Umri wa mtu kuteuliwa kushika nafasi yoyote Serikalini uwe ni walau kuanzia miaka 35

Umri wa mtu kuteuliwa kushika nafasi yoyote Serikalini uwe ni walau kuanzia miaka 35

Miaka 30 is fair enough kama kuna Institutions imara za kuwadhibiti viongozi pale wanapoanza kukengeuka. Ushenzi wa mtu kama Sabaya na Bashite ukikuwa wazi awali kabisa ila wakalindwa (or rather wahusika wakaogopa kudeal nao kwa kuwa mteuzi wao alikuwa Rais na mtetezi wao)

Mtu mshenzi ni mshenzi tu hata akiwa na miaka 70
Kweli tupu, mtu kama Ndugai, Kabudi, Mwigulu hao ni vijana?
 
Akili ya mtu ni ya mtu tu na huwa inatofautiana kati ya mtu na mtu
Miaka 35 wewe ni mzee maisha yanaenda kasi sana
Watu wanaongoza kaya zao wana MIAKA 10 na kaya zimefika (Kaya zinazoongozwa na watoto)
Sasa kijeba huyu ana MIAKA zaidi ya 25 umepewa madaraka amembwelambwela tu
Hiyo ni tabia ya ulevi wa kawaida kabisa wa madaraka ambao haujalishi umri, jinsi, kabila, chama wala mambo yanayofanana na hayo wa mtu husika
Upo sahihi sn mkuu
 
Umezungumza jambo la msingi sana. Nafasi za kiutawala na uongozi wa juu unahitaji umri uliopevuka. Hivi ndivyo ilivyo, hata kwenye vitabu vitakatifu Mwenyezimungu aliwapa utume na unabii wale waliofikia miaka 40. Hii inamaanisha *Age matters. Bila shaka kuna haja ya kuliangalia hili kwa jicho la ziada kwa wenye mamlaka ya uteuzi.
Bahati mbaya watanzania tunapenda zaidi kujadili na tunatumia muda mwingi kujadili matukio na si chanzo au kiini cha matukio.

Ukiangalia kwa sasa utagundua vijana wengi ndio wanatumika katika kutenda maovu ya kiutawala kuliko wazee au watu wenye umri mkubwa ambao uovu au kasoro zao ziko kwenye mambo kama ya wizi na ufisadi lakini sio haya ya kuteka,kuvamia vituo vya tv/radio na mengine ya aina hiyo.


Hialii hii ni moja ya sababu ya ma-DC na mara- RC wengi vijana kulaumiwa kwa mambo kama kuweka watu ndani hovyo hovyo kinyume kabisa na sheria, au kutoa lugha za kutishia uhai na maisha ya watu wengine.
 
Kweli tupu, mtu kama Ndugai, Kabudi, Mwigulu hao ni vijana?
Ni kweli lakini watu kama Mwigulu, Ndugai na Kabudi huwezi kuwatumia kwa kuwapeleka field wakaongoze uporaji kwa kutumia silaha au kuvamia kituo cha utangazaji kama radio au tv.
 
Ni kweli lakini watu kama Mwigulu, Ndugai na Kabudi huwezi kuwatumia kwa kuwapeleka field wakaongoze uporaji kwa kutumia silaha au kuvamia kituo cha utangazaji kama radio au tv.
Hawapati muda tu lakini ni watu waovu vibaya sn Mwigulu amefanya maovu makubwa same to Ndugai
 
Bahati mbaya watanzania tunapenda zaidi kujadili na tunatumia muda mwingi kujadili matukio na si chanzo au kiini cha matukio.

Ukiangalia kwa sasa utagundua vijana wengi ndio wanatumika katika kutenda maovu ya kiutawala kuliko wazee au watu wenye umri mkubwa ambao uovu au kasoro zao ziko kwenye mambo kama ya wizi na ufisadi lakini sio haya ya kuteka,kuvamia vituo vya tv/radio na mengine ya aina hiyo.


