Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Kwa kuwa ni shuhuda ntatoa yangu ,Ila staki pm au judgement, haya ni mambo yaliyopita tulifanya ,tusiaemane vibaya.

Kisa Cha kwanza kilitokea 2010 hapo, nlikuwa kijana Sana Ila mganga huyo yupo Ila jina wala namba sitoi. Nlikuwa nauza spare parts za Mercedes ,Faw ,Howo n.k kwa duka la jamaa kutoka turkey hapa dar,nenda keko uulize jina la Mchopa wa spare parts utapewa story ucheke uanguke .
Ss nlikuja kujua kazi nikataka kumpiku boss, mshkaji wangu akanieleza kuhusu mganga fulani Chipu, Sumbawanga mpaka namba nikapewa. Yule mshkaji alipofatlia nkajidai mambo ya mganga staki Ila kimya kimya weekend moja nlisepa kwenda kule mwenyewe .
Ikumbukwe mkoa wa rukwa wala sumbawanga nlikuwa sijawahi kanyaga, nliposhuka stendi nkaulizia kuulingana na maelezeo ya yule braza mpaka kijiji nkakipata , nikiwa almost kufika kwa yule mganga (sitaki kumtaja jina) nlipatana na mbwa alikaa Kama amechizika hvi ,aisee nlitoka mbio akinifukuza ,nliingia ndani ya compound nkihema nikipiga kelele ,kukatokea yule mganga akamfukuza tule mbwa Kisha kunipa karibu .
Kufupisha, Mzee aliniongoza kwa kichaka chake nkapata jiwe limeegemea mti kando Kuna kijumba kidogo na hapo tulipokaa nakumbuka kulikuwa na kisu kina damu Yaani kichafu ,dhahiri kuonyesha kafara watu walikuwa wanafnya pale.
Kimbunga kilianza pale Mzee aliponiuliza ntakacho nkamwambia nataka kumzidi boss niwe tajiri, akaongea mambo yake Kisha lile jiwe likageuka bibi kikongwe ,alinipa kile kisu akaniambia Kama mm ni jasiri na nataka Mali nichukue kisu kile kisha nifuate kinjia fulani kulikuwa hapo ,kile ntapata kife.
Kushika njia Ile nlipatana na kuku nkampita sikushkanisha ,nilipoendelea mbele bila kupata kitu nkakumbuka nliambiwa kile ntapatana nacho ,nilirudi faster Sana.
Mzee yule kuku tulikimbizana ktk ya nyasi ile kumshika nlikata bawa ila akapepea na hio moja mbali sikumpata ,hii tukio ilipita Kama 2 hours hvi nikimkimbiza kuku yule.
Kurudi nlipata kile kibibi kinacheka balaa,nlirudi nimeshika pande LA bawa nlilokata natoka jasho sana ,akaniambia mwanangu una roho ngumu ,nenda mambo yako yatakuwa sawa ,Ila nisiwai kula kitimoto.
Long story short pale keko nilichakata mbususu nyingi Sana Tena Sana ,yule bosi alipanda ndege na familia Yao hawajarudi mpaka leo aisee .
Aliyopo pale kwa ss nijamaa anaitwa shafa ,anauza matunda kando Kuna stationary ya jamaa anaitwa dula wananikumbuka Sana tu .
Nlikuja jisahau nkala sausage one day nkiwa na Dem fulani kisu ,wanawake Yaani wapuzi ,aliponilisha tu moyo ulipasuka nkakumbuka vile nliambiwa , kila kitu kilienda na hewa mpaka zile pisi nlizokuwa zanikimbiza ...Ila nlijenga nyumba moja kubwa Sana mpaka Leo wazazi na dada zangu wanaifaidi , ujana aisee stosahau .
Leo hii nishamaliza masomo nina Mali Ila sijafikia enzi zile .
Walioko keko nenda kwa dula , au Rick Ross bonge fulani anaendesha bajaji pale ,muulize jina Mzee wa mbususu au Mchopa wa spare utapewa bonge LA story kunihusu enzi hizo .
Kwa nliowakosea enzi zile ,nisameheni Bure ni kiburi cha pesa tu na ujana , uchawi upo Ila Kama unajua kuplay smart nao
Hukuua kitu na ulilipa shingapi na je keko gani unaiongelea
 
Ni story kweli ya jamaa yangu wa karibu sana.

Mkewe alianza kuumwa pressure akiwa na ujauzito wa miezi 6.

