Umeshawahi kujiuliza wewe ni nani?

Umeshawahi kujiuliza wewe ni nani?

Yeah, hata mimi hua naona ni kwa sababu sasa nimekua mkubwa na nina mambo mengi ya kufanya vilevile kichwa kimejaa mambo mengi tofauti na nilivyokua mtoto.
Utoto raha sana, no stress tofauti na sasa.
Hivi sasa ukitaka kujiuliza wewe ni nani mara yanakuja mawazo mengine!

Kweli kbs
 



Wewe ni nani?



Wewe sio kazi yako unayofanya, wewe sio kundi la watu unalojihusisha nalo.

Wewe sio mawazo yako,

Wewe sio Akili yako,

Wewe sio mwili wako,

Wewe sio mtu mwenye furaha, huzuni, hasira wala shida kama unavyojifahamu,

Wewe sio tafsiri uliyozoea kuifahamu.





Wewe ni nani?

Wewe sio ambaye wazazi wamekuambia,

Wewe sio ambaye marafiki wamekuwa wakikuambia,
Wewe sio ambaye viongozi wa dini wamekuwa wakikuambia,
Wewe sio ambaye serikali imekuwa ikikuambia,

Wewe sio maelezo unayotumia kujielezea kuhusu wewe.




Achia mbali majina unayoitwa, maelezo unayojielezea kwenye mitandao kama Facebook au mitandao mingine ya kijamii.




Achia mbali jina lako, aina ya mtu unayejijua wewe ndiye, sifa ulizonazo, muonekano, asili, tamaduni yako au sifa ulizoandikiwa kwenye kitambulisho chako cha kazi au masomo,




Je unajisikiaje hivyo vyote ukiviachia mbali na kujiuliza wewe ni nani.




Nini kinabakia ukitoa mali zako, mwili, akili, shida, mawazo yako, imani yako, mazoea yako, tamaa zako, jina unalopewa na watu au unalojipa wewe, na sifa unazopewa na watu na sifa unazopewa wewe?




Wewe ni nani?




Kama wewe sio unachofanya,

Kama wewe sio unachofikiria,

Kama wewe sio unachopenda,

Kama wewe sio maelezo unayotumia kujitambulishia,

Je Wewe ni nani?




Tambua kwa kina...




Hauzuiliwi na mipaka ya mwili,

Wala wewe sio mapigo ya moyo wako,

Wewe sio Akili yako, mawazo yako na hisia zako,

Je kama wewe sio hivyo vyote je wewe ni nani?




Vuta pumzi taaratibu, hewa hiyo inaingia kwenye mapafu halafu inaingia kwenye kila seli ya mwili wako.

Funga macho, acha kuwaza, acha kuweka mawazo nje yako, hisi nafasi inayobakia iliyo kimya, na isiyo fikiria, waza, wala isiyokuwa na hisia yoyote kutoka kwenye milango ya ufahamu.




Kumbuka wewe ni nani, kumbuka hauna mipaka, mwili utakufa utauacha, jinsia yako nayo unaiacha, mali utakuwa nazo bali nazo utaziacha, hisia ulizonazo ambazo chanzo chake ni mwili wako nazo utaziacha mwilini, hasira na mawazo nayo yote utayaacha, sifa ulizopewa kama vile ulikuwa mchoraji bora au mwimbaji bora n.k nazo utaziacha kwani nazo zinategemea mwili mfano unaimba kwa kutumia mdomo lakini ukifa unauacha na huo mdomo na sifa zake ulizozizoea.

Je kama maisha yako ya hapa duniani yatakapoisha vyote hivi unaviacha...

Je wewe ni nani???








Wewe ni ufahamu unaofahamu vyote hivyo,

Jiangalie ndani yako kwa kina,

Wewe ni empty,hauna kitu

Wewe ni sehemu ya muumbaji,

Kila ukionacho, unachokiwaza, unachokitenda, na unachokizungumza kinawakilisha ulimwengu wa ndani yako.




Wewe na mimi ni kitu kimoja, wewe upo kama mimi na mimi nipo kama wewe.




Tunachopaswa kufanya katika safari ya maisha ni kujijua na kujitambua. . .



