Umri unaenda, nachanganyikiwa

Wala usijali kabisa, umuhimu wako kwenye ardhi hii ya dunia ni mkubwa mno kuliko unavyo dhani, huenda maisha yasinge kuwa hivi yalivyo kama usingekuwepo wewe mleta mada.

Katika hali ya kawaida kwa maisha ya mwanadamu yoyote mawazo kama haya hayana budi kuwepo haswa kwa mwenye jaliwa la akili inayochanganua, kuna msemo usemao wasiwasi ndio akili, I wish kuongea nawe private , lakini ujumla wa yote ondoa negative think , maisha ni mazuri sana.
 
Miaka 27 si mingi na si midogo.

Kila mtu na wakati wake na wakati wa Mungu hauchelewi.
 
Unamshukuru Mungu kwa matatizo ya wengine ambayo wewe huna?
Huo ni ubinafsi, roho mbaya na yawezekana wewe ni sadist mkubwa.

NB: Tuendelee kukataa dini, hasa za kikoloni na mambo yake yote.
 
MIAKA YANGU 27 INANITETEMESHAAAAAA

Kijijini kwenu wazazi hawana ardhi, mashamba, mifugo, mitumbwi, nyavu n.k

Jamii zingine kama za watanzania wenye asili ya Kiarabu, Kihindi, Kisomali vijana hutegemewa kuendeleza pale walipoishia wazazi.

Hili suala la kukimbilia mjini wakati wazazi hawana chochote walichowekeza mjini lakini kijijinj wana mali nilizotaja hapo paragraph ya pili ni kujiita masikini wakati siyo kweli baba wa babu alimrithisha babu, naye babu yako akamrithisha baba yako mali hizo kijijini.

Lakini wewe umezipuuza kukimbilia mjini kutaka kuigiza familia ambazo tayari walifika mjini kitambo unataka kujifananisha nazo, hilo ni kosa kubwa.

Rudi kijijini ukaendeleza pale wazazi walipoishia, ya mjini waachie ambao wazazi wao waliwekeza kitambo na usisononeke kuona wenzio wana majumba, ardhi, daldala, kampuni n.k mjini ukataka kushindana nao. Wa mjini wameachiwa na wazazi na kuendeleza.

Kifupi wewe siyo masikini, lakini hufahamu hilo. Rudi haraka kijijini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…