Wiki nyumbani, wiki hospitali yalikuwa ndiyo maisha yake.

Tulifikia wakati tulishauri daktari atoe mimba mama apone. Daktari alikataa kabisa. BP ilikuwa inapanda hadi 180.

Huwezi amini, alijifungua salama japokuwa mtoto alikuwa njiti.

Cha ajabu, baada ya kujifungua tu, tumbo lilijaa mara mbili ya alipokuwa na mimba. Alivimba miguu kiasi cha kushindwa hata kusimama. Daktari anasema licha ya hali hiyo, hawaoni tatizo lolote katika kupima na hata BP imerudi hadi 110.

Ikawa mshikemshike, hali tete. Si mgonjwa wala watunzaji na daktari mwenyewe tumekata tamaa. Ndipo mmoja wa ndugu akasema nitatenda dhambi mgonjwa apone.

Alikuwa mkristo wa imani ya juu. Wale wa kusali na kulala kanisani. Alikwenda kwa witch doctor. Hakupewa chochote zaidi ya kuambiwa arudi hospitali na kwamba atajua yeye cha kufanya na mgonjwa baada ya saa 3 atasimama.

Alipofika hospitali mgonjwa alishazima. Anasubiriwa tu akate moto.

Baadaye akawa kama ameshtuka fulani, akafungua macho. Akaonekana kurejea uzimani.

Kweli baada ya saa 4 hivi, mgonjwa aliweza kusimama kwa kujitegemea. Akawa mzima tena.

Sote tulimwamini yule witch doctor. Shemeji yetu mzima hadi leo, tena kwa gharama ya sh. 30000/= tu.
Unataka upige mtu nn hahahaha
 
Yupo bibi anatibu vidonda vya tumbo pamoja na wale wadada ambao wakipata mimba zinatoka au hawapati mimba nilimpeleka jamaa alikuwa anaumwa pumu ikimbana mpaka sindano ndio apate nafuu alitumia dawa week akapona kabisa ajabu hakuwahi kumpa hata soda yule bibi Sasa sijui huu ni uganga au niiteje
Mkuu pumu inanisumbua mno, nipe connection ya huyo mganga
 
Kuna siri gani kuhusu kitimoto,mana waganga wanaikataa na huku kwenye dini za wazungu na waarabu wanaikataa,
Kitimoto na bangi inaangusha nguvu za Giza kabisa Yaani ,Mungu alitupa silaha Ila wengi hawajui ,ukiwa unasumbuliwa na jini ,uchawi au Chuma ulete ,pika na ule tu kitimoto au chukua majani ya bangi weka kwa maji uoge nayo ,Mzee mapepo yanasepa kabisa . Utakuta wengi wanaliwa na mganga Bure Hela
 
mimi nina babu yangu na uzuri anajulikana sana sana viunga vya mwahako,mwakidila,bagamoyo na mchukuuni hata mwarongo alikotokea mama kimbo wanamjua sana sana ni maarufu

Kisa chenyewe, nina ndugu zagu arusha walikua wana jirani yao anaumwa maradhi ya kuchanganyikiwa, yan vikipanda ni wa kufunga kamba,bas sjui ilikuaje mana ilitokea tu nilimpigia kaka angummoja akanambia sista niko tanga ila niko ndani ndani maramba huku nikimaliza nitakucheki nije nyumbani tukaongea kidogo tukaagana hapo hakunambia kilichomleta tanga bila taarifa ni nini

bas sku ya pili yake akanipigia akaniambia wamemleta mtoto wa jiran yao kwa mganga lakini wapo muda karibu wiki ila hawaoni nafuu yoyote zaidi ya kupoteza pesa hapo wazo la huyo babu yangu halikunijia nikamueleza mama yangu juu ya mkasa wao mama ndio kunikumbusha akanambia kwa nini usiwapeleke kwa babu yako wakajaribu mimi sasa nikamwambia mama mh wasipofanikiwa si yatakua yale yale lakini moyo ukanisukuma wasaidie kuwapeleka

nikampigia kaka nikamwambia kam vipi waje mjini tufunge safar kwa huyo babu kweli walikuja tukaenda tukiwa mimi, kaka zangu wawili,mgonjwa na mama yake,lakini kabla hatujatoka nikampigia babu nikamuuliza kama yupo kuna watu wana shida akanambia nipo njoo tukaenda