[h=3]Asante.[/h]
Who am I ,swali zuri na umebana kotekote kwa kusema jina lako sio wewe,akina amina wapo wengi,huu ni uthibitisho kuwa hilo jina ni kibandiko tu na unaweza kubadili jina na ukabaki yuleyule,hili swali linaweza kukuchanganya lakini kuna viashiria vitakubainisha kuwa wewe ni nani
Kwanza wewe ni mtoto wa mtu fulani ,ambaye amejipa utambulisho na amepokea utambulisho mwingine wa babu yako na babu wa babu yako na kuendelea,hii inamaanisha utajitambua wewe ni nani kwa kuangalia umetoka familia na mizizi yake
Pili kwa kuangalia DNA yako,hapa duniani hakuna mwenye DNA zinazofanana,hata mapacha wana DNA zinazotofautiana,huu ni utambulisho tosha kuwa binadamu hatufanani na kila mtu ana nasaba/DNA yake.
Nini kingine kinachokutofautisha baina ya wewe na mimi?mahali na muda kwa kiingereza wanasema space and time,mahali nilipo mimi na mahali ulipo wewe ni tofauti hata kama wote tupo tabata na tunakaa nyumba moja,chumba kimoja,kitanda kimoja bado wewe utalala pemben yangu au juu yangu ila hatutaweza kuwa katika sehemu moja kwa asilimia 100,lazima tupishane space.kwa nadharia yako kusema kuwa sisi ni wamoja haina ukweli,tupo tofauti na hatuwez kuwa sawa hata siku moja,mazingira uliyokulia na mimi ni tofauti,mazingira uliyokulia yanaweza kukufanya uwe mtu wa hasira wakati mimi nimekulia mazigira tofauti ni mpole,kila mtu anapata tabia yake kulingana na makuzi aliyokulia na namna gani alivyofanikiwa kukabiliana na changamoto alizokutana nazo,kama alipokuwa mdogo akiwa ana hasira anafanikisha jambo lake basi tabia yake itakuwa hivyohivyo.
 
Mimi ni Mimi ,nilivyo Mimi nitabaki kuwa Mimi , nisipo Mimi sio Mimi na wala sio mimi
 
Mimi ni Mimi ,nilivyo Mimi nitabaki kuwa mimi , nisipo Mimi sio Mimi wala sio Mimi
 
Iam a Spiritual bro,covered by a body sorrounded by contextual..! daily living for preparing destiny that is my better place.!
 
Iam a Spiritual bro,covered by a body sorrounded by contextual..! daily living for preparing destiny that is my better place.!
 
Who am I ,swali zuri na umebana kotekote kwa kusema jina lako sio wewe,akina amina wapo wengi,huu ni uthibitisho kuwa hilo jina ni kibandiko tu na unaweza kubadili jina na ukabaki yuleyule,hili swali linaweza kukuchanganya lakini kuna viashiria vitakubainisha kuwa wewe ni nani
Kwanza wewe ni mtoto wa mtu fulani ,ambaye amejipa utambulisho na amepokea utambulisho mwingine wa babu yako na babu wa babu yako na kuendelea,hii inamaanisha utajitambua wewe ni nani kwa kuangalia umetoka familia na mizizi yake
Pili kwa kuangalia DNA yako,hapa duniani hakuna mwenye DNA zinazofanana,hata mapacha wana DNA zinazotofautiana,huu ni utambulisho tosha kuwa binadamu hatufanani na kila mtu ana nasaba/DNA yake.
Nini kingine kinachokutofautisha baina ya wewe na mimi?mahali na muda kwa kiingereza wanasema space and time,mahali nilipo mimi na mahali ulipo wewe ni tofauti hata kama wote tupo tabata na tunakaa nyumba moja,chumba kimoja,kitanda kimoja bado wewe utalala pemben yangu au juu yangu ila hatutaweza kuwa katika sehemu moja kwa asilimia 100,lazima tupishane space.kwa nadharia yako kusema kuwa sisi ni wamoja haina ukweli,tupo tofauti na hatuwez kuwa sawa hata siku moja,mazingira uliyokulia na mimi ni tofauti,mazingira uliyokulia yanaweza kukufanya uwe mtu wa hasira wakati mimi nimekulia mazigira tofauti ni mpole,kila mtu anapata tabia yake kulingana na makuzi aliyokulia na namna gani alivyofanikiwa kukabiliana na changamoto alizokutana nazo,kama alipokuwa mdogo akiwa ana hasira anafanikisha jambo lake basi tabia yake itakuwa hivyohivyo.

Samahani sana kwa kuchelewa kuiona hii comment. Umejitahidi sana kujibu. Lakini mkuu hata hivyo ulivyovitaja navyo vinapita. DNA sio identity yako bali ni identity ya Mwili ulio nao sasa. Ukifa unaacha DNA zako kwenye mwili wako. DNA ni kama code ambayo inajitengeneza pale mbegu mbili zinapoungana na chembechembe zako zinakutana na kushuffle kutengeneza code mpya ambayo haitapishana sana na code za mbegu zilizoumba. Ndio maana unafanana na ndugu zako.