Hialii hii ni moja ya sababu ya ma-DC na mara- RC wengi vijana kulaumiwa kwa mambo kama kuweka watu ndani hovyo hovyo kinyume kabisa na sheria, au kutoa lugha za kutishia uhai na maisha ya watu wengine.
Mbona Anthony Mtaka hajafika huo umri na ana hekima na busara kuliko hata Ndugai?
 
Naona wakati umefika tuweke kigezo cha umri kwa watu wanaoteeuliwa kushika nafasi au madaraka makubwa serikalini na katika Utumishi wa umma.

Katika nchi yetu, uteuzi hufanywa zaidi na Raisi na wateule wa Raisi wote hupewa dhamana au madaraka makubwa na hivyo kuna uwezekano baadhi hupewa madaraka makubwa kuzidi umri wao( wanakuwa hawajakomaa).

Vijana wengi wa kitanzania chini ya miaka 35 wanakuwa bado wanasumbuliwa na ujana na hivyo inakuwa rahisi kulewa madraka na pia ni rahisi zaidi kwa watawala wabovu kuwatu vijana kwa mambo yaliyo kinyume na maadili yetu na hata utu wa mwanadamu.

Mbali na kusumbuliwa na ujana( kupsndisha mabega, n.k) ni wazi pia watawala huwachukulia vijana wanaowapa madaraka kama watoto wao wa kuwazaa hivyo inakuwa rahisi kuwatumia kwa mambo ya hovyo.

Ukiacha katika majeshi ambako amri ndio hutawala hivyo inakuwa rahisi hata kuwatumia watu wenye umri mkubwa kufanya mambo ambayo ni kinyume na sheria za nchi na maadili ya kitabzania, nii vigumu kwa watawala kuwatumia wateule wenye umri sawa na wao kutenda mambo ya hovyo kama wanavyoweza kuwaagiza au kuwatumia vijana waliowapa madaraka.

Hivyo, japo si vijana wote wanakosa busara za uongozi na wanaoweza kutumika vibaya, napendekeza umri wa wateule wote wa Raisi nchi hii kuanzia walau miaka 35 na ikibidi zaidi ya hapo.

Najua wako vijana wanafanya vizuri tu katika uongozi, ila ni bora tuweke hiki kigezo ili kuondoa au kupunguza risk ya kuwa na vijana wanaotumika vibaya na watawala au kuwa na vijana ambao bado hawajakomaa kupewa madaraka makubwa ya kuteuliwa na Raisi au Mamlaka nyingine za uteuzi.

Vijana wengi wa kitanzania wa leo hii sio sawa na wale wa miaka ya nyuma walioweza kupewa madaraka makubwa na wasiwaangushe waliowapa madaraka.

Kuhusu viongozi wa kuchaguliwa, hiyo ni agenda nyingine ingawa bado agenda hiyo inaweza ku-fit hata katika hii mad na hivyo hapa sitaiongelea.

Nawasilisha.

Magu mwenyewe alikuwa above 55 lakini ndio alikuwa anaoongoza kwa ulevi wa madaraka. Makonda, Mwigulu nk hao wote wako above hiyo 35, unawaona walivyo na siasa za kishenzi?
 
Mwl Nyerere kawa Rais akiwa na miaka 38 lakini waliokuwepo wanasema hakuwai kufanya matendo ya kipumbavu na kihuni, Dr Salimu sijui aliteuliwa akiwa na miaka 22 kuwa Waziri lakini hakufanya upumbavu na uhuni, hizi ni tabia za watu, mwendazake alikuwa muuaji kwani alikuwa under 35?
 
Hawapati muda tu lakini ni watu waovu vibaya sn Mwigulu amefanya maovu makubwa same to Ndugai
Kama nilivyosema tangu mwanzo kwenye huu uzi, exceptions lazima ziwepo ila tunaangalia majority katika kundi la umri fulani wana-behave vipi kufikia conclusion.
 
