Umeshawahi kujutia kumsaidia mtu?

Umeshawahi kujutia kumsaidia mtu?

Mkuu umenikumbusha machungu binafsi niliwahi kumsaidia brother shukrani aliyo nipa iliniumiza mno,Nikamsaidia tena rafiki kwa Sasa nimejifunza bora kuwa na roho mbaya. Allah anisamehe.
 
Inawezekana biashara zao au mafanikio yao yana mikataba katika ulimwengu wa Roho.
Si rahisi hata kidogo kumuacha ndugu yako porini masaa ya saa nne za usiku wakati uwezo wa kumsaidia unao.
Lakini muhimu ni kwamba saidia tu, wewe saidia kwa namna yoyote ile unaweza kusaidia.
Usitegemee chochote kutoka kwa unae msaidia.
 
Lakini hata yeye anaweza Kukosa hela. Kwani mwalimu anakuwa na hela kilasiku?
Wengine Wana miradi ya Maendeleo akiipata tu anapeleka huko.
Usipokipata unacho kihitaji kwa mtu fulani, usifikirie moja kwa moja kuwa umenyimwa.
Wanakuwa hawana wakati mwingine.
Inauma sana aseee. Kipindi namaliza chuo nilikuwa sina nauli kabisa ya kurudi home wazazi walipata majanga flan yakawamalizia pesa kabisa. Nikamuomba rafiki yangu kipenzi ambaye nilimsaidia sana na kumtreat kama ndugu kipindi iko alikuwa kapata ajira ya ualimu ana mwaka mzima kazini nikamuomba aniazime japo shilingi elfu kumi na tano then nikifika home ntamrudishia huwezi amini jamaa alininyima iliniuma saaana nikajifunza kitu ukiwa na shida watu wanakukimbia
 
pole sana bwana ndugu, huwa wanasema ukitoa toa bila kukumbuka na ukipokea pokea bila kusahau.
 
Wakati fulani nilikuwa Sina hela kabisaa. Kukawa na rafiki yangu nilimkopesha hela siku za nyuma, akawa hakulipa hela yangu.
Mie nikakausha.
Wakati huo Sasa amepata shida tena anataka nimsaidie na Mimi hela Sina.
Nikamwambia siko vizuri, lakini huyu ndugu yangu aliendelea kunisumbua kila Mara anataka hela wakati ukweli Sina.
Lakini akilini mwake anajua hela ninayo, sitaki kumpa kwasababu mwanzo hakurudisha wakati sivyo.
Na Kama ningekuwa na hela ningempa Mimi sijali.
Nikiwa nacho natoa tu, Kama msaada na Kama mkopo. Ukidhulumu nashukuru.
 
sijuti maana nilifanya nililoweza. nimeshawahi kumkopesha mtu pesa ambayo niliikopa kwa mtu mwingine ili tu nimsaidie kutokana na kushibana kwetu. Cha ajabu mimi nilimaliza mkopo wangu kwa mtu mwingine lakini yeye alinilipa theluthi tu na hapo anaishi good life kinyama huku mimi nakaa kishida tu. Halafu hata hashtuki ila sijutii maana kashajipa termination na somo gumu kanipa. Sasa hivi ninakupa ninachoweza kutoa, sijitoi mbuzi wa kafara tena
 
Dah kaka inawezekana lakini unafanya hivyo kwa ndugu zako hadi kwa mama mzazi aliyekuzaa(Mungu amrehemu shangazi)...Mwaka 2012 baba mdogo aliumwa sana wakati anaumwa akasema kabisa iwapo atakufa basi Likologeka(huyo mkuda) akitoa gari na tukizipokea hatutafika salama maana ameshindwa kumsaidia matibabu akiwa hai japo walimtaka sana msaada,,,,alipokufa ni kweli alitoa fuso 2 kitu cha ajabu hazikuwaka zile gari ikabidi zikakodiwe zingine msiba ulipoishi gari nzima.
Inawezekana biashara zao au mafanikio yao yana mikataba katika ulimwengu wa Roho.
Si rahisi hata kidogo kumuacha ndugu yako porini masaa ya saa nne za usiku wakati uwezo wa kumsaidia unao.
Lakini muhimu ni kwamba saidia tu, wewe saidia kwa namna yoyote ile unaweza kusaidia.
Usitegemee chochote kutoka kwa unae msaidia.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Mi nilimsaidia jamaa gari akaenda nalo kijijini kwao kaenda kutangaza ni lake siku amerudisha nikwa napita nalo njiani nasikia baadhi ya waliomuona nalo wananiuliza naona nanii kakuuzia gari yaani nilichoka ghafla
 
Dah kaka inawezekana lakini unafanya hivyo kwa ndugu zako hadi kwa mama mzazi aliyekuzaa(Mungu amrehemu shangazi)...Mwaka 2012 baba mdogo aliumwa sana wakati anaumwa akasema kabisa iwapo atakufa basi Likologeka(huyo mkuda) akitoa gari na tukizipokea hatutafika salama maana ameshindwa kumsaidia matibabu akiwa hai japo walimtaka sana msaada,,,,alipokufa ni kweli alitoa fuso 2 kitu cha ajabu hazikuwaka zile gari ikabidi zikakodiwe zingine msiba ulipoishi gari nzima.
Kuna wanoua Mama na Baba zao mpaka na wadogo zao karibu wote kwa mikataba ya aina hiyo, inategemea masharti.
Sasa jijui jepesi ni lipi.
 
