Umri wa mtoto kuweza kujisadia sehemu husika

Mfundishe taratibu ataelewa...hakikisha siku unazokuwa nyumbani unamfundisha na dada wa kazi akiwepo ili ajue kuwa hilo nalo ni jukumu lake.
 
kuendelea kumvalisha pampa pia mtu wa miaka 2 na nusu siyo sawa, mtafutieni vikaptula vingi, akijojoa mnambadilisha, hiyo pia imemlemaza!
 

vizuri sana,mi wa kwangu kwa kweli huwa nawaanzishia wakiwa na miezi minne kuwaweka kwenye poti akifikisha mwaka na nusu hata kitandani hakojoi anakuwa amesha jicondition huwa naamka usiku kuwakojolesha.
 

Aisee umenisaidia sana maana nimeumiza sana kichwa na mwanangu anafika miaka miwili mwezi wa tano lakini kamechangamka mapema
 
Kuna jamaa aliwahi niambia, "alimtrain" mwanawe kipindi kirefu kutumia "pot" bila mafanikio, siku moja akamweka mwanawe pembeni ashuhudie akakaa yeye kwenye "pot" akadondosha mambo! "Pot" lilivyosafishwa tu, halikupita saa moja mtoto nae akalikalia akapiga mambo...baada ya hapo usiulize, mtoto na "pot", "pot" na yeye...

Sometimes creativity matters alot...
 
Mfundishe taratibu ataelewa...hakikisha siku unazokuwa nyumbani unamfundisha na dada wa kazi akiwepo ili ajue kuwa hilo nalo ni jukumu lake.


Ushindwe kumlea mwanao afu unakuja kifua mbele Eti dada wa kazi ajue kua ni jikumu lake
Lolz............mama ndie mwenye jukumu lakujua mwanae anakula nn.....analala wapi.....choo chake kikoje anapata choo kizur?

Lakn cha ajabu wanawake wanakwepa majukum yao na kuwapatia wadada wakaz lol kwa sh ngap haswa mnayowalipa
 
Mfundishe tu ataelewa kidogo kidogo
Umleavyo.ndivyo akuavyo
 
ngafu . . . .
Pole mwaya, japo umechelewa kumuanzishia kidogo sio mbaya sana. Anza sasa hivi ili akifikisha miaka mitatu umuachishe kabisa hizo diapers(kwanza zinakula hela sana).

Watoto wanajifunza vitu kwa mazoea. Wangu wa miezi 14 last week nilikuwa nimemvua nguo ili akaoge bahati nzuri muda huo huo akaanza kufanya mambo yake. Nikavuta poti haraka nikamkalisha aendelee pale huku namuongelesha "bebé anapupu, tulia -----, unapupu? Sema pupu" na kenyewe kanaitikia tu alafu kakaanza kusema pupu. Leo asubuhi alikuwa na diaper, akanifuata ananiambia "pupu,pupu" huku kanaendelea kufanya mambo yake kwenye pampers. Kwahiyo kameshajua kupupu ni kufanya nini, na kwamba kuna sehemu ya kupupia.

Tenga muda umfundishe mwanao. Usimpigie kelele wakati wa hilo zoezi, mfundishe taratibu kwa upendo huku unamuongelesha kuhusiana na hilo swala.

Tatizo wamama/hata wa dada wa kazi wengi (wale wenye hela ya diapers) wanakwepa hili zoezi kwa uvivu/kinyaa cha kudeal na pupu ya mtoto. Mtu anaogopa mtoto atapupu kwenye poti, chini ama kwenye nguo apate kazi ya kusafisha kwahiyo bora diaper. Akifanya mambo yake anamtoa tu na kumfuta na wipe amemaliza. Hata kuwanawisha na maji wanakwepa. Wanasahau kwamba kuvaa hizo pampers kwa muda mrefu ni adhabu haswa kwenye mazingira ya joto bila, kisababishi cha UTI haswa kama mtoto hasafishwi vizuri kila wakati, bila kusahau gharama. Hizo 4000, 5000, 12000 na 30000 unazonunulia diapers kila wiki/mwezi mnunulie mtoto hata toys tu afurahie.

Tusiwe wa mjini sana kwenye malezi ya watoto wetu. Kinyaa weka pembeni, mpe mtoto raha na uhuru wa kupata upepo kila anapokuwa nyumbani.
 
Last edited by a moderator:
gorgeousmimi nashukuru sana,nilianza kumzoesha mwanangu kutumia poti badala ya pampers na sahivi ameshazoea kabisaa hata ikitokea nimemvalisha pampers hajisaidii mpaka nimtoe hiyo pampers.
Ubarikiwe sana sana
Cc: Lizzy
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…