Umughaka ni mtu wa kawaida tu ndugu zangu,ni deiwaka tu asiyekuwa na lolote

Umughaka ni mtu wa kawaida tu ndugu zangu,ni deiwaka tu asiyekuwa na lolote

UMUGHAKA

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2021
Posts
2,753
Reaction score
12,932
Nsikuchoshe na Usinchoshe, Tusichoshane!


Kuna Vijana baadhi ambao wamekuwa wakinifata pm Kwa kuniomba angalau niwape kazi au Vibarua kama vinapatikana!

Ndugu zangu, kwanza nawashukuru Kwa kudhani huenda Mimi UMUGHAKA naweza kuwasaidia, yawezekana ni taswira yangu hapa JF Kwa Vijana wengi ndio inapalekea hadi kuamini na kukubalika miongoni mwa Vijana wengi, Niwaambie tu ndugu zangu, Mimi pia ni muhangaikaji mwenzenu nisiyekuwa na lolote la maana!

Mimi binafsi ni muendesha Bodaboda tu ambaye ni deiwaka tu hapa mjini, uzuri ni kwamba huwa sichagui labda kazi inikimbie! Hivyo ndugu zangu siko kama mnavyonidhania! Huenda baadhi yenu mnaniona kama UMUGHAKA ni mzugaji tu atakuwa na kazi nzuri serikalini au kwenye taasisi fulani,hapana wanangu Mimi pia ni Hustler mwenzenu huku kitaani!

Niwaombe tu ndugu zangu ambao mnayajua machimbo ya Kazi za kideiwaka iwe UFUNDI, SAIDIA FUNDI, VIWANDANI, MASHAMBANI N.K hebu wasaidieni Vijana wenzenu maana Kuna Vijana hapa JF wanapitia msoto heavy,usione watu wanajichatisha hapa JF kila siku lakini Hali zao ni mbaya mno!

JF imekuwa ni sehemu ya kuwapatia faraja angalau kila wanapopekua nyuzi kadhaa,lakini kiukweli watu au Vijana wengi humu ndani Wana Hali mbaya! Tafadhali kama unaouwezo wa kuisaidia saidia bila kuwachoka Vijana!

Kama Kuna sehemu unapiga kazi za nguvu na bado nafasi zipo,basi washirikishe Vijana wenzio hapa JF Ili nao wakapambane,Vijana wanataka kazi lakini Kuna muda wanatafuta bila mafanikio,hawapaswi kusimangwa!

Kama Kuna fursa huko washitue Wana waje muipige wote,TUACHE UBINAFSI NA UCHOYO!
 
Kwa Dar es salaam wapite na kutembelea maeneo ya kisarawe2 wilaya ya kigamboni wakiwa na copy za vitambulisho vya NIDA, leseni za udereva au vitambulisho vya kura pamoja na barua za utambulisho za serikali za mitaa walipotoka au kuishi.

Kuna viwanda vingi vinatoa ajira kwa vijana wasio na ujuzi wowote.
 
Kwa Dar es salaam wapite na kutembelea maeneo ya kisarawe2 wilaya ya kigamboni wakiwa na copy za vitambulisho vya NIDA, leseni za udereva au vitambulisho vya kura pamoja na barua za utambulisho za serikali za mitaa walipotoka au kuishi.

Kuna viwanda vingi vinatoa ajira kwa vijana wasio na ujuzi wowote.
Safi sana Kwa Taarifa hii nzuri mkuu
 
haojamaa niwepesi kutapeliwa🤣🤣tangulini jitu limekalia stori zauongo likawa nakazi hadi liwape watu vibarua?
 
Tatzo la vijana wa humu sio waaminifu na wanajisahau sana baada ya muda ukishampa kazi anayoana kashayapatia hivyo kusahau misingi ya kazi uliompa,
Nilimsadia mtu hapa baadae akaanza kuniletea visheria uchwara kisa alisoma sheria, ubaya akanikuta mimi mwenyewe bush lawyer mzuri tu
 
Tatzo la vijana wa humu sio waaminifu na wanajisahau sana baada ya muda ukishampa kazi anayoana kashayapatia hivyo kusahau misingi ya kazi uliompa,
Nilimsadia mtu hapa baadae akaanza kuniletea visheria uchwara kisa alisoma sheria, ubaya akanikuta mimi mwenyewe bush lawyer mzuri tu
Usiwachoke Vijana Kwa baadhi ya Ujinga na Upumbavu wa Vijana wengine mkuu,saidia usichoke!
 
Kwa Dar es salaam wapite na kutembelea maeneo ya kisarawe2 wilaya ya kigamboni wakiwa na copy za vitambulisho vya NIDA, leseni za udereva au vitambulisho vya kura pamoja na barua za utambulisho za serikali za mitaa walipotoka au kuishi.

Kuna viwanda vingi vinatoa ajira kwa vijana wasio na ujuzi wowote.
Sawa, vizuri ukitaja kiwanda direct maana huko watu wamepita wakaambulia patupu labda kwa bakhressa buguruni ndo kuna mtindo huo.
 
Sio issue ya Jf Ila tatizo la ajira ni zito sanaa hata street ni kugumu sana

Wengi wetu bado ni jobless tu Ila tuna hustle kupata mkate wa kila siku... Kwa hiyo ndugu zangu

Msikate tamaa fosini hadi iwe
 
Sio issue ya Jf Ila tatizo la ajira ni zito sanaa hata street ni kugumu sana

Wengi wetu bado ni jobless tu Ila tuna hustle kupata mkate wa kila siku... Kwa hiyo ndugu zangu

Msikate tamaa fosini hadi iwe
Hakika mkuu
 
Back
Top Bottom