Kama nilivyosema tangu mwanzo kwenye huu uzi, exceptions lazima ziwepo ila tunaangalia majority katika kundi la umri fulani wana-behave vipi kufikia conclusion.
Vipi marehemu mkuu tabia zake alikuwa under 35? na ndiyo hawa akina Makonda, Mnyeti, Sabaya wameiga kwake, shida ni kwamba hatuadai watu kuja kuwa viongozi tunaandaa watu kuja kuua wapinzani. Over
 
Vipi marehemu mkuu tabia zake alikuwa under 35? na ndiyo hawa akina Makonda, Mnyeti, Sabaya wameiga kwake, shida ni kwamba hatuadai watu kuja kuwa viongozi tunaandaa watu kuja kuua wapinzani. Over
Wewe mbona huelewi?Unaelewa maana ya watawala kuwatumia vijana kufanya uovu?Hao uliowataja huoni wako Katika kundi hilo?
 
Hapa tunazungumzia aghalabu ya mambo. Mtu mzima (mwenye umri mkubwa) kuna mambo yanaendana na yeye na haitegemewi yeye kufanya baadhi ya mambo. Na hii haimaanishi kwamba hakuna hao watu wazima wenye kufanya mambo tofauti. Kwani kwenye msafara wa mamba na kenge pia wamo. Kwa mfano hatutegemei kwa watu wenye umri wao wenye madaraka wakakutwa night club wakigombania wanawake (madada poa) wakati hili jambo kwa vijana wenye umri wa kati kwao wanaona ndioa life style. Kwa hiyo tuweke angalizo kwamba tunaposema umri uzingatiwe hatumaanishi kuwa hakuna wenye umri mkubwa ambao hufanya ufyororo wanaoufanya vijana...! Lakini karma ibaki pale pale kwamba Ifike wakati vyeo ktk nafasi za uongozi ziangalie na umri wa mtu.
Kama mtakumbuka niliwahi kusoma humu kuna mtu aliandika kuwa Mzee Kikwete alitaka agombee tangu awali lakini hekima za wazee zikatumika na kumtuliza na walichomuambia ni kwamba asubiri umri usonge kidogo..
 
Point.......

Vijana karibu wote 85 kuja huku mawazo yao yamekua Kama kuku broiler....

Sasa sabaya 34yrs mawazo mgando..... Anakuwa kiongozi wa wananchi wa wilaya nzima na anaact Kama kamanda mkuu wa genge la majangili.......

Mimi ni opposition in nature lakini nakubali watu the like ya January Makamba. Ukipewa madaraka jiamini, be calm sio kila saa Mimi nasema, watakiona, mtanikoma....

Bora hata Jokate anavyofanya.....yupo kwenye media Sana Ila unaona shule, vyoo na madawati.... Yaani ana positive impact kisarawe....

Sasa sabaya zaidi ya kueakandamiza chadema HAI..... Tuambiwe ni Nini tangiable effect yake pale.....

Kipi leo nikienda nikikiona kwa macho na kushika kwa mkono nasema huyu ni Sabaya..

Tena mnaosema 23 Salim Ahmed Salim alipewa u alozi niwaambie tu watoto wa kuanzia 90 kuja huku ndio useless kabisa......
 
Matatizo ya watu watatu yasiharibu hatma ya vijana wote wa Tanzania. Samaki mmoja akioza ni huyo huyo, labda aliteleza wakati wengine wanaingia kwenye friji
 
Hahahhhaa... Hilo sasa litakua taifa la wendawazimu..!!
Kwa nini liwe taifa la wendawazimu kuruhusu kila mtu kugombea bila kujali vyeti wala umri?

Kuweka vigezo vya umri na vyeti ni ubaguzi unaoashiria walioweka vigezo hivyo hawaamini uwezo wa wapiga kura kufanya maamuzi sahihi pale wanapopelekewa mgombea kijana asiye na vyeti na yule mzee mwenye vyeti. Kama ni kweli wapiga kura sisi hatuwezi kutanabahisha mgombea anayefaa mpaka Katiba ituchagulie, huyo msomi mzee anashindwa nini kuja kutushawishi tumchague?

Naamini wapiga kura ni watu wazima (miaka 18+) na ni wenye akili timamu, wenye uwezo wa kujua ni yupi mgombea sahihi wa kupewa kura.
 
Back
Top Bottom