Umeshawahi kupotea Kariakoo? Juzi ilibaki nukta nipige mayowe

Umeshawahi kupotea Kariakoo? Juzi ilibaki nukta nipige mayowe

Bhs wewe sio mzoefu na kariakoo, kariakoo unatakiwa uijue mitaa yake ma majina yake mfano machimbo ya nguo ni congo street na nyamwezi street lakin kuna mitaa ambayo inakutana na congo au nyamwezi ukijua hlo bhs kariakoo huwez potea mtu akikwambia nko agrey na congo chap unakimbia. Kariakoo kila bidhaa najua mtaaa inakopatikana[emoji119]
Wapi wanatoa imei za samsung
 
Kwa maelezo yako inaonesha manunuzi yako uliyafanya madukani...ningekuwa Mimi kila duka ningechukua mawasiliano yao tena nikitoka kwa nje kidogo napiga picha lango la duka.....tusioijua kariakoo vizuri tuko wengi.
 
Siku moja natoka tegeta na lift ya gari la mshikaji mida ya saa moja usiku,tulipofika k/koo jamaa kanishusha akaelekea zake ferry anaenda kigamboni mm ikabidi nichukue usafiri wa home kule gerezani..nikikumbuka Ile siku kilichotokea nachekaga tu maana jamaa tulipofika k koo aliniamsha Tu oya mwanangu kariakoo hii km vp tomorrow basi..nikashuka!!

usingizi jumlisha usiku sikujua kbs nimeshuka mtaa gani. Akili iliganda km nusu saa najiuliza jamaa kanishusha wapi hapa? Ikanibidi nitembee Tu mm mtoto wa mjini bn siwezi potea k/koo lkn bado akili haisomi kbs ninakoenda ni wapi

Nikasema isije nikatokezea kusikojulikana maana nimetembea kishenzi sifiki gerezani ngoja niulize.Nikamcheki muuza mayai kumuuliza asee naelekea iliko stend ya mwendo Kasi akanijibu sasa huku unakoenda mbona unakaribia kufika mnazi mmoja[emoji1787] ..nikamwambia niitie bodaboda akanijibu labda bajaji.Nikakodi bajaji Kwa buku 4 Hadi gerezani..nikikumbuka najiuliza hivi ilikuwaje nikapotea k/koo siku ile.Sipati jibu
watu bwana mnapoteaje kkoo yaani ww unakodi bajaji toka mnazi mmoja mpka gerezani kwa 4000 wa mikoani mnachekesha
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.
Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo...

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba,

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa,...

Nilikua na location 9..., Nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbenbeee,

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuma hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga...."?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, Yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi....

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki....

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau.

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayoweee....

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa, ..

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini....

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia,
Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani??? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza,

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi...
Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo....


Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta..

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawaliza watu, mliniona nikipita hapa?"
Nimewahi poteana hapo Kariakoo mtaa wenyewe sio complicated
Lengo langu niende NMB nyuma ya kituo cha polisi msimbazi ,nimepanda costa natokea manzese ,badala ya Costa kupita fire ikakatisha mitaa ambayo siijui nadhan ni kwenye ofisi za mwendo kasi pale ila sikunote nilikuwa nimelala,
Tukaenda shushwa mitaa siko familiar nayo
Nikaona isiwe tabu nikachukua bodaboda nikampa maelekezo anishushe BIG BON
Nikapelekwa ila akili yangu ikagoma kbsa kuwa pale ni big bon ,
Petrol station naiona,na kituo cha polisi nakiona ,Ili viko upande tofauti na vinapotakiwa kuwa(KWA mujibu wa akili yangu)
Yaani mfano akili inaniambia kituo cha polisi kinatakiwa kiwe upande wa kushoto kwako mimi naona kiko Kulia kwangu ,nikadaka wenge
Najua kbsa Nmb wako nyuma ya kituo cha polisi ,ila akili yangu inageuza mazingira
Nikaamua kujiripua kwenda mtaa unaonipeleka huko nyuma ya kituo cha polisi Ndo kama nikawa nimeRESET akili
Vitu vyote vikarudi kama vinavyitakiwa kuwa.
 
Wakati unanunua si pia unaandika kwa kitabu yako ? Basi pale juu andika jina laduka na number zao

Dubai wanakupa busness card
Maana kama unanunua sehemu zaidi ya 9 hata kama ni mzoefu ni rahsi kusahu

Mali bila daftari ....
Hapo ndiyo sahihi. Kila unaponunua andika address, jina na namba ya simu. Itakusaidia kuweka kumbukumbu vizuri.
 
Nimewahi poteana hapo Kariakoo mtaa wenyewe sio complicated
Lengo langu niende NMB nyuma ya kituo cha polisi msimbazi ,nimepanda costa natokea manzese ,badala ya Costa kupita fire ikakatisha mitaa ambayo siijui nadhan ni kwenye ofisi za mwendo kasi pale ila sikunote nilikuwa nimelala,
Tukaenda shushwa mitaa siko familiar nayo
Nikaona isiwe tabu nikachukua bodaboda nikampa maelekezo anishushe BIG BON
Nikapelekwa ila akili yangu ikagoma kbsa kuwa pale ni big bon ,
Petrol station naiona,na kituo cha polisi nakiona ,Ili viko upande tofauti na vinapotakiwa kuwa(KWA mujibu wa akili yangu)
Yaani mfano akili inaniambia kituo cha polisi kinatakiwa kiwe upande wa kushoto kwako mimi naona kiko Kulia kwangu ,nikadaka wenge
Najua kbsa Nmb wako nyuma ya kituo cha polisi ,ila akili yangu inageuza mazingira
Nikaamua kujiripua kwenda mtaa unaonipeleka huko nyuma ya kituo cha polisi Ndo kama nikawa nimeRESET akili
Vitu vyote vikarudi kama vinavyitakiwa kuwa.

