Umoja wa Mataifa: Watu milioni 27 wanakabiliana na njaa DRC

Umoja wa Mataifa: Watu milioni 27 wanakabiliana na njaa DRC

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

drc


Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa yamesema theluthi ya wakazi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanakabiliwa na njaa kali na wametoa wito wa kuongezewa fedha za dharura ili kukabiliana na janga hili.

Shirika la chakula duniani (WFP) na shirika la chakula na kilimo yamesema , hali haijawahi kuwa mbaya kiasi hiki kwa kuwa na raia wa Congo zaidi ya milioni 27 ambao wana uhitaji wa chakula kwa haraka- hii ni idadi kubwa ya watu kuliko eneo lolote lile duniani.

Lakini mashirika hayo ya UN yameelezea ukubwa wa janga kuwa ni wa kushangaza na kusema DRC inapaswa kuwa na uwezo wa kulisha watu wake na hata kuuza nje chakula cha ziada.

Migogoro ndio chanzo cha njaa hiyo haswa katika jimbo la mashariki ambako kuna makundi ya waasi ambao wanafanya mashambulizi kila mara.

Hali ni mbaya katika jimbo la Kasai ambako kulikuwa na ghasia pia.

Mashirika ya UN yamesema janga la virusi vya corona pamoja na uchumi kushuka pia kumechangia kufanya hali kuwa mbaya zaidi.
 
majeshi ya umoja wa mataifa yaondoke DRC.

Tanzania waruhusu tuivamie kijeshi mistu yote ya Congo.

Kupambana na hao wahuni
 
Back
Top Bottom