tulimkuta nje akatukaribisha ndani tukaingia kilingeni kwake, nikawatambulisha then wakaanza kujieleza shida yao bas babu alichukua tu karatas nakalam akawa anamuangalia yule kijana anaandika akanikabidhi list akanambia hizi ni dawa nazitaka lakini utakayokosa nipigie nendeni maduka ya dawa za asili tena akanambia ziko ghali lakini kazitafteni hizo dawa , tukarudi nyumbani mimi na kaka zangu hao had ngamiani sokoni kuna duka maarufu kwa dawa za asili katika ile list kulikua na mbegu za bangi na dawa kama mbili ambazo wao hawana muuzaji akanambia hizi hatuna, palepale nikampigia babu kumpa mrejesho akanambia nunueni zilizopo hizo nyingine ntazitafuta tukanunua tusirudi nyumbani straight had kwake tukaziacha akasema njoni kesho mje chukua dawa zenu

hio siku jioni yake vikapanda ambapp kesho ndio tukachukue dawa kaka wa watu katoka barabarani ikapita carry akaipanda kwa nyuma, ifahamike huyu kaka ni mgeni, hajawah kufika tanga yeye wala mama yake, hajui anaenda wapi lakini kulikua na watu walimuona wakatupigia kelele yule mgeni wenu amepanda gar inaelekea barabara ya pangani ikabidi kaka zangu wachukue boda kuiwah wakaikuta njiani wakaipigia honi wakasimam wakamchukua mgonjwa wao wakamleta ikabidi afubgiwe chumbani, ni alikua anaongea usiku kucha ukilala ukiamka unamsikia anaongea anaitaja majina yake matatu kwa kurudia rudia kulipokucha baada ya chai tukabebana had kwa babu akapwa za kupaka,za kujifusha za kuoga za kunywa

alitumia mchana na jioni hio siku alilala vibaya mno na kule kwa babu mimi ndio nikawa nauliza tatizo nn babu akajibu huyu ana mtoto wa kijini kichwani sasa alivuta bangi na huyo jini hapatan nazo ndio anamletea hizo shida hakutaka hata mia moja alichojibu akasema akimaliza hizo dawa babu apewe taarifa kuna watu hawana ustaarabu tangu waondoke kurudi arusha had leo kimyaaaaa

Namba za babu plz
 
Endelea kuhusu jamaa mlimpeleka au
Yap mganga alitoa amri ya kwamba mtuhumiwa asithubuku kupigwa kwasababu alijua wazi endapo tungempiga basi kesi ingekua kwake sababu yeye angekua ndio chanzo cha yote so tulichokifanya tulimpeleka kwa mganga akapewa onyo baadae tulimpa taarifa mzee wake kua kijana wako amekutwa na tuhuma za wizi baadae mzee wake alimuamisha shule.
 
Ilikuwa Ujiji. Nimepigika kinyama mimi na mwanangu Q. Ghafla mbele yangu naona bango la Uganga, kwa maelekezo hakukuwa mbali na pale. Tunafika tunapisha na wateja ( kama sikosei ni mtu na wakeze ).
Yule Mganga alikuwa ni mwanamke! Basi baada ya salam akaanza makeke yake, shida zetu akazipatia Mule mule toka mwanzo wa Safari yetu mpaka ile siku tunafika kwake! Shida ikawa moja tu! Anataka 40000, sasa nikajiuliza yaani huyu Bazazi ameona yoote lakini kashindwa kujua kama hatuna ata mia? Nikamwambia fresh Mmama we tufanyie kazi sisi tutakupa 60000 sio hiyo 40000, basi ile kainuka tu kuingia ndani kuchukua madubwana yake, mimi nikakusanya pesa 45000 zilikuwa pale kwenye ungo na kinokia Obama nikamwambia Q mwanangu hii nauli tusepe. Tukatokomea hivyo yaani mpaka Mwaloni. Tukauza kale kanokia 15000 jumla tukawa na 60, tukala 7000, tukalipia boti 6000 kwa kila mmoja. Kufika mbele mbele huko kuna kijiji kipo ndani ya Gombe, mida ya saa 1:30 ile Boti inazama, tunatumbukia kwenye lile ziwa, maji naanza kuyaona meusi mwanangu hajui kuogelea anakaba shingoni anaogopa kufa, hali inazidi kuwa tete kila nikijitahid anishike japo ukosi wa shati yule maaluni kakaza kabali......sitosahau. yule mama alitupiga kitu kizoto. Siiendelezi naishia hapa.
Unazngua malizia
 
Back
Top Bottom