Mkuu kupotea sio ujinga ni kawaida na kulijua jiji pia sio ujanja bali ni mazoea na sehemu hiyo
Wakati mwingine yanatokea mashariki we unaona ni magharibi
 
Dah nakumbuka kabla ya mwendokasi madaladala ya Mbezi tulikua tunapandia hapa msimbazi karibu na sheli ya big bon, kuna siku nimezunguka madukani wee! Kurudi kituo cha daladala nimesahau wala sheli siioni😂 nilizunguka siku ile na kuuliza watu naogopa wasijekua vibaka wakanipora so naitafuta ile sheli siioni kumbe nazidi kuelekea mnazi mmoja huko. Nikaona basi sasa kama ntaibiwa kwa kuuliza basi! Nikamfata machinga mmoja ndiyo akaniambia huku mbali rudi na njia ileee nikafata nikaona big bon hii hapa nilifurahii fasta nikaingia kwa bus😂😂😂

Siku nyingine ndugu yangu katoka mkoani kaja kununua mzigo kariakoo akaniomba nimsindikize yeye ni mgeni, tumeenda tumenunua kurudi tupande bus tena sioni kituo dah alinikejeli eti "nilidhani wewe ni mwenyeji kumbe mshamba tu kama mimi"😂😂 hadi tukaulizia kituo kilipo ndiyo tukaoneshwa.

Siku nyingine naenda kariakoo huku congo, hilo bus linaenda Machinga complex! Tumeshushwa hapo sielewi nimeuliza naambiwa nenda njia ile dah naendaa hata sifiki aah nikachukua boda kumbe nilikua nimevuka congo bila kujua naenda mnazi mmoja hivooo😂
 
Nimeona huu Uzi nikamkumbuka juzi ,ijumaa nilipotea , ni zaidi ya miaka mitano sijaingia kariakoo ndani ndani ,Sasa hiyo juzi ndo nikaenda, kilichonitokea stki ata kukumbuka🤣,

Nilienda asubuhi Kwa dhumuni la kununua kitu ambapo ingechukua Kama 2hrs niwe nimerudi, yaani nilinunua nilichokifata lakini cha ajabu nilorudi jioni baa da ya kupotea njia
 
Kuna dada alipiga yowe kama wewe na anachagua watu wakuuliza mimi nilivaa suruali ya kitambaa kubwa nimekula mkanda nje ndio akanifuata kuniuliza alizunguka kuanzia saa nne asubuhi Hadi nakutana naye saa kumi
Alinunua kandambili baada ya viatu vya mchuchumio kumchosha kwa kuzunguka
Alikuwa anataka atoke akapande bus za mbagala
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna dada alipiga yowe kama wewe na anachagua watu wakuuliza mimi nilivaa suruali ya kitambaa kubwa nimekula mkanda nje ndio akanifuata kuniuliza alizunguka kuanzia saa nne asubuhi Hadi nakutana naye saa kumi
Alinunua kandambili baada ya viatu vya mchuchumio kumchosha kwa kuzunguka
Alikuwa anataka atoke akapande bus za mbagala
Ila inataka moyo sana kupotea kariakoo
 
Mkuu kupotea sio ujinga ni kawaida na kulijua jiji pia sio ujanja bali ni mazoea na sehemu hiyo
Wakati mwingine yanatokea mashariki we unaona ni magharibi
Mtu unaweza ukapotezwa na akili yako japo ile sehemu unaifahamu,unaweza kupotea coz akili yako inakua ipo mbali sana,ndio maana mtu akitulia,akili nayo hutoa ushirikiano na utakumbuka unapokwenda,

Kupotea ni jambo la kawaida hasa kama mtu ana mawazo,kupotea sometimes hakuhusiani na uenyeji au ugeni.
 
Dah nakumbuka kabla ya mwendokasi madaladala ya Mbezi tulikua tunapandia hapa msimbazi karibu na sheli ya big bon, kuna siku nimezunguka madukani wee! Kurudi kituo cha daladala nimesahau wala sheli siioni😂 nilizunguka siku ile na kuuliza watu naogopa wasijekua vibaka wakanipora so naitafuta ile sheli siioni kumbe nazidi kuelekea mnazi mmoja huko. Nikaona basi sasa kama ntaibiwa kwa kuuliza basi! Nikamfata machinga mmoja ndiyo akaniambia huku mbali rudi na njia ileee nikafata nikaona big bon hii hapa nilifurahii fasta nikaingia kwa bus😂😂😂

Siku nyingine ndugu yangu katoka mkoani kaja kununua mzigo kariakoo akaniomba nimsindikize yeye ni mgeni, tumeenda tumenunua kurudi tupande bus tena sioni kituo dah alinikejeli eti "nilidhani wewe ni mwenyeji kumbe mshamba tu kama mimi"😂😂 hadi tukaulizia kituo kilipo ndiyo tukaoneshwa.

Siku nyingine naenda kariakoo huku congo, hilo bus linaenda Machinga complex! Tumeshushwa hapo sielewi nimeuliza naambiwa nenda njia ile dah naendaa hata sifiki aah nikachukua boda kumbe nilikua nimevuka congo bila kujua naenda mnazi mmoja hivooo😂
🤣🤣🤣🤣kariakoo Haina mwwnyeji
 
Back
Top Bottom