Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
UMOJA wa Afrika (AU) umeifungia nchi ya Niger kushiriki katika shughuli zote zinazohusiana na muungano huo kutokana na mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa mwezi uliopita.
Kitengo cha amani na usamala katika umoja huo kimetoa wito kwa nchi wanachama wa AU kujiepusha na masuala yoyote yanayoweza kuunga mkono na kuidhinisha mapinduzi ya kijeshi na Niger.
Umoja huo pia umesisitiza wito wake kwa viongozi wa kijeshi nchini Niger kumuachia huru Rais Mohamed Bazoum aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia.
Jumuiya ya nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS), umetishia kutumia nguvu za kijeshi kumrejesha madarakani rais Bazoum.
Kitengo cha amani na usamala katika umoja huo kimetoa wito kwa nchi wanachama wa AU kujiepusha na masuala yoyote yanayoweza kuunga mkono na kuidhinisha mapinduzi ya kijeshi na Niger.
Umoja huo pia umesisitiza wito wake kwa viongozi wa kijeshi nchini Niger kumuachia huru Rais Mohamed Bazoum aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia.
Jumuiya ya nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS), umetishia kutumia nguvu za kijeshi kumrejesha madarakani rais Bazoum.