KUhusu space na time, space na time is an illusion. NI kama vile ilivyo kwenye matter. Matter is energy. Hivyo kila uonacho ni energy na sio matter kama unavyoona. Ukichunguza deep labda ka microscope nzuri utaona ni energy zinavibrate katika shapes tofauti na katika vibration tofauti kutengeneza reallity.

Ila ukitaka kujua wewe ni nani angali ndani yako. Usijidefine kwa vitu vinavyopita kama vile jinsia, muonekano, mawazo, maisha n.k kwani vyote hivi unaviacha hapahapa duniani.
 
mimi ni mimi hamna mtu kama mimi

Usijidanganye. Ndio maana unafundishwa usimtendee mwenzio usichopenda kutendewa, lengo kuu ni kuwa wewe ni mimi na mimi ni wewe. Ukinitendea mabaya umejitendea wewe na sio mimi. Life is an illusion. Wazo la kujiona wewe ni wewe ni jaribio la kupima akili yako. Ni kama vile mbwa anayeona mkia lakini hajui kuwa ni wake. Amka na uione dunia kwa undani, ina siri kubwa sana ndugu yangu.
 
Iam a Spiritual bro,covered by a body sorrounded by contextual..! daily living for preparing destiny that is my better place.!

Mwanadamu ni sehemu ya ulimwengu iliyojitambua. Ufahamu wako wa kuwa wewe upo na ndiye huyu ni tofauti kuu kati yako na viumbe vingine na ni tofauti kati yako na vitu ambavyo havina uhai. Lakini utambue kuwa kila kitu kinategemeana ulimwenguni. Unachokiexperience sio hakipo nje yako bali kipo ndani yako. NI sawa na kujitazama kwenye kioo bila kujua kuwa unayemuangalia ni wewe.

Wewe sio huo mwili, maisha yako na huo mwili ni mafupi sana kulinganisha na uwepo wako wa milele. Wangapi walikufa zamani na waliishi miaka mingapi na umepita muda gani? Mfano ukiishi miaka 90 katika body yako miaka itapita na miaka hiyo inapitwa kulinganisha na miaka ya uwepo wako wa milele.

Kujua wewe ni nani, usitumia ufahamu wa mwenzio anavyosema, kwani hujui naye amejua wapi kwani kila mwanadamu anaishi katika reality yake. Kujua wewe ni nani ondoa unachofundishwa ni jiangalie ndani yako, jichunguze kwa makini na hakikisha unapata jibu. JIbu lipo ndani yako.
 
Samahani sana kwa kuchelewa kuiona hii comment. Umejitahidi sana kujibu. Lakini mkuu hata hivyo ulivyovitaja navyo vinapita. DNA sio identity yako bali ni identity ya Mwili ulio nao sasa. Ukifa unaacha DNA zako kwenye mwili wako. DNA ni kama code ambayo inajitengeneza pale mbegu mbili zinapoungana na chembechembe zako zinakutana na kushuffle kutengeneza code mpya ambayo haitapishana sana na code za mbegu zilizoumba. Ndio maana unafanana na ndugu zako.

KUhusu space na time, space na time is an illusion. NI kama vile ilivyo kwenye matter. Matter is energy. Hivyo kila uonacho ni energy na sio matter kama unavyoona. Ukichunguza deep labda ka microscope nzuri utaona ni energy zinavibrate katika shapes tofauti na katika vibration tofauti kutengeneza reallity.

Ila ukitaka kujua wewe ni nani angali ndani yako. Usijidefine kwa vitu vinavyopita kama vile jinsia, muonekano, mawazo, maisha n.k kwani vyote hivi unaviacha hapahapa duniani.

Na tukishaviacha vyote hapa duniani sisi tunaenda wapi?
 
swali hili nilikuwa najiuliza zaman. na nilkuwa nabaki kujishangaa. lkn kwa sasa hata nikitafakar haitokei tena hali ile.
 
Fahamu kwanza wewe ni nani. Utapata majibu yote. Huwezi kujua unaenda wapi kama hujui wewe ni nani. Kwa sababu hutajua asili yako.

Kwahiyo njia ya kujua hayo yote ni kwa kujiuliza maswali kuhusu mimi? Maana mimi nikianza tu kujiuliza hayo maswali huwa mawazo Yanakuwa mengi sana.
 
Nawazaga sana hayo mawazo nikilewa " all in all mimi ni mimi tu
 
Back
Top Bottom