzi wako kwa sababu umeona mahusiano yenu "hayatofika mbali" (hamjagombana kabisa)

Umeshawahi kuachana na mpenzi wako kwa sababu umeona mahusiano yenu "hayatofika mbali" (hamjagombana kabisa)

Upendeleo hudanganya na uzuri ni ubatili bali mwanamke amchaye Bwana ndiye atakaesifiwa. (Mithali 31:30) uliweza isome yote ikipendeza hii iwe standard yako

Muhimu weka vigezo vya unaemtaka lakini Muombe Mungu kwa imani yako, fuata amri zake,sheria na taratibu zake... Lakini jitahidi usiwe na haraka kwenye mahusiano jipe muda na chunguza hata katika namna muhisika hajui ili kabla hujafanya maamuzi uwe na picha kamili.....
hapa pa "kutokua na haraka na mahusiano" nilishawahi pajaribu

kilichonkuta wajanja walimuoa mpenzi wangu na kadi ya harusi nliletewa

kisa kujitia baba paroko sina haraka nipo kwenye utafiti.
 
[emoji4][emoji4]...

Tumezaliwa na kukuzwa katika generations tofauti, wanaoandika hivyo wengi ni wa kizazi cha utandawazi "internet era"...

Naelewa sana tuu! Tabia ya kuomba omba sio poa kabisaa!

Ni kama mimi, mwanaume aniombe hela nitaelewa amekwama na sio aniandikie zile "xaxa, xku n.k" hilo siwezi kulivumilia kabisaa tho sijawahi kumbana nalo!
 
Kwa mimi nimeshawahi kukatisha safari baada ya kuona hili gari hili sitoboi nalo Kigoma,safari lazima iishie njiani tu maana sio kwa ma mushkeli haya.

Nilipata mpenzi huko nyuma tukapendana vizuri tu,maisha yakawa yanaendelea Si unajua tena mnapokua wapenzi lazima kila mtu ajue ratiba za mwenzake hata kama hatupo pamoja ila akiulizwa sasa hivi CONTROLA yuko wapi anajua cha kujibu kadhalika na kwangu.

Jumapili ni siku ya ibada yeye yupo kwao na mimi kwangu kila ikifika jpli mimi naenda zangu kanisani nikirudi namcheki mwenzangu namuuliza vipi za ibadani,ananijibu kua hakwenda,ukimuuliza kwanini anakwambia alikosa nguo, basi unauchuna.

ikifika jpli ijayo hivyo hivyo haendi sababu yake ni nguo/uchovu/kuumwa aseee nilimwambiaga ukweli mkavu kabisa ila bado tabia ikawa ile ile,Nguo za kutoka mitoko anazo kama 100 NA USHEEE ila za kanisani hana,ikikaribia jpili nguo zote Znachafuka.

Yule dada nilimpiga chini maana nilijihisi na date na PEPO maana hata tukiwa pamoja ukimwambia Ombea chakula "hataki" ukimlazimisha ataishia kuanza kula bila kuomba,nikaona isiwe kesi Nikaachia nafasi wengine.

Another one

alikua ni mpenzi wangu tulipendana haswaaa,siku 1 nilikua zangu nimekaaa nacheki Tv nikamuuliza "hivi una salio kwenye simu yako nataka kumtumia mama" akaniambia simu haina hata salio kuna 5000 tu",nikamwambia hiyo hiyo mtumie mama kwa vocha itamtosha sana akanijibu asee unawezaje mtumia mama sh.5000 ya vocha mwanaume mzima?

nikamuuliza swali "eti umeniulizaje??" akarudia swali lake "unamtumiaje mama 5000 ya vocha mwanaume mzima?" nikamwambia huo ndio uwezo wangu kuliko nisimpe hiyo 5000 akae bila vocha si bora nimtumie hiyo najua atajiunga vifurush kidogo kidogo na hatoitumia yote,ila yule mwanamke alinikatalia katu katu..

Akaniambia wewe mtumie mama hata 10,000 kidogo ita leta maana,nikamsisitiza siwezi tuma zaidi,akasema basi mwache akae hivyo hivyo au kakope hata kwa mtu umtumie,aseee tukiacha masihara yule dada nilimwambia live pale pale "naomba uondoke kwako niache kidogo" kweli akaondokaa

sikumtafuta tena na ndio ukawa mwisho wangu na yeye,ki ufupi nina list ya magari kadhaa niliyositisha nayo safari kutokana nakuona huko mbeleni hatutokuja kuwezana kabisaaa,so nikaamua tu kujiongeza.

SweetieLee Ulishawahi anzisha thread fulan hivi ya kumkinai "crushiee" wako sasa ile situation ebu fanya hakua just a crushie ila mliendelea hadi mkawa wapenzi then baada ya wiki mbili au mwezi unamkinai au inatokea tu kitu anakufanyia "kinakuchefua kabisaaa"....

