Ummy Mwalimu apiga marufuku kulazimisha watu kuchanja, Watanzania waliochanja wamefika milioni 8.5

Ummy Mwalimu apiga marufuku kulazimisha watu kuchanja, Watanzania waliochanja wamefika milioni 8.5

Kwani malimao, tangawizi na vitunguu swaumu vimeisha! Hiyo ndiyo dawa ya uhakika kabisa ya huo mlipuko.
I stand with GwajBoy that awepo wasio chanjwa na waliochanjwa hili ikitokea waliochanja wakawa mazimwi basi wasiochanja waendeleze taifa.
 
Watanzania hawataki chanjo ya uviko 19, wanataka dawa za Ukimwi tuu.
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameendelea kupiga marufuku tabia za Watoa huduma kulazimisha wananchi wanaoenda kupata huduma za afya kulazimishwa kuchanja, ameeleza kuwa tabia hiyo ni kinyume cha miongozo na maadili ya taaluma za Watoa huduma.

Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kujitokeza kupata Chanjo ya UVIKO-19, hasa watu walio katika hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo kama vile wenye magonjwa sugu (Shinikizo la damu, kisukari, magonjwa, saratani, UKIMWI n.k) na wazee.

Amebainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya imelenga kufikia asilimia 70 ya watu waliochanja ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Dunia wa kupambana dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Ameyasema hayo wakati akiwa na Waziri wa TAMISEMI na Mwakilishi kutoka Wizara ya fedha katika Mkutano na Katibu Mkuu Msaidizi na Mratibu Mkuu wa Kimataifa wa mapambano dhidi ya UVIKO-19 kutoka Umoja wa Mataifa Dkt. Ted Chaiban aliyeambatana na wajumbe kutoka WHO na UNICEF.

Ameongeza kuwa mpaka kufikia Aprili 5, 2022 tayari watu milioni 8.5 wameshapatiwa Chanjo ya kupambana dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 na kuweka wazi kuwa, bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuweza kuchanja watu waliobaki ili kuweza kuishi na ugonjwa huo kama magonjwa mengine.

Source: Voice of Bongo
ASANTE STUDIO. WIKI MBILI ZIKIZOPITA ALITUAMBIA WALIOCHANJA NI LAKI SABA NUKTA 8. LEO NI MIL 8. ! IKO VYEDI HII
KAZI IENDELEE
 
Back
Top Bottom