Umoja wa Ulaya Wasaini Makubaliano Kuendeleza Maendeleo Endelevu Zanzibar

Umoja wa Ulaya Wasaini Makubaliano Kuendeleza Maendeleo Endelevu Zanzibar

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
NEw_117.JPG
Umoja wa Ulaya (EU) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamesaini makubaliano mawili muhimu yanayolenga kukuza maendeleo endelevu, uhifadhi wa bahari, na usawa wa kijinsia.

Makubaliano hayo yalisainiwa mbele ya Riziki Pembe Juma, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; Rita Laranjinha, Mkurugenzi Mtendaji wa Masuala ya Afrika wa Huduma za Nje za Umoja wa Ulaya; na Hans Stausboll, Kaimu Mkurugenzi wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya Kanda ya Afrika, pamoja na maafisa waandamizi wa serikali na wadau wa maendeleo.
NEw_134.JPG
Makubaliano ya kwanza, yenye thamani ya TZS bilioni 32 (€ milioni 11), yanahusu uhifadhi wa bahari kupitia Mradi wa Bahari Yetu. Mradi huu, unaotekelezwa na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira (IUCN), unalenga kushughulikia changamoto muhimu za kulinda rasilimali za bahari, kukuza uvuvi endelevu, na kupambana na uchafuzi wa plastiki.

Aidha, mradi huu utaziwezesha jamii za Zanzibar kiuchumi kwa kuanzisha fursa za maendeleo endelevu huku ukihifadhi bioanuwai tajiri ya bahari ya Zanzibar.

Makubaliano ya pili yanatenga TZS bilioni 8.8 (€ milioni 3) kupitia mpango wa Umoja wa Ulaya wa Gender Transformative Action Zanzibar, unaotekelezwa na UN Women kwa kushirikiana na wizara inayohusika na masuala ya jinsia Zanzibar. Mpango huu unalenga kuondoa vikwazo dhidi ya haki za wanawake na kuimarisha nafasi za uongozi wa wanawake katika sekta za umma na binafsi. Aidha, mkazo mpya utawekwa kwenye kukuza elimu ya wasichana, hususan elimu ya juu.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bi. Laranjinha alisema: “Makubaliano haya yanaonyesha dhamira ya Umoja wa Ulaya katika kuleta maendeleo Zanzibar, hususan katika sekta za uchumi wa buluu na kuimarisha usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.”

Kwa upande wake, Stausboll aliongeza: “Makubaliano haya ni ushuhuda wa dhamira ya Umoja wa Ulaya ya kuleta manufaa na maendeleo ya kudumu kisiwani Zanzibar. Miradi hii italeta ustawi wa pamoja,, na ujumuishaji wa kijamii.”

Awali, Laranjinha na Stausboll walifanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, kabla ya kushiriki hafla ya utiaji saini. Mnamo tarehe 10 Desemba, wanatarajiwa kushiriki katika Mazungumzo ya Ushirikiano kati ya Umoja wa Ulaya na Serikali ya Tanzania, hatua inayotegemea kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu na kushughulikia vipaumbele vya pamoja vya pande zote mbili.

Usuli:
Umoja wa Ulaya nchini Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mdau muhimu katika ushirikiano na Tanzania pamoja na Afrika Mashariki. Umoja wa Ulaya imeanzisha mkakati wa Global Gateway ili kukuza nadhifu, usafi na usalama wa kijitali, sekta za nishati na usafiri pamoja na kuimarisha afya, elimu na mfumo wa utafiti duniani kote. Mkakati wa Global Gateway unatekelezwa kwa pamoja chini ya timu ya nchi za Ulaya, ambazo ni taasisi za Umoja wa Ulaya na Nchi Wanachama wake.
 
Back
Top Bottom