Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Taarifa iliyotolewa kwenye mkutano ya kamati ya amani na usalama ya Umoja wa Afrika imeeleza wasiwasi mkubwa kuhusu uvamizi wa nzige wa jangwani ulioanzia mwezi Juni mwaka jana na kuendelea kuziathiri nchi za Afrika Mashariki
Wameonya kuwa tatizo hilo huenda litakuwa janga la bara nzima kama hatua za haraka hazitachukuliwa.
Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa pia wameonya mapema kuwa kuzaliana kwa nzige wa jangwani kutaendelea katika Eneo la Pembe ya Afrika, na kusababisha ongezeko la idadi ya nzige katika nchi za eneo hilo na kuwa na makundi mapya ya nzige katika mwezi Machi na Aprili.
Wameonya kuwa tatizo hilo huenda litakuwa janga la bara nzima kama hatua za haraka hazitachukuliwa.
Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa pia wameonya mapema kuwa kuzaliana kwa nzige wa jangwani kutaendelea katika Eneo la Pembe ya Afrika, na kusababisha ongezeko la idadi ya nzige katika nchi za eneo hilo na kuwa na makundi mapya ya nzige katika mwezi Machi na Aprili.