Kuna dada nilimuuliza hili swali akaniambia yeye pia kashawahi muacha mtu,kisa ilikua kampenda jamaa vizuri jamaa alikua mtu mstarabu kupita maelezo ila hakuamini siku wanafanya mapenz jamaa akawa anasisitiza anataka TIGO asee yule dada akaniambia CONTROLA nilimuangalia yule kaka juu mpk chini kisha nikainuka nikavaa nguo nikasepa,na ndio ikaawa mwisho wa mazoea na yule mkaka.

Haya na wewe tuambie ilikuaje ukamuacha ukasitisha safari

Note : sababu isiwe UGOMVI au mkwaruzano wa aina yeyote ile.
yaan mkuu mim nimetoka kuvunja mahusiano Jana tu kwa sabab iyo naona mwenzang ananichora tu af me nipo seriously na yeye nikakata mitambo
 
unafikiri wa umri huo atakupga kizinga cha vocha hoooiiyaaaa

hao akikukosa kosa sanaaaaaaa "hela ya kodi"

au simu yake samsung s7 edge imepasuka kioo so anaomba umsaidie ipone

kaulize bei ya hicho kiooo sasa (unaweza t
Of course ni matatizo ya kujitakia Mkuu choose wisely ukiona you are drowning why carry on

Mimi sio muhumini wa kulalamika na nawashangaa sana wanaolalamika fanya assessment ya Maisha yako kaa kwenye nafasi yako
Ushauri mzuri sana huu
Cc CONTROLA
 
Kuna mmoja huyu Juzi Juzi nimeona niachane nae maana niliona Safari ya kuanzia Mtoni kwa azizi ally mpaka Mbagala Tu haiwezekani

Kisa kiko hivi beibe nimeichoka IPhone yangu 7+ nataka XR, nikamwambia Mfuko wangu unaweza ku Afford 8+ hiyo XR siwezi si kwamba sina ila siwezi weka bajeti huko kwenye mambo ya fashion na luxury ambazo Kimsingi hazina mwisho na kila siku zinatoka mpya

Majibu yake sasa ooooho hauwezi kunipangia choice unayotaka wewe mimi natumia brand ninayotaka Mimi, nikajisemea Dooh hapa gari haiwezi kufika Safari nikashuka njiani

Nb; Sikulalamika nikamuacha na Maisha yake, Jaribu kumbadilisha mwenzi wako ukiona haiwezekani Walk away Don’t kill yourself [emoji120]
Alikuwa anajifanya nayeye ni Muhimili
 
Kuacha acha nayo sio poa...kitu muhimu ni wake wa waume should learn how to behave wakiwa mahusianoni...

It takes two to tango...
Si unamuacha tu unatafuta ambaye hana vizinga?? Au wasio na vizinga ndiyo wanakuwaga wabovu na ninyi mnataka wazuri na wasio na vizinga??
 
hapa pa "kutokua na haraka na mahusiano" nilishawahi pajaribu

kilichonkuta wajanja walimuoa mpenzi wangu na kadi ya harusi nliletewa

kisa kujitia baba paroko sina haraka nipo kwenye utafiti.
Hakua wa kwako huyo mkuu, haya haraka haraka imekufikisha wapi mkuu?? Zaidi ya kukutana na vimeo
 
Si unamuacha tu unatafuta ambaye hana vizinga?? Au wasio na vizinga ndiyo wanakuwaga wabovu na ninyi mnataka wazuri na wasio na vizinga??
shida sio kumuacha

shida sio uzuri

shida ni kumjua asie na vizinga
 
CONTROLA naomba usinikumbushe, niliwahi date mwanaume ana maneno huyo..!!
Yaani ukikosea usiombe vichambo vyake utajuta!! anakuchamba mpaka unahisi uchizi, vile ukijishusha kuomba radhi ndo kama unachochea moto wa kuchambwa, na vile I hate offensive words niliondoka kimya kimya hata sikuaga.! Mpaka Leo I can't date mtu wa kunitukana hata kidogo maana hiyo ni ticket ya one way to the 'delete button'..!!

Mwingine huyo alikuwa ana wivu huu wangu hauoni ndani, in fact huu ukasome, let say mnaongea ukamuambia I got to do something, anakuambia how long will it take? unajibu only 10 minutes sababu nataka kukosha vyombo, After a while anapiga, unajibu umemaliza ila unadeki, haha' utajuta unaambiwa ulisema tu vyombo hukusema kama kuna kudeki.!! Hapo ujue kashamaindi muda sana, yakanifika haaaapa.!! Jamani nilikimbia speed mfanowe hakuna.!!
Hahahahaha uyo mwanaume wa vichambo Ni mtu wa pwani Nini??
 
Back
Top Bottom