Umewahi kusikiliza story za vijiwe vya bodaboda?

Umewahi kusikiliza story za vijiwe vya bodaboda?

hoof eater

Member
Joined
Jun 11, 2024
Posts
35
Reaction score
71
Habari za wakati?
Pengine kwa umri wako,nafasi au ufinyu wa muda ulionao umekupelekea Kutowahi kukaa ata dakika moja kwenye vijiwe vya bodaboda, basi zifuatazo ndio mada au agenda pendwa kwenye vijiwe hivyo.

Tips za kubeti;
kama we ni mdau wa betting hususani kwenye upande wa soka, basi jaribu kutembelea kwenye vijiwe vya bodaboda utakuja kunishukuru. Hawa jamaa wanafatilia ligi zote duniani na wajua timu nyingi sijawahi kuona, huku ndipo kuna mashabiki wa kisampasa ya uturuki, huku ndio unakuta mtu anaijua 1st eleven ya FC Basel.

Wake za watu;
Bodaboda wana siri sana, ila ukijichanganya kwenye vijiwe vyao siku mbili tatu, utajua mke wa nani analiwa na nani na mke wa nani anaenda guest gani? Yaani unaweza kukuta wanamjua mke wako kuliko unavyomjua wewe, aisee usiwadharau. Kiufupi wanaongoza kujua michepuko ya watu wengi wa mitaa husika especially wakina mama.
Ukisikia manzi yako anakwambia ana boda wake, basi ishi vizuri na huyo boda wake utakuja kunishukuru.

Wasanii wa bongofleva;
Kwenye vijiwe vya bodaboda hua kuna takwimu za ajabu sana za wasanii, yaani huku utaambiwa mpaka bei ya kiatu alichovaa diamond kwenye wasafi festival ya mwaka jana, bado ubishi wa mond na kiba nao haumalizi week mbili unaibuka.

Story ambazo ni nadra sana kuzisikia kwenye vijiwe vya bodaboda ni story za siasa, hawa jamaa unaweza kuwawekea 10000 wakutajie nafasi ya doto biteko serikalini na wakashindwa. Na hii ndio sababu wanatumika sana na wanasiasa unapokaribia wakati wa uchaguzi.

Usilojua kuhusu bodaboda hawa ndio wameukuza mziki wa singeli mpaka hapa ulipofika leo.

Niambie wewe umesikia story zipi kwenye vijiwe vya bodaboda.
 
Kivipi wameukuza
Wakati singeli inaanza bongo kwenye miaka ya 2010's huku maproducer wa mtaani wakitumia sampling za kwenye visual DJ. hakuna media iliyokua tayari kuupokea mziki huu kutokana na nature ya production lakini pia maudhui yake, ikumbuke walisample beat za taarabu mara nyingi, sasa kilichotokea ni kwamba bodaboda ndio waliupeleka huu mziki mjini kwa kuupiga sana kwenye pikipiki zao na kwenye vigodoro.

Ikumbukwe huu mziki ni wa uswahilini na ulisapotiwa sana na kizazi cha uswahilini ambacho 90% ndio kimezaa hawa bodaboda.

Mwisho kabisa wasanii wa awali wa singeli walikua ni mabodaboda na ma dj wa vigodoro achana na hawa wasanii wa mainstream waliokuja kucheza na fursa baada ya kujua kuna wimbi kubwa la mashabiki kwenye aina hii ya mziki.
 
Kuna boda waliitwa petrol station wakajaziwa mafuta ilikua ziara ya katibu mkuu wa ccm , nikakutana nae namuuliza kiutani naona leo uko full tank akajibu, sijui wamesema tukampokee nani anakuja ni kama mbunge au diwani wa mbelembele huko, nilicheka sana
 
Kuna boda waliutwa petrol station wakajaziwa mafuta ilikua ziara ya katibu mkuu wa ccm , nikakutana nae namuuliza kiutani naona leo uko full tank akajibu, sijui wamesema tukampokee nani anakuja ni kama mbunge au diwani wa mbelembele huko, nilicheka sana
Hahahah ndio maana nimesema wanatumika sana na wanasiasa kusababu ya uwelewa wao mdogo wa kwenye masuala ya siasa.
 
Nioneshe timu inayoitwa kisampasa nikupe elfu tano sasa hivi
IMG_20240615_110301_010.jpg
 
Back
Top Bottom