Nilimsaidia mdada flani niliyekutana nae Chuo, alikuwa na shida sn kiuchumi, nikapigana mpaka akapata kazi Serikalini kwenye Taasisi nyeti sn, huu ni mwaka wa 4 hakuwahi ht kuniambia asante ya mdomo alivyoripoti kazn akauchuna tu, jamaa yng pia nikamsaidia kupata kazi kwenye Kampuni moja hapa bongo ya mawasiliano lakini alivyopata kazi hakuwahi kunitafuta wala kuniambia asante mpaka alivyoharibu kibarua na wakampiga chini kabisa ndio akanipigia sim nilimtimulia mbali aliniharibia kwa yule bosi mpk leo sina hamu tena ya kumsaidia mtu apate kazi.
Pole sana
 
Bro naelewa ni nini unapitia, mimi kuna wakati nasema kuwa i wont help anybody kutokana na mambo kama haya lakini inafikia point nasema basi tu Mungu ndo analipa, mimi imefikia point nimefuta namba za simu zote kwenye simu yangu za watu ambao hawana faida wala manufaa kwangu, nimefuta hata namba za ndugu mpaka wa kuzaliwa .

Kunakipindi mtu unapitia unajiona kama dunia nzima uko peke yako unakutana na mtu unamueleza matatizo yako tena mtu anaekujua kabisa lakini the way ana respond mpaka unakata tamaa unaona haina haja tena ya kueleza shida zako kwa yeyote.
Exactl exactly full exactly mkuu inakatisha tamaa sana hasa akiwa ndo pekee unaemtegemea

Kwa kipindi hki kigumu nachopitia sifahamu kama roho ya upendo na huruma kama itaendelea kuwapo
 
Katika hili jambo kuna kitu muhimu nasema haswa linapokuja swala la kujenga urafiki haswa ule wa kusaidiana, kuna makabila hata uwe na shida gani hawawezi kukusaidia ila wenyewe wanapenda kusaidiwa lakini wao wana roho ngumu na za paka katika kusaidia.

kiukweli mtanisamehe ila utafiti niliufanya ukiwa na urafiki na MPARE,MUHA, MRANGI na MKINGA usije ukategemea umepata rafiki wa shida na raha hata kidogo sahau kiukweli ukiwa na rafiki MUHA,MPARE,MRANGI NA MKINGA jiandae kisaikolojia siku ukipata shida usitegemee kama atakusaidia sahau kabisa hawa watu wameumbwa na mioyo ya husda ni wagumu kutoa vitu vyao kusaidia wenzao ila wao wanapenda sana kusaidiwa ..........

hivyo unapokuwa na urafiki na MPARE,MUHA, MRANGI na MKINGA
Mkuu wote hao mzazi wao n MMAKONDE
 
Mkuu pole sana, vumilia, katika jamii watu wa namna wapo. Japo unajutia msaada ulioutoa ila usikufanye usiwe na moyo tena wa kusaidia, endeleza tabia yako ya kusaidia kadri ya uwezo. Kusaidia sio lazima uwe na mali, msaada hata kwa mawazo chanya juu ya jambo husika.

Jamaa yako ipo siku atakukumbuka ila muda bado haujafika, wanadamu tuna hulka ya kusahau ya nyuma na kusahau waliotusaidia kufika hatua fulani ila tukikwama tunajikuta tunarejea tena kwa wale wale tuliowasahau tena kwa aibu(Muumba wetu atujalie tuepuke hii tabia).
Amina umeongea jambo la msingi sana mkuu
 
Tunapofeli ni pale tunapowasaidia watu na kutegemea kupokea sawsawa, zaidi au Pungufu ya misaada tunayotoa.
Huu ni mtazamo wa ajabu Sana, Binafsi sijawahi kuwa na mtazamo wa namna hii.
Fikiri kidogo juu ya ma Global wanaokuja kutoa misaada mbalimbali huku kwetu Kama wangekuwa mitazamo ya aina hiyo.
Ingetoka hela kweli ukizingatia jamii ambazo hawa watu huenda kutoa misaada?
Ukiwa na uwezo wa kumsaidia mtu fanya hivo.
Sijui mnajifunza kutoka wapi kutoa kunakotazamia kupokea.
Msaada ni tofauti na Mkopo.
 
Back
Top Bottom